Nimeibiwa simu na mwizi ametoa pesa tiGO Pesa!

Nimeibiwa simu na mwizi ametoa pesa tiGO Pesa!

Ukiwa na namba ya simu wale mawakala wa kusajili laini wanaweza kukutajia namba ya nida. Yani kimantiki wewe ulichelewa kuchukua maamuzi ya kulinda laini baada ya kuibiwa. Bila shaka hapo baada ya kuiba mwizi alitaguta wakala akapata namba ya nida na detail zako kisha akafanya process ya kutengeneza password mpya na kutoa hela baadae. Scenario kama hii ni rahisi kufanikiwa
Majibu sahihi 100% anzia hapa
 
  • Thanks
Reactions: Lax
Kosa lipo kwa mamlaka ya serikali kama TCRA , kuruhusu mtu kupata taarifa za mtu hasa majina kamili kwa kutumia SIM card.
Issue siyo tigo, issue nikuwa na uhakika wa majina kamili ya mtu uliomuibia,
 
Kuna jamaa alikuja south kwa kukimbia kesi ya wizi wa mitandao anasema Magomeni yeye alikuwa ananunua line baada ya vibaka kuiba simu line wanamuuzia yeye anatoa pesa au kama haina pesa anaomba kutumiwa pesa na ndugu sometimes no sometimes yes
Yes..ukiona umepoteza line..kama hukuweka pin,,,ifutie usajili..au renew fasta...maana wanapelekewa wahuni Tena kwa kuuziwa Ili wapige Hela kwa kuwapigia ndugu zako,,,,ila watu wa aina hii wakishikwa hutasikia habari zao tena
 
Mzembe mkubwa ni wewe.

Kwa nini hukuchukua hatua za haraka za kufunga hiyo line? Wewe ulimpa mwizi muda wa kutosha kukuibia.

Ukipoteza line ama kadi ya benki piga simu kwenye benki ama mtandao wako haraka wafunge hiyo line ama kadi uwe salama.

Hapa sio mwizi wala tigo wenye makosa
Hivi hujui dk5 Kwa mwizi mzoefu ni nyingi sana ni sawa na mwaka mzima kwako?

Ule muda Bado huamini kama umeidondosha ama umesahau sehemu yeye tiyri kashamalizana nawewe.

Huko bank unaweza piga simu ikaita dk15 na hujapokelewa ovyo kabisa
Tena kama Hawa NMB ndo basi kabisaa utaimbiwa mapambaio Hadi sikio lichoke na akipokea anakwambia nenda TAWI lililo karibu Yako
 
Tigo at it again.

Kampuni ina kashfa za udukuzi bado unang’ang’ana tu.

Kule hata wafanyakazi wake wa IT lazima wanatoa hizo taarifa.

Kampuni ya hovyo sana. Wengi humo wanajikuta ni wana usalama.
Tigo ina wadukuzi ni balaa. Line naitumia kwa mawenge mno
 
Kutoka wapi?
Kupata nida ya mtu ni rahisi sana has ukiwa na namba ya airtel au tigo, kwahyo huyo alienda kwa wale mawakala wanaosajili laini wakamsaidia kuipata nida yako alafu akapga cm tigo kuwaambia amesahau namba ya siri hivyo abadilishiwe ,,,akishawwambia hivyo ataambiwa ataje namba zake za nida na tarehe na mwaka wa kuzaliwa ndivyo alivyofanya
 
Hata nchi yetu hiyo sheria wameweka. Mitandao kama TTCL na Voda wanajitahidi kuifuata lakini Tigo wao ndo ma-nunda.

Nilipotezaga ki simu na laini zote tatu. Kilichotokea nilirenew laini ya TigO bila shida yoyote kwa wakala tu. Laini ya voDa na TTcl ilinibidi kwenda kwenye 'shop' zao. Ya voda nikafanikiwa hapo lakini ya ttcl ikaongezeka kipengele cha kuwa hadi na loss report.

Wakati ule niliwamaindi kwa mtiririko wa ttcl then voda then wa mwisho hao tigo...... lakini kumbe kiusalama linaanza baba lao ttcl halafu voda then wa mwisho ndio hao tigo😅.
Huu ni ushuhuda binafsi.
Last year nilipotez lain ya voda, nilipata taabu ku renew mpaka loss report wako makin sana
 
Nimeibiwa simu yenye line ya Tigo na nilipoenda kuchukua line mpya naangia salio la pesa nakuta hakuna kitu! Kwenye statement inaonekana mwizi ametoa pesa mara tatu. Hii inawezekana vipi mtu hajui password yangu atoe pesa??
Pole sana kam umeibiwa simu ina thamani kubwa na pesa zako ni nyingi nitafute ili nipate kumrudisha mwizi wako atakutafuta yeye mwenyewe kabla ya siku 7 utakuwa umepata simu yako na pesa zako ulizoibiwa ikipita siku saba hujanitafuta tukafaya dawa sitoweza tena kumrudisha mwizi wako. Kazi kwako Mkuu.
 
Kweli kabisaa na makosa makubwa tunayoyafanya ni kusevu nida zetu kwenye contacts, kwaiyo ni rahisi kabisaaa mtu anapita na pesa kama yake
Mfano nimeibiwa simu, namba ya NIDA kweli nimeisevu kwenye contacts zangu. Jee alieiba simu vp ataingia kwenye contacts zangu na simu ina password? Ili aweze kutumia si mpaka aflash simu na akiflash simu si hamna kitu kinabaki?
 
Hata mm hiyo imenitokea niliibiwa simu kwenda kurudisha line nakuta pesa hakuna hata Mia kwenda tigo naambiwa mwizi aliomba PIN reset wakampa 0000 akabadili number akatoa pesa sina hamu na tigo
Yaani kirahisi hivyo? Wana maskhara na maisha ya watu hawa TIGO, ina maana security hamna, hata ID&V haiapply kwao?
 
Back
Top Bottom