Nimechukia sana kukosekana kwenye ajira za jana. Nina jazba sana nimekata tamaa

Nimechukia sana kukosekana kwenye ajira za jana. Nina jazba sana nimekata tamaa

Mtu unatembeza CV mpaka kutembeza cv ndo inakuwa kazi yako.
Ila hy slogan ya kuwa disappointment inanifanya nicheke huku nalia mana hakuna namna tena.
Yah unatembeza CV we mie nilishajikatia tamaa! Mtu aniambie lete CV ntapeleka ila sio kupuyanga una apply ilimradi tu unajipotezea muda tu na kazi hupati ng’oo!

Kazi zipo mikononi kwa watu aisee!
 
Kuna makosa mengine yanahitaji mda mrf kuyarekebisha na sio kwa siku kadhaa, mfano suala la ajira kuna graduate zaid ya laki tatu waliolimbikizwa mtaani na mwendazake, kuwapunguza hawa mpk waishe is not overnight process.
Ukizingatia wengine wanaongezeka kama kikokotoo cha Heslb cha retention fees😂😂😂
 
Kuna mtoto wa rafiki yangu aliniambia kwa machozi jana, kuwa kuna rafiki yake amepata lakini ilibidi mumewe (wa huyo aliyepata) ilibidi atoe milioni moja ili kuhakikishiwa jina la mke wake kuwepo. Sasa nyie endeleeni kusikiliza kelele za Ummy na bosi wake. Tafuteni hela vijana. Nimeamua kujipanga wanangu wakimaliza elimu wasije wakaajiriwa wakasake noti
Kwani kuna ulazima wafike chuo kikuu! Wakimaliza form 4 tu waachane na habari za shule
 
Umeorodhesha kozi nyingi hapo juu....

Kwa hiyo hao wana ajira za kumwaga?!!!

Mathalani mainjinia ili wapate tenda ni rahisi?!!!
Wana uchumi wa kufungua vikampuni uchwara ?!!!

Hao wengine si ndio wanaopanga foleni interview ya watu 10 wenyewe wakiwa 2000?!!!!

Mkuu banaa 🤣🤣🤣🤣
Anaongea tu huyo hajui msoto wa mtaani! Hamna cha kozi yenye hela wala ambayo haina!😂😅😅 Injinia usipoajiriwa basi uwe na kampuni utafute tenders! Nje ya hapo unaumia
 
Kama Magufuli alikosea kwanini wengine wasirekebishe makosa yake? au aliondoka na akili zetu!.
Kama hakuondoka na akili zenu mbona bado kuna watu wanamlaumu kwa ajira za jana wakati yeye alijiendea zake zaidi ya miezi mitatu sasa?
 
Mtu unatembeza CV mpaka kutembeza cv ndo inakuwa kazi yako.
Ila hy slogan ya kuwa disappointment inanifanya nicheke huku nalia mana hakuna namna tena.
Mkuu binafsi nimefanya kazi ya ulinzi, imenipitisha kwenye ofisi nyingi sana. Nimegundua suala la recruitment lina mambo mengi na mara nyingi linategemea sana culture ya kampuni na kazi inayofanyika.

Usitegemee sana CV na ukubwa wa maslahi. Utakuwa very dissapointed.
 
Hio kazi ulio nayo ishikilie vizuri aisee! Hamna namna ingine utaishi ukitupwa mtaani[emoji23][emoji23][emoji23]!!! Mtaani kugumu sana kmmnnr
Daaah asee kweli mkuu....ila kazini nako unoko unoko tu yaan[emoji848][emoji848]
 
Sio wew tu, mimi hapa nna watu kama 7 hapo nyuma wananitegemea na mm nategemea nipate ajira ya serikali nikope bank nikasomeshe wadogo zangu.. hapa nilipo sina hamu natamani ningepata Namba ya Mheshimiwa Ummy nimlilie maana sina namna.. Kwa kweli next time waangalie Hata Mwaka mtu uliohitimu ili wote tupate kwa Uhakika.. inavunja moyo sana..
Wanasomaga sms wanazotumiwa, wewe mtafute kwenye mitandao ya kijamii, kweli inauma watu wanaumia huko mitaani hadi tunawaonea huruma.usimwambie akusaidie wewe kama wewe mwambie waajiri kufatana na mwaka.
 
