Nimechoshwa na Huu umungu mtu unaooneshwa na serikali! Mpaka Sasa Mshahara haujatoka? Mnatuchukuliaje?

Kumbe uko hopeless kiasi hiki?
Kwanini usitumie busara Kama Mshana Jr ?
Hakika umeliangusha taifa la wapare kwa kauli careless Kama hii.
Kama mnaona mnachofanyiwa sio sawa, kwann msiache kazi?
Kila Meimosi kauli ni ile ile kuongezewa mishahara, kwann msiache kazi mana mnachofanyiwa sio haki yenu?
Hv unajua n watu wangapi nje wanatamani kuwa hapo ulipo kwa huo huo mshahara wako?
 
Tarehe 28 hadi tarehe 30
 
Ukiambiwa jiajiri achana na mambo ya ajira za kitumwa hutak,,,,,,,wenzako asubuh tar1 jioni tar30
 
Ukilipwa tarehe 5, mpaka tarehe 5 mwezi umeisha,
Kwahiyo tarehe 22 mpaka tarehe 22 mwezi umeisha.
Imeishia la ngapi?
Mwezi unaanza tarehe 01 na unamalizika tarehe 31 au 30 au 28 kwa mwezi wa february.
Utakuwa hujaenda shule wewe au embu angalia kalenda kama unayo inaonyesha mwezi unaanza lini na unaisha lini.
Kwa hiyo wewe kwa mfano wako huo kutoka tarehe 05 mwezi 05 hadi 05/06 unaweza kabisa kwa shule uliyosoma ukathibitisha kwamba huo ni mwezi wa 05 umekamilika?
Tatizo ni mazoea mabaya ya kutokulipwa mishahara tarehe stahili nakushauri jijengee mazoea kama unategemea huo mshahara panga bajeti vizuri ya mshahara ikitokea mshahara mmelipwa kabla ya mwisho wa mwezi wewe uache ikifika tarehe 01 mwezi unaofuata ndio uanze kutumia.
Kuna jamaa yangu nilimuona zuzu sana walilipwa mishahara sijui tarehe 22 kulikuwa na sikukuu gani sijui akatumia hela hovyo kwenye sikukuu kufika mwisho wa mwezi hana kitu
 
Sawa, unachosema ni sahihi ni lazima kusevu
 
Unastahili kulipwa mshahra baada ya siku ya 30 ya mwezi uliofanya kazi.

Tulia mwisho wa mwezi bado.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…