Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nimetenda wajibu wangu. Nimetimiza ndoto zangu za kuwasomesha wadogo zangu nao wapenda sana.
Ni muda sasa nitafuta furaha. Waliosema raha jipe mwenyewe hawakukosea.
Asante kwa ushuhuda wako unaponyaDah tupo wengi mkuu, personally nimepambana sana kuisaidia familia na ndugu yyte mwenye ttzo, hali iliyopelekea kutoinvest sana katika maisha yangu binafsi zaid ya kujiendeleza na shule. Above all, sijawahi kuwa appreciated na wazaz wala ndugu, na ikitokea kuna jambo sijatatua, nakua miongoni mwa watu wa hovyo sana machoni mwao! Nlichoamua kwa sasa, moja, kutulia na wife na kufanya ishu zetu nje ya mkoa wa home, mbili nafanya lile ambalo tu haliathiri mipango yangu! Hata ufanye nn, furaha haitoki kwa ndugu mkuu.....karibu makao makuu ya nchi tulime alizeti (joking)
Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna Uzi niliandika humu kwa nini watu wenye roho nzuri na kujitolea kwa wenzao huishi maisha magumu au kawaida sana kuliko wale waliowasaidia?Tafuta huo Uzi unakuhusu mkuu.Katika dunia ya sasa jaribu kutafuta furaha yako kabla ya furaha ya wengine tunapata maisha magumu kwa kutaka kuwafurahisha au kuwahurumia wengine na kujiumiza wenyewe.Nimekata tamaa; Nimepigika, nimeteswa, nimedharauriwa, nimeumizwa , sasa Basi !
Ndugu zangu wana MMU kama ambavyo nimetanguliza hapo awali sina namna tena.
Dunia kwangu imekuwa chungu mno. Sioni jema wala.zuri katika dunia hii ya wanadamu. Pengine huko mbinguni aliko Mungu. Ili angalau nipate nafuu ya maumivu moyoni nawiwa kushare hapa.
Nimeumizwa sana na jamii. Kwenye siasa nimeumia sana. Kwenye jamii hivyo hivyo. Kwenye familia nina machungu makali mno. Kazini kwa moto kama kaa la mkaa wa mawe. Ndugu zangu mimi si lolote wala chochote kwao. Kifupi najiona thamani ya kuishi duniani haipo. Mwandishi wa Biblia kitabu cha Mhubiri alisema Duniani kila kitu ni upuuzi mtupu. Naungana naye kwa leo.
Ni hivi; katika makuzi yangu nilikulia mikononi mwa Mama yangu: alinilea kwa shida sana mimi na wadogo zangu. Nikiwa na miaka 9 nilianza kushirikiana na mama kutafuta kipato ili tupate japo mkate wa kila siku. Nilijishughulisha na kazi mbali mbali ikiwemo kilimo, biashara ya kuuza miwa, kuokota mavi ya ngombe na kuuza kama chanzo cha samadi, nimekata nyasi kwa ajili ya kuuzia watu wenye mifugo.
Wakati wote huo pamoja na maisha hayo nilikuwa na faraja maana siku zote mama yangu alitupa moyo mimi na wadogo zangu. Alipambana kila wakati na alidanganya hapa na pale ili tupate kuishi. Nakiri kabisa mama yangu hakuwahi kuwa mwizi wala kumuona akiwa na wanaume wengine kwa ajili ya kutafuta unafuu wa maisha. Baba yangu aliishi mjini na huko alifanya kazi ya kujiajiri na kuoa wake wengine na kutapanya mali.
Nikiwa na miaka 10 nilianza darasa la kwanza hadi nikamaliza form 4. Na nikajiunga na kidato cha kwanza hadi Elimu ya juu.
Wakati wote huo mimi nilikuwa mlezi kwa wadogo zangu na familia yangu kwa ujumla. Niliamini nitapambana hadi tufike mahali maisha yawe bora au atleast nafuu.
Sasa kazi ikaanza. Nikapata job nzuri ambayo inanilipa mshahara mzuri wa kuridhisha. Nikasema asante Mungu. Nitahakikisha wadogo zangu wote wanasoma na kufika pazuiri waliofeli nikawarudisha shuleni na wengine ku-resit mitihani yao. Alhamdulillah hawakuaniangusha wakafaulu nikawaendeleza vyuoni na sasa wengine wameahamaliza wana maisha yao.
