Nimefuatilia mtiririko wa visa, ni wazi kuwa Ndugai aliota mapembe na alikuwa akimdharau sana Rais Samia

Ndugai alimuattack mh. rais personally tena mbaya zaidi akampiga mkwara kuhusu 2025. Alipoharibu kabisa ni pale aliposema kuwa yale maneno yameditiwa na akaomba msamaha, what a fool!!
Magufuri alikopa sana bila kushirikisha bunge na kuwaaminisha wananchi kuwa nchi ni tajiri na miradi yote inasimamiwa kwa fedha za ndani na kipindi chote hiko hakuwahi kuhoji kuhusu mikopo zaidi za kujipendekeza kwa Magufuri. Hoja aliyoitoa haina mashiko, hakuna rais ambaye hajawahi kukopa so tumuache SSH ajenge nchi.
Ndugai ajiuzulu tu kwa mustakabari wake wa kisiasa
 
Wote ni wahuni wa CCM ile ile inayotusumbua kila kukicha watamalizana wenyewe huko huko wasituchoshe.
 
Hatumkubali spika kutokana na jinsi alivyoendesha bunge kibabe na kuendelea kuwalipa wabunge wasio na chama kodi zetu ila HojA yake ina mashiko lazima tuijadili na tupate majibu sahihi
 
Ndugai akikaidi kujiuzulu, atabaki kama mbwa asiye na meno, asiye weza kuona Wala kunusa. Itabidi asitoe maoni yoyote kinyume Cha serikali,wala kuchomekea vimaneno muda wa kuahirisha bunge. Labda awe anachomekea tu mambo ya Simba na yanga. Maneno ya Ndugai ni ya kumchonganisha Rais na wananchi.
 
Ndugai aondoke hatuna kiongozi pale ni mazoea tuu kodi zote hizi na sheria zao ndio wametunga wao ukimuuliza nae anashangaa hamna wachoishauri serikali zaidi ya kuongeza Tozo na kodi mpya kila kukicha..
 
Mama atakuwa amevumilia sana madhara ya mfumo dume kwa muda wote tangu kuapishwa kwake kuwa makamu wa rais. Atakuwa kavumilia dharau za kila aina kutoka kwa wasaidizi wake na wote wanaomzunguka.

Kaona sasa inatosha ngoja apambane na mtu ambaye anamdharau hadharani kwa kutumia kofia yake ya urais.
 
JPM kwa miaka mitano na miezi mitatu alikopa trilioni 29.3 Ndugai akawa kimya kabisa kama haoni kinachoendelea.

SSH amekopa trilioni 1.3 Ndugai anaanza masimango kama vile hakuona kilichofanyika kuanzia 2015-2021 February. Huo ndio unafiki wenyewe.
 
pengine kuna kalaana sehemu pia.
 
Tena vyomba vya dola inatakiwa vimtie nguvuni ataje kikundi Cha wahaini wenzie, wasitake kutuharibia Tanzania yetu wapuuzi hawa
 
Pambanisha Ndugai na Samia tu.

Ukimtaja hayati JPM hautafanikiwa. JPM ni chuma kingine.
 
JPM kwa miaka mitano na miezi mitatu alikopa trilioni 29.3 Ndugai akawa kimya kabisa kama haoni kinachoendelea.

SSH amekopa trilioni 1.3 Ndugai anaanza masimango kama vile hakuona kilichofanyika kuanzia 2015-2021 February. Huo ndio unafiki wenyewe.
Sio tu mnafiki,huyo ni muhaini kabisa
 
Hauhitaji Phd kutambua kwamba Ndugai hampendi mama. Anamchukia kisa tu ni Mwanamke. Huyu si wa kucheka nae huyu.Ajiuzulu tu
Anamdharau Sana Rais, kujiuzulu pekee hakutoshi, Kuna jinai pia inamuhusu,alichofanya kwasisi wakongwe Kuna kila dalili za uhaini
 
Nyie ndio mnapaka mafuta samia kwa mgongo wa chupa huku mkimng'ong'a kwa dharau. Kinachowafanya msiropoke ni kutanguliza tumbo tu. Si ndio nyie mnasema hamumtaki mzanzibari atawale bara? Si ndio nyie mlioanza kutengeneza timu za 2025 mkiongozwa na yule mkuu wenu wa kusini? Tena kuna yule kiherehere alivyosikia jobu anajiuzuru akajifanya anamuwahi kumwambia. Tunawajua nyie wachumia tumbo vizuri kuliko mnavyojijua😂😂😂
 
Mkuu achana hao sukuma gang washenzi,unapoteza nguvu bure hata shetani hakosi watetezi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…