Nimechaguliwa kujiunga na AZANIA SECONDARY SCHOOL A-LEVEL 2023 wanaoijua mnisaidie hapa

Nimechaguliwa kujiunga na AZANIA SECONDARY SCHOOL A-LEVEL 2023 wanaoijua mnisaidie hapa

Advance,chuo ushubwada tumesoma lkn tunalia njaa wasomi kibao ajira kisodA
 
We inaonekana inapanda kichwani.
Nenda katuwakilishe.
Sema kule cheza kama pele, Physics ni S.Chand XI&XII. Achana na sijui Rogers , tumia Michael Nelkon pia.
Kuhusu vitini, usitumie achana navyo, focus na vitabu.
yeahp! hata kufika hapo napenda kutumia vitabu
 
Dah shule hizi zinachelewesha sana,Met wangu tuliyemaliza nae std 7 2003 ana mtoto wa 2004 yupo form 6 sasa hivi.
Nami ninhekuwa na kijana wa form 6 sasa hivi
 
Nilisoma hapo Azaboy advance ECA 2008-2010,tulikuwa tunakaa pale Hostel pembeni kuna watoto wa Zanaki na nyuma watoto wa Jangwani.

By that time Azaboy ilikuwa zaidi ya chuo kikuu Uhuru kama wote,hakuna Mwalimu anamfatilia mwanafunzi.
Tulikuwa tukiamka ni kwenda Maktaba ya Taifa au Ubalozi wa USA kusoma.
Kula kama una hela unaenda kula pale Muhas na wanafunzi wa chuo.

Jioni mnaenda Don bosco kucheza basketball ball au kwenda kuangalia mchezo wa golf kule Gymkan.

Asubuhi tunakimbia kuzunguka UN road,masaki na kuishia GYMkan beach pale tunaoga tuna rudi kusoma.

Usiku kuanzia SAA 4-7 tunazunguka mnazi mmoja, karikaoo na posta kuangalia Madada poa

Weekend tunaenda casinos za posta na kwenda sinza kwenye club za miziki.
 
ongea tu mkuu

Issue ya waalimu especially advance sio, uweke plan zako vizr usome tuition ukate topic. Nakumbuka Physics na chemistry nilisoma topic zote tuition maana waalimu walikua usanii mtupu.

Mimi ni kaka yako mkubwa nimesoma Azania kwa miaka 6.. ie A & O level.

Kwa hostel, ipo inayobeba wanafunzi wachache sana mostly advance floor moja juu na chini olevel wachache, ni vile hatulali masaa yote ni sehemu ya kubadilishia nguo[emoji3] utaelewa baadae!
 
Sipo kubishana najua nachokiongea , nimesoma moja ya shule tajwa hapo hivyo kama kanielewa atayafanyia kazi ila kama atakuwa mbishi ataenda atajiona na atakuja kukiri siku moja kwa kupitia huu huu uzi
Asante .
Mwache aje akapange Magomeni au Aje auziwe Hostel Muhas kwa laki 6.
Anataka boarding Dar aende Pugu vinginevyo awe na Ubalozi Jangwani hapo.
 
Nilisoma hapo Azaboy advance ECA 2008-2010,tulikuwa tunakaa pale Hostel pembeni kuna watoto wa Zanaki na nyuma watoto wa Jangwani.

By that time Azaboy ilikuwa zaidi ya chuo kikuu Uhuru kama wote,hakuna Mwalimu anamfatilia mwanafunzi.
Tulikuwa tukiamka ni kwenda Maktaba ya Taifa au Ubalozi wa USA kusoma.
Kula kama una hela unaenda kula pale Muhas na wanafunzi wa chuo.

Jioni mnaenda Don bosco kucheza basketball ball au kwenda kuangalia mchezo wa golf kule Gymkan.

Asubuhi tunakimbia kuzunguka UN road,masaki na kuishia GYMkan beach pale tunaoga tuna rudi kusoma.