Wengine wakawa wananidhihaki eti toka umefanya kazi una nini mpaka leo. Mbona hakuna ulichofanya cha kuendeleza maisha?? Nafsi yangu ikawa inaumia sana nikiona pesa nyingi nilizotumia kuwanyanyua wadogo zangu wa kike na wa kiume.
Kazini nilikuwa mchapa kazi Mkurugenzi wa shirika akanipa cheo kuwa msimamizi wa operasheni. Hapo ikawa kasheshe...wafanya kazi hawanisikilizi wala kutekeleza maagizo yangu. Mimi ni mkristo naamini katika kutenda haki sikuwahi kumwonea mfanya kazi yeyote. Nilifanya kazi kwa kuzingatia miongozo, kanuni, taratibu na ubinadamu. Pia. Nilijipambanua kuwa kiongozi bora lakini ikafika mahala baadhi ya wafanya kazi waliochini yangu kwenda kunisema kwa boss kuwa nawaonea( wafaya kazi hawa wana undugu na boss) nilifanyiwa kikao na Bodi ya wakurugenzi wakasikiliza malalamiko yao na hoja zangu. Wajumbe wa Bodi walikiri kuwa hawaoni Tatizo wala kasoro yoyote ktk utendaji wangu na kwamba malalamiko yaliyopelekwa na baadhi ya wafanya kazi wenzangu hayana msingi hapo nikapona.
Ikaja katika kundi la wateja yaani wapokea huduma zetu. vibwanga kila kukicha. Hata niwape huduma gani basi malalamiko chini kwa chini hayakosi. Wengine Wakinitolea maneno ya dharau pengine kwa mwonekano wangu wa upole na ushamba kidogo lakini kutokana na kazi yangu ya Wito nawiwa kuwa mvumilivu tu na kusonga mbele.
Mke wangu naye hivyo hivyo haoni kama nafanya chochote kwenye familia. Napewa maneno ya kashifa ya kuudhi na kejeli. Mimi silali mchana wala usiku natafuta maisha. Nafanya kazi kampuni nikitoka naunganisha kwenye kazi zangu binafsi ili kuongeza mpunga.
Wazazi wangu nao hivyo hivyo, nawasikia wakinisema wazi wazi vimaneno vya kejeli kuwa maisha yatanipiga. Ni kama wanafurahi au wanatamani yanipige na mimi sipo tayari kwa hilo labda Mungu mwenyewe akatae.
Huku kwenye mahusaiano ya kimapenzi naomba nisiguse kabisa hali ni mbaya mno. Mimi ni wa kuumizwa tuu. Sijui neema ya dunia hii. Wanafaidi wengine.
Ili ku-make maisha mazuri na kulinda afya yangu nilikataa kata kata kunywa pombe wala kilevi cha aina yoyote nilikataa mambo ya wanawake na utumwa wa mapenzi. Mapenzi yangu yoote niliwapa wadogo zangu. Kiukweli wadogo zangu hawa tisa(9) nawapenda sana. Huniambii kitu juu yao nimewalea toka wanazaliwa hadi sasa ni wakubwa wa mwisho yuko form four now.
Kwa kuwa nimefika mwishi sioni Jema wala zuri katika dunia hii sasa Basi! imekwisha.
Nataka nianze kufaidi pesa zangu mimi mwenyewe. Sitaki mtu anisemeshe. Mimi na maisha yangu. Binadamu nimewachoka. Nitakunywa Pombe mpaka nitapike. Nitavuta sigara mpaka mapafu yakome. Nitalala kwenye madanguro. Nitahonga sana. Nataka ku- neurtralize my sadness. Siwezi kuwa mimi ni wa uchungu tu maisha yangu yote. Siwezi kuwa mimi wa majonzi tu mpaka nife.
Lengo la thread hii sio kutaka ushauri wala nini nataka wengine mjue kuwa tuko tunaoishi na machungu tangu tunazaliwa mpaka tunakufa. Ukiona una furaha katika maisha yako basi ilinde furaha hiyo wengine hatuna bahati.
Asalam aleykum.
