Nimeguswa na wale wananchi waliookoa watu ajali ya ndege

Ulikuwepo ukaona ndege ilijipigiza mbele? Ilijipigiza wapi kiasi cha kufanya hewa iingie ndani..
 
Mavi matupu
 
Umeongea point, lkn kama kungekuwa na quickly response ya hawo experts bas hao local people wangezuiwa au wangeelekezwa na hao experts lkn hawakifika ontime ndio maana wavuvi wamewai, na taarifa ilitolewa mapema kabla ya kuzam meli hiyo
 
Wenye ujuzi ndio hao wanafika muda watakao.
Ajali zinapotokea zinataka utulivu na subra kidogo ili uokozi ufanyike pasi na kuleta madhara zaidi..papara na haraka haraka mara nyingi zinaongeza madhara.
 
Mkuu ulivyokomaa na ajali ya kagera kana kwamba hiyo ndio ajali pekee ambayo imewahi kutokea tz...

Matukio mengi ya ajali wanaowahi na kutoa msaada wa kwanza kwa majeruhi huwaga ni jamii ya watu wa eneo husika...

Zipo mistake ndogondogo za kitaalamu lakini matokeo ya uokozi huwaga ni positive zaidi kuliko hizi negativity za sijui usiokoe kwakuwa tu huna elimu ya kitaalamu juu ya mazingira ya ajali husika.

Yale ma ajali ya meli huko Zanzibar tuliona msaada wa wavuvi ambao hata vyombo vya uokozi vilikuwa vikiwategemea zaidi kwa uzoefu wao, ajali kibao zinatokea ukisikia Kuna majeruhi wameokolewa Basi ujue kwa 95% watu wa kwanza kufika na kuokoa walikuwa ni jamii ya watu wa eneo husika kabla ya ujio wa wataalamu
 
Wataalam watasema kama wavuvi ndio waliofungua milango, mimi sijui aliyefungua milango, abiria au wavuvi..
Kwa mijibu wa taarifa aliyefungua mlango ni muhudumu wa ndege aliyekuwa upande wa nyuma....
 
Mkuu, Una hoja nzuri Ila Acha kuhisi kihisia wazima uhalisia.
Kibongobongo Bado hatujafikia level hiyo ya kusubiria wataalam ili uokolewe unapopata ajali.

Una mawazo chanya Ila kimsingi hayana maana Kwa Aina ya maisha yetu watanzania.
 
Umeongea point, lkn kama kungekuwa na quickly response ya hawo experts bas hao local people wangezuiwa au wangeelekezwa na hao experts lkn hawakifika ontime ndio maana wavuvi wamewai, na taarifa ilitolewa mapema kabla ya kuzam meli hiyo
Tuelimishane kuwa ni vizuri kutoa muda hata wa dk 15 hadi 20 kusubiri rescue team au wenye dhaman ya kuelekeza wafike kwenye tukio km polisi, viongozi nk ili uokozi ufanyike wakati wao wakiwasiliana na wengine kwa msaada zaidi kuliko kufanya haraka inayoweza kutoa matokeo mazuri sawa lakini pengine ikaleta madhara pia..mfano wavuvi sidhani hata wanafaham ndege ilikuwa na abiria wangapi, unaweza kuokoa 5 halafu 10 wakapoteza maisha sababu ya kufanya haraka pasina na ufaham na ujuzi wa kufanya uokozi.
 

Ni kweli
Ila hiyo rescue team yetu sasa! Baadhi ya viongozi hufika na kugeuka wanasiasa kuificha ukweli badala ya ku mobilize resources zije kwa kuokoa, kwa hali hiyo hawa wananchi wa kawaida wanajikuta frontline always!
 
Mkuu, Una hoja nzuri Ila Acha kuhisi kihisia wazima uhalisia.
Kibongobongo Bado hatujafikia level hiyo ya kusubiria wataalam ili uokolewe unapopata ajali.

