Nimechaguliwa kujiunga na AZANIA SECONDARY SCHOOL A-LEVEL 2023 wanaoijua mnisaidie hapa

Nimechaguliwa kujiunga na AZANIA SECONDARY SCHOOL A-LEVEL 2023 wanaoijua mnisaidie hapa

Ahsante. Na simu kwamba wananunua kwa jumla pia? Je, layman(mgeni) kwenye shughuli hizi unamshauri atafute kazi nyingine au ajikite kwenye u-winga?
Unaongea na wale wenye maduka wanakupa kitengo Cha kuzitangaza kwenye social media zote simu na Bei mpya, used na refurbished
 
Hongera , lakin haujasema je wewe ni mwenyeji wa hapo hapo Dar es salaam au unatokea mkoa na shule ndyo umekuleta jijini ??... Kwanini nimekuuliza

1)kama umetokea mkoa kaaa uelewe Dar es salaam hamna shule ya bweni ya serikali namaanisha shule zote maarufu Dar kama
  • Azania
  • Tambaza
  • kabasila
  • chang'ombe
  • jangwani
  • Benjamini na nyingine nyingine wadau watanisaidia

Siyo shule za bweni , hivyo basi kuna hostel za watu binafsi ambazo huwapangisha wanafunzi kwa gharama fulani , mfano zipo ambazo kwa mwezi ni tsh 20000 mbaka 45000
Hizi za 20000/= moja zina kunguni wengii sanaa hili lazima nisa lakini pia siyo nzuri sana kwa mwanafunzi kujisomea kumbuka kwenye hizi hostel uhuru ni wakutosha unaweza hata usikanyage darasani mwezi mzima na hamna atakae kuuliza hapo msala utakuwa kati ya wewe na walimu wa shuleni kwenu

- kwasababu Azania ni boys sina tatizo ila ingekuwa chang'ombe au kibasila kule hapa ningekushauri ukasome sanaa ufuate kilichokupeleka mimi nimeshuhudia wengi wakipoteza direction kutokana na maisha ya hostel maana huko ni kawaida kukuta jamaa na demu wake wote wanasoma darasa moja wanaishi kama mume na mke . Sasa kivumbi huja wakipigana chini hivyo mwenzangu na mimi kama na wewe ni wakuigaiga kufeli nje nje ..

Yapo mengi lakini machache ni hayo
Hizo shule zote kwa advance ni bweni.
 
Cha kwanza kabisa, hama PCM ambako unaenda kupata three ya 15, njoo HKL ili upate one yako safi, ndipo twende sambamba.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nimecheka mnooo
 
Anapewa miezi 2/3 ya kufikiria kuhamia HGL baada ya hapo mlango unafungwa asubiri F za kutosha akiwa PCM
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] aka komae, km ataenda kuweka usharobaro na kufata dents wa jangwani bas ataumaliza mwendo mapemaaa.

Tena phyz ndo kabisaa itamkataa mapemaaa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].
Cna hamu hata.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kuna mate nlisoma nae primary, o leevel alisoma kata akafanikiwa kupata 1 ya 15 akaenda Azaboy PCB 4m 6 kapiga 3 ya 14, analaumu had leo.

Khaaaah!! Lakini mbna ile ni shue kongwee??
Ogopa kusoma PCB azania Bora usome PCM Ila PCB pale shimo la kifo kwa msongo wa mawazo unaingia na 1 unatoka na 0 hio ndio azania walimu wa PCB vichomi,
 
Kwahiyo kombi ya PCM ukifanya mzaha unazungusha zero. Ukifika shule soma. Upuuzi mwingine wowote achana nao ikiwemo mitandao ya kijamii. Kuwa bize na Nelkon, Roger Muncaster, Shayo, na vitabu vingine vinavyohusika. Pia Tuition kwa wingi.
 
Ogopa kusoma PCB azania Bora usome PCM Ila PCB pale shimo la kifo kwa msongo wa mawazo unaingia na 1 unatoka na 0 hio ndio azania walimu wa PCB vichomi,
Ila kiukweli, Jangwani, azania, kisutu, zanaki, hizi shule ziko town kati mnoo, afu full vurugu na heka heka. Mwanafunzu usipokua makini unaanguka huku unajiona.

Kwanza mie ningesoma Dar kwa level yoyote, kati ya ordinary au advance, mmmh sijui km ningekua hapa.
[emoji119][emoji119][emoji119]
 
Huyu alishamiliki smatphone kabla ya kumaliza kidato cha nne,na kuingia JF?hakika kama ni wewe mwenyewe basi shule Kwako itakuwa ngumu sana
 
Combi za PCM, PCB ni mara chache sana kupata walimu wazuri kwa masomo yote matatu.
Achana na shule, ufaulu unategemea mambo mengi mfano.
1. Huko o level ulitafuniwa au una msuli wa kupiga topic bila mwalimu? A level utapiga msuli wa kutosha. Material ni mengi.
2. Ufaulu unategemea uwezo wenu ninyibwanafunzi na uwezo wa waalimu wenu kumaliza sylubus na ku solve sanaaa.
3. Watunga mitihani wanaweza pita mule mlikosoma. Wakipita pembeni ndo hivyo tena.
4. Wewe binafsi na maandalizi yako na uwezo wako binafsi kwenye kila somo...A level utatumia logic, utakremu, utasolve, speed, na uwezo wa kumeza volumes za materials. Ukipwaya mahali ndio udhaifu wako.
5. Afya na mazingira ya kusomea. Azania ni mujini na kila kishawishi. Una utulivu? Pana uhuru wa kutosha !! Wapenzi kama wote kuanzia vitoto vya magomeni na kariakoo, shule na vyuo vinavyowazunguka. Bila kusaha mama ntilie !!
6. Shule nyingi za mjini zinatumiwa sana na magenge ya madawa ya kulevya.. utaambiwa acha kuomba hela wazazi tengeneza hela yako kwa kuuza mizigo yao..ukiingiamo umeishaaa.

Karibu Azania shule yangu ya miaka ya 80
 
Hakikisha husomi...ni wewe na mbususu mbususu na wewe...Kuna vibinti pale jangwani girls ni vitamu hivyo...hiyo shule IPO kati kati ya mji Yani hapo ilipo ndio jicho la dar es salaam...Kuna zambi utazikuta ambazo hukuwahi kuzania kuwa ni zambi...aisee karibu darisalama ujifunze zambi mpya
 
Kama kichwa cha uzi kinavyosema, mimi nimemaliza form four mwaka jana hivyo form five selections zimetoka na nimechaguliwa kwenda Azania sec

Hivyo najua humu kuna watu wanaishi hapo karibu au wamesomea pale naomba mnipe hali ya maisha ya pale,ufaulu wake, n.k

Natokea mikoani na itakuwa mara yangu ya kwanza kuishi dar

Combination nimechaguliwa kusoma PCM

Natanguliza shukurani
Karibuni wajibu


Funny boe
UNA DIVISION NGAPI
 
Back
Top Bottom