Nimefanikisha kutimiza ndoto za binti wangu wa kazi

Nimefanikisha kutimiza ndoto za binti wangu wa kazi

Habari zenu nyote,

Ni takribani miaka 6 sasa tangu niwe na huyu msaidizi wa kazi za nyumbani, nilimchukua akiwa mdogo akiwa na umri wa miaka 15 baada ya kumaliza elimu yake ya msingi.

Maisha ya nyumbani kwao yalikuwa ni duni sana, na wazazi wake walionekana kushukuru sana binti yao kupata hii kazi ambayo mshahara kwa huo mwaka tulikubaliana elfu 30.

Baada ya kukaa nae kwangu, ndugu niliokuwa nakaa nao akiwemo mke niligundua hali ambayo sio nzuri ya kumtumikisha kazi nyingi zinazomzidi umri wake na zingine zingewezwa kufanywa na wao.

Nilizungumza nao na nashukuru walinielewa na wakawa wanamchukulia Kama mdogo wao na hata utambulisho wake kwa wageni haukuwa tena mfanyakazi wa ndani bali mdogo wetu.

Nilimshurikisha mke wangu juu ya kumuendeleza huyu binti na tulipomuuliza nini anapenda kujifunza, alitujibu anahitaji kuwa mshonaji wa nguo.

Tulimtafutia chuo akasoma mwaka mmoja hapo baadae tukamhamishia VETA kwa ajili ya ujuzi zaidi wa mafunzo hayo kwa mwaka mwongine, Alipomaliza aliomba kuendelea na fani nyingine ya urembo na upambaji hapohapo VETA tukamlipia na alimaliza vema.

Baada ya kumaliza tulimnunulia vyerehani viwili kwa kutumia pesa yake ya mshahara tuliyokuwa tunamtunzia na kuongezea ilipopungua na kumlipia frem kwa miezi 6 pamoja na kumuwekea vitenge na vitambaa kidogo kwenye frem akaanza kushona huku akiwa anakaa kwangu kwa miezi miwili.

Baada ya kumchunguza na kuona akili yake imekomaa, tukampangishia chumba cha 30k kwa miezi 4 akahamia na vyombo kidogo.

Nafurahi kuona hadi sasa anaendelea vizuri hakosi 40elfu kwa siku, sasa amepata mchumba anataka kuolewa.

Hili ni Jambo la kujivunia kwangu kuona maisha yake yamebadilika.
Hongera zenu kwa Utu mlionao!
 
Ok. Good. Mungu akubariki kwa msaada mzuri. Swali. Sasa unamwingine, naye utamfanyia naye hivyo hivyo au yule alikuwa special case?

Ulivyo wabana wife na ndugu wawe wanamsaidia kazi zake hawakuuliza basi walimhitaji wa kazi gani kama kazi watafanya wao au uliajiri mwingine wa kumsaidia kazi?

Na hao ndugu wengine uliowataja kwa nini hukuwasaidia ili wawahi kuondoka kwako ili ubaki na wife au umeridhika waendelee kubaki kwako?

Finally, usisahau na kutimiza ndoto za wife na the next beki tatu acha boss wake awe ni mkeo. Utamtatiza wife sana na competition ya ma bek 3.

Sio kwa ubaya ila ni vuzuri pia tuchunguze nyuma ya pazia kama mambo ni shwari.
Hivi anawezaje kumsomesha mdada wa kazi huku mdogo wake yupo nyumbani? Vitu vingine vinajijibu automatically
 
Hivi anawezaje kumsomesha mdada wa kazi huku mdogo wake yupo nyumbani? Vitu vingine vinajijibu automatically
Mzee unajua maisha ya familia yangu na huyo mdogo wangu unaemzungumzia?

Ndugu yaani kumtaja mdogo wangu kwenye uzi wewe ushaconclude kwamba hana mishe zozote, Aiseee
 
Huwenda mungu alikulipa sana kwa uliomtendea huyo bint lkn kuja kusimulia huku tayali mungu ameshafuta mema yooote aliokulipa ambayo ulimfanyia huyo binti,hakuna jambo jema kama kumafanyia mtu wema kisha ukakaa kimya unapata fadhila nyingi sana kwa mwenyezi mungu
Mkuu kwani huku kuna shida gani?
hahaha kwamba nimekosa baraka haha, wewe jamaa umenichekesha sana
 
Umeandika nilichotaka kuielezea...mie wangu alikua akiona ratiba unasoma maharage ananuna hatari....bas DStv ikate mnuno..unamkosesa matamthilia ! yake...khaa!
[emoji23][emoji23] kawa mama mwenye nyumba sasa, yaani haya maisha jamani unaweza kuta boss hana shida binti sasa [emoji24][emoji24][emoji24], unakuta binti safi boss sasa maisha hayako sawa kabisa!
 