Yah unatembeza CV we mie nilishajikatia tamaa! Mtu aniambie lete CV ntapeleka ila sio kupuyanga una apply ilimradi tu unajipotezea muda tu na kazi hupati ng’oo!

Kazi zipo mikononi kwa watu aisee!
Kwahiyo mkuu sasa hivi unajishighilisha na nini?
 
Boss usikate tamaa, amini ipo siku yako.

Mm hua najisemea 'disappointment ni kitu cha kawaida sana kwa mwanadamu' usijipe matarajio makubwa katika kutafuta kitu. Mimi kila siku nasambaza cv mpaka nalia mana hata kazi ya kujitolea pia hupati.
Pole mkuu

Hebu njoo PM
 
Nimejisikia kukata tamaa sana, haiwezekani mtu umehitimu 2016 unaachwa wanakuja kuajiliwa watu wa 2018 wakati hata vigezo hakuzidi nyote mna vyeti nyote mmefaulu,

uchambuzi gani huo uchaambuzi uchwara mlioutumia?

Magufuli ulaaniwe popote pale ulipo wewe ndiye chanzo, mbona Kikwete alikua anaajiri waalimu wote waliohitimu?

sikupendi magufuli na hata sitakupenda umetutia umaskini mtupu

kwanini kigezo kisiwe mwaka wa kuhitimu? wajjiri 2015 wakiisha wafate 2016 wakiisha wafate 2017

upuuzi mtupu endeleeni kuneemeka sisis tusote mtaani bhana
Badala ya elimu tunayoipata kumsadia mtu kupambana na maisha, inamlemaza , inamfanya aone maisha bila ajira ni mateso, inamletea sonoma, pressure na maradhi yatokanayo na mkazo.
 
Hii barua ni nzuri nahisi ni ngumu yeye kumfikia, kwa nini usingemwandikia moja kwa moja kwenye account yake huko insta au tweeter?
 
Mkuuu endelea kupambana but sisi wengne tupo humu kwenye ajira zaidi ya miaka 7 kama tusingekuwa tushalemewa na majukum tunatamani kutoka but hakuna ujanja.Huku kwenye ajira hasa za ualimu ni kuwatengeneza masikini walio na elimu zao.

Hebu fikiria mm binafsi nimekaa miaka nane bila kupandishwa daraja na nimekuja kupanda ongezeko sh 110,000/= hivi kweli miaka nane unasubiria tu uongezewe hiyo fedha ikusaidie katika maisha yako na majukum yanaongezeka kadiri umri unavyoongezeka.

Tatizo Tz mazingira ya kujiajiri ni magumu sana but right yangekuwa mepesi hakuna ambae angependa kuajiliwa hasa kada ya elimu.

Mm nashauri kama una uwezo wa kuanza na kidogo jiajiri miaka mitano ijayo utakuwa mbali lakiini ualimu ni kazi inayokatisha tamaaa

Sent from my TECNO KA7O using JamiiForums mobile app
 
Pole sana Mkuu!Nakuelewa sana unachosema!!JK Angekuwepo ange handle hiyo ishu ya Ajira vizuri!!Angekuja na suluhisho!!Hata hivyo Walimu hawatoshi nchini na sector nyingine pia hawatoshi kabisa!!!Huo ndio ukweli!!mama hadi mwakani atafanya kweli!!!
Tatizo ni hali ya uchumi. Serikali haina uwezo wa kuajiri wahitimu wote wa vyuo vya ualimu. Huo ndio ukweli mchungu.
 
Back
Top Bottom