Nimegundua ndugu yangu wa damu ni mshirikina

Kuna njia mbili za wew kupata msaada wewe utachagua moja ... jitafakari rudi kafanye ibada mwombe MUNGU tafta sadaka maalum ya kujitakasa hakika MUNGU ni mwenye rehearsal nyingi atakufunika dhidi ya watu wabaya ...adui zako watakuwa adui wa MUNGU.... njia ya pili ni wew kwenda kwa mganga konki MshanaJR atakupa mwongozo ..... ila na sisitiza njia ya kwanza ndo best
 
Nakusomaa vizuri sana
 
Hapo kwenye kuharibuana KAZI, limeniguaa sana. Mimi ni mhanga wa hayo. Naandaa kombora zito sana sijakubali kabisa. Siku nitakayofyatua, hata Inzi hawakula mzoga huo.
 
Muumba wangu mimi haitwi Allah sawa huyo ni wako

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
 
Kuna mmoja kasema eti mama yako atakuroga vipi wakati kakuzaa, kakutunza na kukusomesha juu, si angekuroga ukiwa mtoto au tumboni!

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
 
Duu!

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
 
Komenti bora ya mwaka 2023. Pamoja sana mkuu.

Kwa mtoa mada: wagenga walisema meli huzamishwa na maji ya ndani na sio ya nje so nakielewa vizuri sana unacho kisema
 
Kuna mmoja kasema eti mama yako atakuroga vipi wakati kakuzaa, kakutunza na kukusomesha juu, si angekuroga ukiwa mtoto au tumboni!

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
Hata wachawi wanazaa na wana watoto.

Kuna KANUNI ZA UCHAWI, hawaui hovyo hovyo.

Anakuzaa vizuri na anakulea ila ikifika WAKATI MUAFAKA utaita maji MMA.
 
Na Ndivyo wanavyo fanya, halafu anachukuliwa mwenye akili zaidi

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
Sahihi kabisa.

Wana-target mtoto mwenye akili zaidi katika familia, yule shujaa, the LIGHT BEARER, huyo ndio wanampiga mavitu mazito ya KICHAWI.

Ni vita kali na ya ajabu, lakini UKIWAHI KUAMKA hawatakuweza MILELE.

Mama mchawiii ni balaaa. UTASHANGAZWA.
 
Sasa kama wazazi wako au mzazi utajinasua vipi! Sababu anakujua tangu tumboni, mtihani huo!

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
 
Tafuta kikosi kazi mkatie mirija! Bila ya hivo ndugu maana bila ya hivo utachezewa sana
 
bro unataka kusema kwamba ndugu yako na wewe pia mlikua mnaenda kwa wataalamu wanawaambia ndugu yako ni mwanga??una uhakika upi????kama unahitaji msaada nicheki tushauriane maana niliwahi kukumbwa na ishu kama hii usije kuwanyooeshea watu vidole..
 
Hebu weka ushahidi usiotia shaka kama nduguyo anakuroga,usije ukawa unamhisi vibaya tu
 
Wewe mchane ukweli tuu,,"Mwambie nduguu!!kuliko haya mateso unayonipa kwa mauchawi yako ya kinyoko mbili si bora uniue tuu Mamameeehh"huku macho makavuuu!!!
Usikute anamhisi vibaya tu, inawezekana Wala sio huyo nduguye
 
Sasa kama wazazi wako au mzazi utajinasua vipi! Sababu anakujua tangu tumboni, mtihani huo!

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
Hii inahitaji ufundi wa kiroho na utulivu sana.

Yaani utulie kweli kweli na uwe mvumilivu ili upate ujuzi wa kujinasua, haitaki papara. Ukiwa mtulivu, msaada utakuja kimaajabu au kimaono. Something of DIVINE NATURE will come in between to intervene or infuse knowledge unto your spirit [FOR YOU TO TAKE APPROPRIATE ACTION] (A GUIDANCE).

Hapa unaweza kukuta kuna MAMIKATABA ya ajabu ya kiroho baina yako na mama yako bila wewe kujua, au mambo mengine ambayo ni MAPANA ZAIDI kiroho.

JAMBO ZURI NI KWAMBA, kila kitu kilishapimwa katika UZANI WA KIROHO kabla haujazaliwa. Kila kitu kiko katika UDHIBITI.

Kama ni JARIBU lililopangwa kimkakati, basi lina lengo la kukufunza kitu kikubwa zaidi. Lazima uwe mtulivu sana na ujifunze KUJITAMBUA.

TIBA PEKEE ni kuingia katika ufahamu wa ndani sana, ndani ya roho yako, na utulie sana.

HUDUMA YA KWANZA ni kukata MASHINA yote ya kichawi ambayo unahisi ni SPIRITUALLY UNPLANNED / AJALI YA KIROHO / UNWORTHY / MALEVOLENT. NA PIA KUKATA KILA SPIRITUAL CORD / KAMBA inayoleta MAWIMBI HASI YA UMEME kwenye mwili wako, regardless yanatoka wapi.

Utakuwa na kazi nzito kidogo lakini UTAWEZA. Maana hapa utakuwa unapambana na JESHI KUBWA SANA LA AJABU NA BAYA, lakini UZURI NI KWAMBA HILI JESHII NI DHAIFU SANA KWAKO KIMIZANIA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…