Nimekoma walahi! Pilau la buku nimelinunua kwa 32,000 za dripu mbili

Nimekoma walahi! Pilau la buku nimelinunua kwa 32,000 za dripu mbili

Usipendelee kula vyakula vya bei chee hasa uswahilin.
Ni bora nishinde njaa ila maeneo haya ya uswazi nitatafuta atleast hotel inayoeleweka ndio nile kama nimebanwa sana.
 
Hali hii leo mbona kazi ipo!

Katika pitapita zangu maeneo flani flani hiv nikasikia sauti kutoka katika kipaza ikinadisha "pilau buku, pilau nyama buku... njoo ujipatie". Nikaona yesss, dunia ni yetu sote.

Nikajikoki pale ndizi ya mia mbili na juisi ya muwa. Nikaketi taratiibu nijipimie. Wallahi punde baada ya kujishindilia pilau la nazi nikasikia "prrr prrrr prrr" tumbo linaunguruma na maumivu kias.

Nikajaa kujishtukia niko mlangoni mwa choo cha msikiti mana hata nauli iliishia kwemye choo cha kulipia. Nikajimaliza pale vya kutoshana nguvu ikatoweka, nikaomba msaada wa pikipiki ya msikiti nikapelekwa hospitali. Hapa nilipo nina drips ya pili na nishamaliza elfu 32 kwa matibabu haya yanayoendelea

Dua zenu wazee
Ukiendelea kujilegeza hapo hospital utapigwa drip hata 5 .
 
Nipo Kaka ,sema siku mbili hizi nilikuwa mpakani huko niliipata mteja wa vidonge vya Arvs ikabidi nimpelekee Kaka nisije kufa njaa kwa watu huku
Ah sawasawa mzee mapambano tu. Muhimu siku zinakwenda kidogokidogo hivyohivyo. Mpakani kuna fursa gan huko? Vijana wana mitaji humu hawana exposure wanang'ang'ania dar alaf haiwalipi.

Fursa fursa huko shea nao wa kujilipua wajilipue tu
 
Hapo mchawi anaweza kuwa Pilau (limechacha kisha likafufuliwa kwa kupikwa upya kwa madiko diko mengine ili kukata mchacho) au hiyo Juice ya miwa (maana usafi wake huwa ni mgumu).
Juice ya miwa napenda ila nawazaga sana wanavyokamua pale na ile mchanganyo na barafu..ila pia kweli hali ngumu , sasa misosi ya buku au msosi chini ya 2000 sh lolote linawezekana ..nyama kwasukwasu, nyanya kwasu, mchele ovyo..kula vya jana vilivyochanganywa na vya leo..ndo mana madiko diko huwa mengi ili kuficha mambo ya radha na harufu
 
Hali hii leo mbona kazi ipo!

Katika pitapita zangu maeneo flani flani hiv nikasikia sauti kutoka katika kipaza ikinadisha "pilau buku, pilau nyama buku... njoo ujipatie". Nikaona yesss, dunia ni yetu sote.

Nikajikoki pale ndizi ya mia mbili na juisi ya muwa. Nikaketi taratiibu nijipimie. Wallahi punde baada ya kujishindilia pilau la nazi nikasikia "prrr prrrr prrr" tumbo linaunguruma na maumivu kias.

Nikajaa kujishtukia niko mlangoni mwa choo cha msikiti mana hata nauli iliishia kwemye choo cha kulipia. Nikajimaliza pale vya kutoshana nguvu ikatoweka, nikaomba msaada wa pikipiki ya msikiti nikapelekwa hospitali. Hapa nilipo nina drips ya pili na nishamaliza elfu 32 kwa matibabu haya yanayoendelea

Dua zenu wazee
Hii kama Mbagala nini pale fremu za kanisa la Roma😆😀😀🤣
 
Kipato kikiwamba mkuu unajishindilia tu 😂
Hapana hapana mdogo angu. Umeona sasa matokeo yake.. ulishindwa bas hata kuomba upimiwe chips za 1500 zimetoka jikon unywe na Afiya au maji ya 500???
Kuna time lazima ujipe thaman bila kujali hali ulionayo.
Mtaji pekee wa masikin ni afya.
SIchezagi michezo ku mess up na afya yangu.
 
Juice ya miwa napenda ila nawazaga sana wanavyokamua pale na ile mchanganyo na barafu..ila pia kweli hali ngumu , sasa misosi ya buku au msosi chini ya 2000 sh lolote linawezekana ..nyama kwasukwasu, nyanya kwasu, mchele ovyo..kula vya jana vilivyochanganywa na vya leo..ndo mana madiko diko huwa mengi ili kuficha mambo ya radha na harufu
Juisi za miwa usafi sio standard japo uchafu ule sio wa kukera au kumpeleka mtu kitandani. Lakin pale kuna muingiliano mkubwa sana na wadudu hasa nzi wa njano na usafi wa miwa au mashine. Mana mashine zinalala nje na miwa haioshwi inaparwa tu
 
Hii kama Mbagala nini pale fremu za kanisa la Roma😆😀😀🤣
Ushaanza sasa! Sijaja kuharibu biashara ya mtu mkuu. Unapita pita mazingira yale? Mm pale njia yangu kila siku naishi hapa chini ya kanisa
 
Back
Top Bottom