Habari zenu nyote,

Ni takribani miaka 6 sasa tangu niwe na huyu msaidizi wa kazi za nyumbani, nilimchukua akiwa mdogo akiwa na umri wa miaka 15 baada ya kumaliza elimu yake ya msingi.

Maisha ya nyumbani kwao yalikuwa ni duni sana, na wazazi wake walionekana kushukuru sana binti yao kupata hii kazi ambayo mshahara kwa huo mwaka tulikubaliana elfu 30.

Baada ya kukaa nae kwangu, ndugu niliokuwa nakaa nao akiwemo mke niligundua hali ambayo sio nzuri ya kumtumikisha kazi nyingi zinazomzidi umri wake na zingine zingewezwa kufanywa na wao.

Nilizungumza nao na nashukuru walinielewa na wakawa wanamchukulia Kama mdogo wao na hata utambulisho wake kwa wageni haukuwa tena mfanyakazi wa ndani bali mdogo wetu.

Nilimshurikisha mke wangu juu ya kumuendeleza huyu binti na tulipomuuliza nini anapenda kujifunza, alitujibu anahitaji kuwa mshonaji wa nguo.

Tulimtafutia chuo akasoma mwaka mmoja hapo baadae tukamhamishia VETA kwa ajili ya ujuzi zaidi wa mafunzo hayo kwa mwaka mwongine, Alipomaliza aliomba kuendelea na fani nyingine ya urembo na upambaji hapohapo VETA tukamlipia na alimaliza vema.

Baada ya kumaliza tulimnunulia vyerehani viwili kwa kutumia pesa yake ya mshahara tuliyokuwa tunamtunzia na kuongezea ilipopungua na kumlipia frem kwa miezi 6 pamoja na kumuwekea vitenge na vitambaa kidogo kwenye frem akaanza kushona huku akiwa anakaa kwangu kwa miezi miwili.

Baada ya kumchunguza na kuona akili yake imekomaa, tukampangishia chumba cha 30k kwa miezi 4 akahamia na vyombo kidogo.

Nafurahi kuona hadi sasa anaendelea vizuri hakosi 40elfu kwa siku, sasa amepata mchumba anataka kuolewa.

Hili ni Jambo la kujivunia kwangu kuona maisha yake yamebadilika.
Hakika ni kitu cha kujivunia sana. Mungu atakurudishia!
 
[emoji23][emoji23] kawa mama mwenye nyumba sasa, yaani haya maisha jamani unaweza kuta boss hana shida binti sasa [emoji24][emoji24][emoji24], unakuta binti safi boss sasa maisha hayako sawa kabisa!

Hahaha bas akabebeshwa mimba...nikamwambia maisha sio unavyofikiri wewe. Bas alidhan akizaa mtoto atamspoil as I do!..hhah kachakaa balaa yuko huko Musoma. Namuona huruma kaolewa na wababe. Full vipigo. Akampa jina mwanaye jina langu. So nnatakiwa kumsaidia mtoto yule walau aende shule!
 
Hahaha bas akabebeshwa mimba...nikamwambia maisha sio unavyofikiri wewe. Bas alidhan akizaa mtoto atamspoil as I do!..hhah kachakaa balaa yuko huko Musoma. Namuona huruma kaolewa na wababe. Full vipigo. Akampa jina mwanaye jina langu. So nnatakiwa kumsaidia mtoto yule walau aende shule!
Duu pole yake, halafu mabinti wasiku hizi wameranduka kweli hata ukimshauri anaona unamzibia, kuna mmoja alikuwa kwa ndugu yangu nikamshauri vizuri sana, na walikuwa mjini kabisa boss anamwamini kwakila kitu, safari na katoto ka boss ni ndege tu, baadaye kaona ni upuuzi nakuja sikia kaolewa na mbabe kipondo kwa sana maisha duni mtoto kaumwa hata pesa ya hosp shida mpaka mtoto kafia mgogoni mme yupo kwa kahaba
 
Duu pole yake, halafu mabinti wasiku hizi wameranduka kweli hata ukimshauri anaona unamzibia, kuna mmoja alikuwa kwa ndugu yangu nikamshauri vizuri sana, na walikuwa mjini kabisa boss anamwamini kwakila kitu, safari na katoto ka boss ni ndege tu, baadaye kaona ni upuuzi nakuja sikia kaolewa na mbabe kipondo kwa sana maisha duni mtoto kaumwa hata pesa ya hosp shida mpaka mtoto kafia mgogoni mme yupo kwa kahaba
Yaani wanaharibu Sana maisha yao kwa tamaa za kijinga!
 