Usiku kuanzia SAA 4-7 tunazunguka mnazi mmoja, karikaoo na posta kuangalia Madada poa

Weekend tunaenda casinos za posta na kwenda sinza kwenye club za miziki.
Wewe sasa ndiyo tunaongea ligha moja , unajua wengi wemeshindwa kumshauri dogo vizuri , wengi hawajui utofauti wa hostel na boarding , yani hapa dogo anavyosikia pale Azania pana hostel akili yake inafikiri pale Azania kupo kama kulivyo minaki au pugu kitu ambacho ni tofauti .

Wengi wamebaki kumwambia dogo sijui shule ipo town, kariokoo karibu mara cjui mademu wa zanaki na jangwani ni wazuri vitu ambavyo havita msaidia kabisa katika safari yake yakielimu .

Mimi nimemwambia maisha ya hosteli ni tofauti mnooo na maisha yale ya shule za bweni zilizopo mikoani , hivyo kuna gharama za ziada dogo lazima ajipange mfano wakati nikiwa katika shule mmoja hapo jijini ilitubidi pale hostel kujinunulia Unga na mboga kwa ajili ya kupikia na wale wenye uwezo wajuu wao walipewa pesa na wazazi wao kwa ajili ya kununua chakula . Watu waliomo humu hawamwambii huyu juu ya vitu kama hivi afu yeye ni pcb je maisha ya na mna hiyo atayaweza ingawa najua zipo baadhi ya hosteli ambazo watu hupikiwa sasa je hapo Azania watu waliopo hostel wanapikiwa ??? Je hosteli zipo ndani ya shule au ni za nie ya shule Maswali kama haya sioni dogo akiuliza yeye yupo bize kuwashangilia watu wanaomwambia habari za mademu wa jangwani na ishu za kariokoo afu ni PCB huyu mmhh ayaaa !!!! ...

Wengine wamenishangaa niliposema siyo shule za bweni lakini hapo hapo wakasema nafasi za bweni ni chache , wengine wakasema lazima utoe rushwa ndipo upate , wengine wakasema ni kwa ajili ya wanawake tu , sasa kwa mtu unayetumia akili hapa umeshajua hasa nini kinaendelea hapo , na ni hatua gani azichukue .
 
Hongera sana,
Nenda ukasome utapata exposure kubwa na nzuri maeneo ya kufika mjini na Kariakoo unatembea tu.

Utaona mengi,
 
Mkuu hongera na karibu United Nations (hilo ndilo jina la barabara iliyopo shule ya Azania).

Barabara hiyo ina shule kubwa kama Jangwani Girls Secondary School ambayo inapakana na Aazania, mbele huko kuna Tambaza High School.

Shule ya Azania imekaa sehemu nzuri sana mjini, kwenda mjini kabisa Dar au Kariakoo unatebea tu, ipo karibu na hospitali ya Muhimbili.

Sina uhakika kuhusu habari za elimu kwa sasa, nimetoka mitaa hiyo siku nyingi, lakini utapata huduma zote muhimu karibu.
Huu ndiyo uungwana. Hongera sana kaka Kiranga
 
Kama kichwa cha uzi kinavyosema, mimi nimemaliza form four mwaka jana hivyo form five selections zimetoka na nimechaguliwa kwenda Azania sec

Hivyo najua humu kuna watu wanaishi hapo karibu au wamesomea pale naomba mnipe hali ya maisha ya pale,ufaulu wake, n.k

Natokea mikoani na itakuwa mara yangu ya kwanza kuishi dar

Combination nimechaguliwa kusoma PCM

Natanguliza shukurani
Karibuni wajibu


Funny boe
Utaweza kweli Kutunza hela hasa Pocket Money?
 
Hakikisha mpaka unamaliza cha sita pale kariakoo unafahamika na wenye maduka kwa kuwa winga wao, then usiunge chuo endelea na mbishe hapohapo kko, utakuja kunishukuru bdae. Chuo utasomaga hata bdae.
Hivi winga maana yake ni nini mkuu? Nia hawa wanaotangaza simu status au?
 
Mwache aje akapange Magomeni au Aje auziwe Hostel Muhas kwa laki 6.
Anataka boarding Dar aende Pugu vinginevyo awe na Ubalozi Jangwani hapo.
Watu hawamwambii ukweli dogo
 
Back
Top Bottom