Nimeku "miss" kwa kiswahili

Nimeku "miss" kwa kiswahili

Mimi ningependa kweli kama kungewezeka hesabu halisi ya maneno ya kiingereza tukailinganisha na hesabu halisi ya maneno ya kiswahili.

Swali hili ni gumu sana hasa ukizingatia kwamba lugha zote mbili ni "lingua franca", zimechanganya na kutohoa kutoka lugha nyingine nyingi pamoja na vilugha/lahaja za himaya yazo. Kwa hiyo Kiswahili cha Mvita kinaweza kuwa na maneno ambayo hayapo katika kiswahili cha Barawa au Ngazija. Kipi ni kiswahili na kipi kidigo linaweza kuwa swali gumu.

Pengine tunafikiri tu kwamba kiingereza kina maneno mengi zaidi kwa sababu kina historia ndefu zaidi ya kuchapishwa na kimetapakaa dunia nzima, na hatujui maneno mengi ya kiswahili.

Ukiangalia kamusi ya kiingereza - angalau mimi nikiangalia- naona maneno mengi sana yanatumiwa katika vitabu na magazeti, watumiaji wa kiingereza walioelimika kwa kadiri, hususan wale ambao kiingereza ni lugha yao ya kwanza, wanayajua. Hili jambo hunipa matatizo mara nyingine ninapoandika kwa kutumia maneno ya kiingereza ambayo nafikiri kwa kiwango cha mtu anayejua kiingereza cha kubabia kama mimi ni ya kawaida tu, wengine wanaona naandika maneno magumu. Lakini hili laweza kuwa kwa sababu Watanzania wengi si waongeaji wa kiingereza kama lugha yao ya kwanza, na mimi mara nyingine hutaka kuweza uandishi kama wa mtu ambaye kiingereza ni lugha yake ya kwanza.

Lakini nikiangalia kamusi za kiswahili nagundua kwamba maneno mengi sana yanabaki kuwa kwenye kamusi bila kutumiwa katika kiswahili cha kawaida. Sitashangaa nikisikia kwamba kwa kila maneno mawili yanayotumika kila siku kwenye kiswahili, kuna nane mengine hayatumiki na ukiwauliza waongeaji wa kiswahili hawayafahamu.

Kwa hivyo narudi katika swali langu, je tunafikiri kwamba kiingereza kina maneno mengi zaidi ya kiswahili kwa sababu huo ndio ukweli wenyewe au kwa sababu hatukijui kiswahili vizuri?

Kwa hiyo mimi nashauri ukubwa wa lugha tuungalie kwa kuzingatiaa maneno ambayo hasa watu walio wengi wanayajua na wanayatumia katika mawasiliano yao ya kila siku si uwingi wa maneno ndani ya kamusi. Yaliyo ndani ya kamusi yataendelea kutumika taratibu kwa ajili ya kuikuza lugha, ukizingatia kwamba Kamusi huwa inaandikwa na jopo la wataalamu wachache tu kuwakilisha lugha ya watu walio wengi ndani ya jamii husika.
 
Kwa hiyo mimi nashauri ukubwa wa lugha tuungalie kwa kuzingatiaa maneno ambayo hasa watu walio wengi wanayajua na wanayatumia katika mawasiliano yao ya kila siku si uwingi wa maneno ndani ya kamusi. Yaliyo ndani ya kamusi yataendelea kutumika taratibu kwa ajili ya kuikuza lugha, ukizingatia kwamba Kamusi huwa inaandikwa na jopo la wataalamu wachache tu kuwakilisha lugha ya watu walio wengi ndani ya jamii husika.

Hapo utakuwa huongelei ukubwa wa lugha, bali ukubwa wa matumizi ya lugha, vitu viwili tofauti.
 
Ndiyo. Na ninadhani ndiyo topic iliyopo kwenye jukwaa, au?

Topic ni kutafsiri kutoka kiingereza kwenda kiswahili. Kama tafsiri ipo lakini watu wengi hawaijui kwa kutojua lugha kwao wenyewe, kwa mujibu wako wewe, tafsiri haipo.

Unataka kufanya tatizo la watu kutojua lugha yao liwe sawa na tatizo la ufinyu wa lugha, hata kama lugha si finyu bali msamiati wanaotumia watu ndo finyu.
 
Topic ni kutafsiri kutoka kiingereza kwenda kiswahili. Kama tafsiri ipo lakini watu wengi hawaijui kwa kutojua lugha kwao wenyewe, kwa mujibu wako wewe, tafsiri haipo.

Unataka kufanya tatizo la watu kutojua lugha yao liwe sawa na tatizo la ufinyu wa lugha, hata kama lugha si finyu bali msamiati wanaotumia watu ndo finyu.

Kiranga, hapo kwenye bold. Ni matumizi ya lugha. Kujua au kutojua lugha inaashiria matumizi yake.
 
Kiranga, hapo kwenye bold. Ni matumizi ya lugha. Kujua au kutojua lugha inaashiria matumizi yake.

Matumizi ya lugha yanahusu watu, si lugha yenyewe.

Kama lugha ina msamiati mpana na mzuri lakini hautumiki vilivyo, tatizo ni la watu, si la lugha.