Yaani wanaharibu Sana maisha yao kwa tamaa za kijinga!
Sana nilimwambia kuna akili yakujiongeza kuna wengine Mungu aliwajalia akili ya kuzaliwa hakuna ushauri wa mtu unajiongeza mwenyewe na Mungu anakusaidia, sasa wewe unapata washauri wazuri watumie, lakini ndiyo hivyo
 
Na Mimi nashukuru Mungu msichana wangu wa kazi wa Kwanza nilihakikisha anatunza mshahara mpaka kununua cherehani yake halafu Mimi nikamlipia Ada ya mafunzo.....ingawa aliondoka Kwa jeuri lakini baadae alirudi kuomba msamaha. Sasa yupo kijijini amekuwa single mama na kazi ya ushonaji inamsaidia
Msichana wangu wa sasa naye ameshanunua cherehani yake na nimeshamtafutia shule ataanza next month.
Nashukuru Mungu
 
Hizi ndizo mada tunaziitaj humu..

Sio ujinga wa ngono kimasihara kla siku..

Mods hizi ndizo nyuzi za kuzipa kipaumbele..

Sio ujinga ujinga tu..
 
Ndugu umefanya jambo kubwa sana maishani mwako na huyo dada kadri atakavyowasaidia wengine basi ujue una fungu lako hapo lipo kwa Mungu...ulichokifanya hakina utofauti au naweza kusema ni zaka kwa upande wetu waislamu(wanoujua watanisahihisha).

M/Mungu akubariki wewe na familia yako na ukoo wenu
Habari zenu nyote,

Ni takribani miaka 6 sasa tangu niwe na huyu msaidizi wa kazi za nyumbani, nilimchukua akiwa mdogo akiwa na umri wa miaka 15 baada ya kumaliza elimu yake ya msingi.

Maisha ya nyumbani kwao yalikuwa ni duni sana, na wazazi wake walionekana kushukuru sana binti yao kupata hii kazi ambayo mshahara kwa huo mwaka tulikubaliana elfu 30.

Baada ya kukaa nae kwangu, ndugu niliokuwa nakaa nao akiwemo mke niligundua hali ambayo sio nzuri ya kumtumikisha kazi nyingi zinazomzidi umri wake na zingine zingewezwa kufanywa na wao.

Nilizungumza nao na nashukuru walinielewa na wakawa wanamchukulia Kama mdogo wao na hata utambulisho wake kwa wageni haukuwa tena mfanyakazi wa ndani bali mdogo wetu.

Nilimshurikisha mke wangu juu ya kumuendeleza huyu binti na tulipomuuliza nini anapenda kujifunza, alitujibu anahitaji kuwa mshonaji wa nguo.

Tulimtafutia chuo akasoma mwaka mmoja hapo baadae tukamhamishia VETA kwa ajili ya ujuzi zaidi wa mafunzo hayo kwa mwaka mwongine, Alipomaliza aliomba kuendelea na fani nyingine ya urembo na upambaji hapohapo VETA tukamlipia na alimaliza vema.

Baada ya kumaliza tulimnunulia vyerehani viwili kwa kutumia pesa yake ya mshahara tuliyokuwa tunamtunzia na kuongezea ilipopungua na kumlipia frem kwa miezi 6 pamoja na kumuwekea vitenge na vitambaa kidogo kwenye frem akaanza kushona huku akiwa anakaa kwangu kwa miezi miwili.

Baada ya kumchunguza na kuona akili yake imekomaa, tukampangishia chumba cha 30k kwa miezi 4 akahamia na vyombo kidogo.

Nafurahi kuona hadi sasa anaendelea vizuri hakosi 40elfu kwa siku, sasa amepata mchumba anataka kuolewa.

Hili ni Jambo la kujivunia kwangu kuona maisha yake yamebadilika.
 
Habari zenu nyote,

Ni takribani miaka 6 sasa tangu niwe na huyu msaidizi wa kazi za nyumbani, nilimchukua akiwa mdogo akiwa na umri wa miaka 15 baada ya kumaliza elimu yake ya msingi.

Maisha ya nyumbani kwao yalikuwa ni duni sana, na wazazi wake walionekana kushukuru sana binti yao kupata hii kazi ambayo mshahara kwa huo mwaka tulikubaliana elfu 30.

Baada ya kukaa nae kwangu, ndugu niliokuwa nakaa nao akiwemo mke niligundua hali ambayo sio nzuri ya kumtumikisha kazi nyingi zinazomzidi umri wake na zingine zingewezwa kufanywa na wao.

Nilizungumza nao na nashukuru walinielewa na wakawa wanamchukulia Kama mdogo wao na hata utambulisho wake kwa wageni haukuwa tena mfanyakazi wa ndani bali mdogo wetu.

