Nimegundua mpenzi wangu akiwa na marafiki zake, huwa ananiita mimi kimburu

Nimegundua mpenzi wangu akiwa na marafiki zake, huwa ananiita mimi kimburu

Attachments

  • 17216721761750.8368765232159374.jpg
    17216721761750.8368765232159374.jpg
    2.3 MB · Views: 3
Kimburu ni aina ya paka wa porini, paka aliyeasi na kuamua kuishi porini huitwa kimburu. Kimburu ni maarufu sana kwa kukamata kuku wa kienyeji.
 
Katika pitapita kwenye maeneo ya ofisi ya mpenzi wangu, nikasikia wananiteta, ''kimburu wangu ananivuruga kweli, hataki kutulia na mimi, kila wakati ni migogoro tu''

Wenzie wakamuuliza, kimburu ndio nani; ndipo aliponitaja equation x.

Baada ya kusikia hayo maneno, hata sikuingia ofisini kwake, ikabidi niendelee na mihangaiko yangu.

Hapa bado natafakari, kwa nini ananiita mimi kimburu?

Nipeni ushauri wakuu, au na nyie wapenzi wenu wanawaita majina ya ajabu ajabu wakiwa na marafiki zao?​
Mburu kwa kichaga cha Vunjo ni mbuzi sasa kimburu ni "Kambuzi 😁😁
 
Mtoto akitoka kucheza na wenzie,akirudi home kachafuka vumbi mwili mzima...huwa tunasema unaonekana Kama kimburu...
 
Huku uzaramuni ni Ile mt mbadi inayopasulia mayai kwenye koo inatema maganda wakati imeshakula mtaga mayai kiatambo!
 
Kimburu ni mvizia kuku mnyama anaiba kuku na kuwatafuna inaonekana na wewe ni kicheche . Kisukuma kimburu ni kicheche
 
Kimburu ni paka aliyeasi yaani yule paka aliyetoka kwa bwana wake kulingana na tabia zake chafu may be kuiba mboga au hata kula vifaranga vya kuku na baadaye akafukuzwa na bwana ake kwenda kuishi porini,,, kwahyo maisha yake ni kujitafutia chakula na kula vifaranga vya kuku huyo ndiye KIMBURU
 
Back
Top Bottom