Nimejisikia uchungu sana nyimbo za taifa zilipopigwa wakati mechi kati Kili Stars vs Zanz Heroes inaanza

Nimejisikia uchungu sana nyimbo za taifa zilipopigwa wakati mechi kati Kili Stars vs Zanz Heroes inaanza

Nimesoma maoni ya wadau humu, nimegundua kwamba kitendo cha Tanzania kurudi kwenye mfumo wa vyama vingi vya siasa 1992 na kupelekea kuondoka Somo la Siasa mashuleni, elimu ya uraia kwa vijana wetu imekua ndogo sana
 
Rais Mwinyi alipongeza ZRA kwa kukusanya Takribani Bilioni 288 kwa miezi 5. (55.4 Bilioni) kwa mwezi
Ni kwa mujibu wa Gazeti la 'The Citizen'. Akitoa pongezi hizo Rais anasema mafanikio mengi katika ujenzi wa Barabara, maji, afya na elimu ni matokeo ya ukusanyaji mzuri wa kodi wa 'SMZ'

Jana Naibu Waziri mkuu Biteko amezindua Jengo la Uhamiaji Pemba lililogharimu Takribani Bilioni moja.
Katika uzinduzi huo alikuwa na kamishna wa Uhamiaji wa Tanzania na Naibu Waziri wa Mambo ya ndani
Jengo limejengwa kwa gharama za Uhamiaji JMT, yaani kutoka Bajeti ya Wizara ya mambo ya ndani

Kama tulivyowahi kujadili, fedha za huduma za Uhamiaji Zanzibar zinabaki SMZ, lakini gharama za Uhamiaji zinabebwa na JMT ambayo ni kodi za Tanganyika. Kwanini SMZ isijenge jengo hilo kwavile wanakusanya fedha za Uhamiaji ?

Zanzibar inapata 10% ya Bajeti ya JMT, ina mgao wa fedha ziwe ni Mikopo au misaada na makusanyo ya kodi hayavuki bahari. Zanzibar haina mchango katika Muungano.

Gazeti la Mwananchi limetoa kanda na michango yake ya kodi kwa Taifa, Dar es Salaam ikibeba 84% , ikifuatiwa na Kanda ya Kaskazini, Ziwa, Kati , kusini na Nyanda za Juu. Zanzibar haikuonekana.

Pamoja na hayo fedha zinazokwenda Zanzibar kutoka Tanganyika a.k.a Tanzania ni nyingi kuliko kanda yoyote iliyotajwa hapo juu licha ya ukweli kwamba Zanzibar haina Bajeti za Wizara nyeti na zenye gharama

Hoja inabaki pale pale kwamba rasilimali za Tanganyika zimegeuzwa za Tanzania na hapo zinakuwa 'abuse'.
Hakuna msimamizo wa rasilimali za Tanganyika! Na abuse imekuwa kubwa sana awamu hii.

Tunahitaji Tanganyika isimamie rasilimali zake, kama Muungano unahitaji waulizwe Wazanzibar!
Inasikitisha kwa kweli.
 
Back
Top Bottom