Nilimshurikisha mke wangu juu ya kumuendeleza huyu binti na tulipomuuliza nini anapenda kujifunza, alitujibu anahitaji kuwa mshonaji wa nguo.

Tulimtafutia chuo akasoma mwaka mmoja hapo baadae tukamhamishia VETA kwa ajili ya ujuzi zaidi wa mafunzo hayo kwa mwaka mwongine, Alipomaliza aliomba kuendelea na fani nyingine ya urembo na upambaji hapohapo VETA tukamlipia na alimaliza vema.

Baada ya kumaliza tulimnunulia vyerehani viwili kwa kutumia pesa yake ya mshahara tuliyokuwa tunamtunzia na kuongezea ilipopungua na kumlipia frem kwa miezi 6 pamoja na kumuwekea vitenge na vitambaa kidogo kwenye frem akaanza kushona huku akiwa anakaa kwangu kwa miezi miwili.

Baada ya kumchunguza na kuona akili yake imekomaa, tukampangishia chumba cha 30k kwa miezi 4 akahamia na vyombo kidogo.

Nafurahi kuona hadi sasa anaendelea vizuri hakosi 40elfu kwa siku, sasa amepata mchumba anataka kuolewa.

Hili ni Jambo la kujivunia kwangu kuona maisha yake yamebadilika.
Hongera sana mkuu, huyo ndio uzalendo, na kuonyesha imani yako kwa Muumba wako. Tofauti na wale wapiga porojo wa mitume , wa kutoa sadaka, wa kuimba sabato,na ujinga mwingine wa kiitikadi za kidini ambazo haiongezi thamani kwa binadam mwenzake. Wale wenye itikadi Kali za dini na wao walete matendo yao anayozidi hili la kwako tuone. Mungu akubariki sana kiongozi
 
Na Mimi nashukuru Mungu msichana wangu wa kazi wa Kwanza nilihakikisha anatunza mshahara mpaka kununua cherehani yake halafu Mimi nikamlipia Ada ya mafunzo.....ingawa aliondoka Kwa jeuri lakini baadae alirudi kuomba msamaha. Sasa yupo kijijini amekuwa single mama na kazi ya ushonaji inamsaidia
Msichana wangu wa sasa naye ameshanunua cherehani yake na nimeshamtafutia shule ataanza next month.
Nashukuru Mungu

Wew ni #MshuaMaster

Hongera sana kwa Moyo huo..

Barikiwa sana
 
Habari zenu nyote,

Ni takribani miaka 6 sasa tangu niwe na huyu msaidizi wa kazi za nyumbani, nilimchukua akiwa mdogo akiwa na umri wa miaka 15 baada ya kumaliza elimu yake ya msingi.

Maisha ya nyumbani kwao yalikuwa ni duni sana, na wazazi wake walionekana kushukuru sana binti yao kupata hii kazi ambayo mshahara kwa huo mwaka tulikubaliana elfu 30.

Baada ya kukaa nae kwangu, ndugu niliokuwa nakaa nao akiwemo mke niligundua hali ambayo sio nzuri ya kumtumikisha kazi nyingi zinazomzidi umri wake na zingine zingewezwa kufanywa na wao.

Nilizungumza nao na nashukuru walinielewa na wakawa wanamchukulia Kama mdogo wao na hata utambulisho wake kwa wageni haukuwa tena mfanyakazi wa ndani bali mdogo wetu.

Nilimshurikisha mke wangu juu ya kumuendeleza huyu binti na tulipomuuliza nini anapenda kujifunza, alitujibu anahitaji kuwa mshonaji wa nguo.

Tulimtafutia chuo akasoma mwaka mmoja hapo baadae tukamhamishia VETA kwa ajili ya ujuzi zaidi wa mafunzo hayo kwa mwaka mwongine, Alipomaliza aliomba kuendelea na fani nyingine ya urembo na upambaji hapohapo VETA tukamlipia na alimaliza vema.

Baada ya kumaliza tulimnunulia vyerehani viwili kwa kutumia pesa yake ya mshahara tuliyokuwa tunamtunzia na kuongezea ilipopungua na kumlipia frem kwa miezi 6 pamoja na kumuwekea vitenge na vitambaa kidogo kwenye frem akaanza kushona huku akiwa anakaa kwangu kwa miezi miwili.

Baada ya kumchunguza na kuona akili yake imekomaa, tukampangishia chumba cha 30k kwa miezi 4 akahamia na vyombo kidogo.

Nafurahi kuona hadi sasa anaendelea vizuri hakosi 40elfu kwa siku, sasa amepata mchumba anataka kuolewa.

Hili ni Jambo la kujivunia kwangu kuona maisha yake yamebadilika.
Hongera sana Kiongozi
 
Back
Top Bottom