Una mawazo chanya Ila kimsingi hayana maana Kwa Aina ya maisha yetu watanzania.
Utakuwa ujinga wa kiwango cha juu kutetea experience mbovu..kila mahali polisi wapo, tena siku wengi tuna namba zao, viongozi wapo nk..watu wasubiri hata dk 20 ili wenye dhamana za kushughulika na usalama wa watu na mali zao wafike ili chochote kinachofanyika kifanyike kwa maelekezo..ajali ya morogoro kwa mfano ya ile Lori ya mafuta wewe unaona ni sawa ilivyofanyika watu kuvamia pasina na tahadhari hata ya usalama wao wenyewe..walipona sasa, na ubongo bongo wako..
 
Futa huu upuuzi uliouandika.
 
Huu nao ni Upumbavu. Kwa hiyo ukipata ajali Barabarani karibu na waendesha Bodaboba wasikusaidie mpaka kikosi cha uokoji cha Serikali kije??
 
Aisee!!, Point yako inaweza kuwa na maana kwa baadhi ya scenerio , hao wataalamu unaowazungumzia wamemuokoa nani pale?, all 26 alive's victim wameokolewa na wavuvi.In desperate times hususani accident human intuition inaanza then inafautia logic katika uokozi ,Mungu awape nguvu waliopoteza wapendwa wao , Mungu wabariki waliorisk maisha yao kuwaokoa wengine
 
Wataalam wenyewe si ndio tumewaona wako ufukweni huku wameshikiwa miamvuli? Ndio hao ulitaka wasubiriwe wakati abiria wako chini ya maji?

Kwenye uokozi, speed comes first. Expertise is overrated!

Hebu tuambie, bila hao wavuvi na mitumbwi yao kuna abiria angetoka humo akiwa hai?
 
Ajali zinapotokea zinataka utulivu na subra kidogo ili uokozi ufanyike pasi na kuleta madhara zaidi..papara na haraka haraka mara nyingi zinaongeza madhara.
Ni kweli kwamba kunahitajika utulivu na maarifa wakati wa dharura, lakini jiulize hao wataalam unaosema walikuwa wapi! hadi wavuvi na wananchi wa kawaida wakafika kwanza?

Tunahitaji kuwapongeza wananchi kwa jitihada zao.
Kilichotakiwa ni Wataalam kufika kwanza ili kuwaongoza wananchi, kwa bahati mbaya hawakuwepo.

Ingalikuwa ni ujinga kuwatazama watu wanatapa tapa eti wakisubiriwa wataalam ambao hatujui kama wapo.

Tatizo ni kutokuwa na maandalizi ya dharura na akili zetu Waafrika na sisi Watanzania ni kutojifunza.

Meli ya MV Bukoba ilitosha kutufunza kwamba lazima tuwe na kikosi cha uokoaji 24/7 katika ziwa Victoria.

Bukoba kuna Bandari na kiwanja cha ndege kama ilivyo Mwanza.

Kulitakiwa kuwe na kikosi cha uokozi kikiwa tayari saa 24 kwa wito wa dharura.
Sijui kama kipo na kama kilikuwepo kikowapi hadi wavuvi watangulie!

Gharama za kikosi cha uokoaji ni ndogo sana ukilinganisha na idadi ya V8 zinazozunguka nchini.
Tunawezaje kuwa na Helicopter ya kutangaza sensa lakini hatuna boti ya uokozi wakati wa dharura

Dodoma kila anayesimama anapongeza huduma nzuri za jamii !!
Ni mwendo wa mapambio na kujikomba tu, eti leo tuwalaumu wavuvi kwa kujitoa!

Dodoma hakuna anayefikiri dharura hata siku moja, kila mmoja akikamata kipaza sauti ni kusifia tu.

Kesho utasikia wanatoa rambi rambi, hawa ndio wakuwaambia wakae kimya siyo wavuvi waliojitolea

Ninyi wa Dodoma msitutie kichefu chefu wakati huu wa msiba , msitoe rambi rambi wala msiongelee ajali ya ndege, endeleeni na mapambio na kusifia, mafao yenu yapo salama, tuacheni tuomboleze ndugu zetu!

Haya hayapaswi kutokea miaka 60! Ni aibu sana.

JokaKuu Pascal Mayalla Mag3
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…