Kuna watu watakwambia utatenga vipi ndugu, wakati mkeo sio ndugu yako! Lakini maisha mengine ndugu huumiza kuliko mtu baki na ukiwaendekeza utashindwa kujenga familia yako, siku ya siku hao ha watakucheka na kila mtu atakuwa kwake na familia yakeDah tupo wengi mkuu, personally nimepambana sana kuisaidia familia na ndugu yyte mwenye ttzo, hali iliyopelekea kutoinvest sana katika maisha yangu binafsi zaid ya kujiendeleza na shule. Above all, sijawahi kuwa appreciated na wazaz wala ndugu, na ikitokea kuna jambo sijatatua, nakua miongoni mwa watu wa hovyo sana machoni mwao! Nlichoamua kwa sasa, moja, kutulia na wife na kufanya ishu zetu nje ya mkoa wa home, mbili nafanya lile ambalo tu haliathiri mipango yangu! Hata ufanye nn, furaha haitoki kwa ndugu mkuu.....karibu makao makuu ya nchi tulime alizeti (joking)
Sent using Jamii Forums mobile app
Huwatengi ila hufanyi lolote ambalo litaharibu maisha yako binafsiKuna watu watakwambia utatenga vipi ndugu, wakati mkeo sio ndugu yako! Lakini maisha mengine ndugu huumiza kuliko mtu baki na ukiwaendekeza utashindwa kujenga familia yako, siku ya siku hao ha watakucheka na kila mtu atakuwa kwake na familia yake
Ndio tabia ya ndugu utawasomesha kwa kujibana watafanikiwa na kuajiriwa au kujiajiri maisha yao yatakua mazuri wakati wewe unakonda kwa mamikopo uliokopa kuwasaidia halafu Siku utayoomba msaada watakwambia hela zako ulikua unazichezea kwa anasa ndo maana huna maendeleo hapo ndo utajua thamani ya kujiimarisha kabla kusaidia wengineKuna watu watakwambia utatenga vipi ndugu, wakati mkeo sio ndugu yako! Lakini maisha mengine ndugu huumiza kuliko mtu baki na ukiwaendekeza utashindwa kujenga familia yako, siku ya siku hao ha watakucheka na kila mtu atakuwa kwake na familia yake
Na unakuta mpaka wazazi wanamgeuka mtoa misaada na kuwakubali zaidi wanaosaidiwa yaani inaumiza sana, mwanamke anayeolewa na mwanaume ambaye kwao wote wanamtizama yeye daa nimaumivu mpaka basi, yaani kama catapilah linatengeneza barabara ikiwa tayari linabebwa kwenye gar lingine ili lisiharibu hiyo barabaraKuna Uzi niliandika humu kwa nini watu wenye roho nzuri na kujitolea kwa wenzao huishi maisha magumu au kawaida sana kuliko wale waliowasaidia?Tafuta huo Uzi unakuhusu mkuu.Katika dunia ya sasa jaribu kutafuta furaha yako kabla ya furaha ya wengine tunapata maisha magumu kwa kutaka kuwafurahisha au kuwahurumia wengine na kujiumiza wenyewe.
Hawajui hilo na hata siku umekwama utaambiwa unawanyima wewe ni mchoyoHuwatengi ila hufanyi lolote ambalo litaharibu maisha yako binafsi
Sent using Jamii Forums mobile app
Hujakosea ndugu mpaka matusi utapokea, yaani sijui nikitu gani sie ngozi nyeusi mpaka unashindwa kuelewa ni kitu gani!Ndio tabia ya ndugu utawasomesha kwa kujibana watafanikiwa na kuajiriwa au kujiajiri maisha yao yatakua mazuri wakati wewe unakonda kwa mamikopo uliokopa kuwasaidia halafu Siku utayoomba msaada watakwambia hela zako ulikua unazichezea kwa anasa ndo maana huna maendeleo hapo ndo utajua thamani ya kujiimarisha kabla kusaidia wengine
Asante mkuuKuna Uzi niliandika humu kwa nini watu wenye roho nzuri na kujitolea kwa wenzao huishi maisha magumu au kawaida sana kuliko wale waliowasaidia?Tafuta huo Uzi unakuhusu mkuu.Katika dunia ya sasa jaribu kutafuta furaha yako kabla ya furaha ya wengine tunapata maisha magumu kwa kutaka kuwafurahisha au kuwahurumia wengine na kujiumiza wenyewe.
Nakwambia kuna watu utasikia una roho mbaya lakini huo ndiyo kweliMkuu kuna kosa kubwa umelifanya ndilo linalokutesa!!USIBEBE MAISHA YA MTU NA KUTAKA KUYABADILISHA!!!yaani mwache ndugu apambane mwenyewe kwenye mazingira ya kawaida hata shule ya kawaida ili usilipe magharama makubwa mno!!!waache wasome na kupambana katika mazingira ya kawaida atakaefaulu msomeshe shule za kawaida!!!!Pia usibebe maisha ya mtu moyoni boresha kwako na wanao hata wazazi wakichoka uje uwalee kwako!!sio ubadili maisha yao!utahangaika sana na kufeli!!