Ukisema tuangalia ukubwa wa lugha kwa mujibu wa matumizi, ushaacha kuangalia ukubwa wa lugha na kuanza kuangalia matumizi ya lugha, kitu tofauti, kwa sababu unaweza kuwa na lugha ndogo (kwa maneno) lakini yenye watumiaji wanaoitumia 100% na lugha kubwa lakini msamiati unaotumiwa ni 20% tu.
 
Matumizi ya lugha yanahusu watu, si lugha yenyewe.

Kama lugha ina msamiati mpana na mzuri lakini hautumiki vilivyo, tatizo ni la watu, si la lugha.

Ukisema tuangalia ukubwa wa lugha kwa mujibu wa matumizi, ushaacha kuangalia ukubwa wa lugha na kuanza kuangalia matumizi ya lugha, kitu tofauti, kwa sababu unaweza kuwa na lugha ndogo (kwa maneno) lakini yenye watumiaji wanaoitumia 100% na lugha kubwa lakini msamiati unaotumiwa ni 20% tu.

Sasa hapo si unazidi ku-verify kwamba lugha inategemea watu? How does it "kua" bila watu? Kipi kinamtegemea mwenzake kati ya hivi viwili, mtu na lugha?
 
Sasa hapo si unazidi ku-verify kwamba lugha inategemea watu? How does it "kua" bila watu? Kipi kinamtegemea mwenzake kati ya hivi viwili, mtu na lugha?

Watu ni nani?

Kama Watanzania kwa wastani wanajua maneno 20,000 na kina Mzee Akida na jopo lao TUKI pamoja na watu wachache wa pwani ambao wanafika 5% ya Watanzania wanajua maneno 200,000 ya kiswahili, kiswahili kina maneno mangapi kwa mujibu wa muhtasari huu?
 
Nani anelewa string theory na Nostradamic quatrains hapa. Kuna forum za abstract math tangu lini JF? Forum za molecular physics zimeanza lini hapa?
wasamehe bure wametoka nje ya mada
 
wasamehe bure wametoka nje ya mada

Kuna frequency fulani za fikra kati yangu na Kiranga nimeamua atakuwa tu rafiki wa utani hivi. So kuna mambo mengine mi nitamjibu na wewe usijue ni utani tu.... Kiranga ana utani fulani hivi; na usipomwelewa utalia....
 
Watu ni nani?

Kama Watanzania kwa wastani wanajua maneno 20,000 na kina Mzee Akida na jopo lao TUKI pamoja na watu wachache wa pwani ambao wanafika 5% ya Watanzania wanajua maneno 200,000 ya kiswahili, kiswahili kina maneno mangapi kwa mujibu wa muhtasari huu?

Kwa hiyo bado unasisitiza tutumie idadi ya maneno na si kuangalia matumizi ya maneno ya Kiswahili kama ambavyo watu wanaweza kuyatumia? Ukubwa wa lugha uwe determined na idadi ya maneno yaliyo kwenye Kamusi na yanayoweza kutumika na 5% ya watanzania?
 
Kwa hiyo bado unasisitiza tutumie idadi ya maneno na si kuangalia matumizi ya maneno ya Kiswahili kama ambavyo watu wanaweza kuyatumia? Ukubwa wa lugha uwe determined na idadi ya maneno yaliyo kwenye Kamusi na yanayoweza kutumika na 5% ya watanzania?

Waswahili (na waongeaji wa kiswahili) inabidi tujue kiswahili zaidi.

Na kama hatukijui, tusilalamikie kiswahili kwani kiswahili si tatizo, kina msamiati tajiri na uwezo wa kuunda istilahi mpya kwa uthabiti, tatizo labda ni sisi tusiotaka kukijua na kukitumia.

Mtu mwenye mamilioni ya fedha benki, lakini hajui kuhesabu na hawezi kuyatumia, ukiulizwa kama ana mamilioni ya fedha utasema hana kwa sababu hajui kuyatumia?

Huyu tatizo lake si kukosa fedha, fedha anazo.

Tatizo lake ni jingine, labda ujinga, hajui kutumia akaunti/ ATM etc.

Wewe unataka tuseme hana fedha kwa sababu hajui kutumia ATM, wakati ana mamilioni benki.
 
Kiranga;

You are a fighter, not an arguer. Sasa si hatujui? Na mpaka tujue ndiyo lugha itakuwa imekua!

Unaongelea necessary conditions za lugha kuweza kukua, na si kwamba tuna lugha kubwa simply msamiati usiohesabika umejaa ndani ya dictionary ambao wala hautumiki na yeyote.
 
Last edited by a moderator:
Kiranga;

You are a fighter, not an arguer. Sasa si hatujui? Na mpaka tujue ndiyo lugha itakuwa imekua!

Unaongelea necessary conditions za lugha kuweza kukua, na si kwamba tuna lugha kubwa simply msamiati usiohesabika umejaa ndani ya dictionary ambao wala hautumiki na yeyote.

Hapana.

Unachanganya kukua kwa lugha na kukua kwa matumizi ya lugha, vitu viwili tofauti.

Tuchukue mfano wa kwamba Kiswahili kilikua sana miaka iliyopita kwa sababu hakukuwa na Kiingereza, kikafikia maneno takriban 200,000 yajulikane kwa kila muongea Kiswahili, watu walikipenda kweli.

Kiswahili kishakua hapo.

Halafu baadaye Kiingereza kiingilie, nguvu za lugha za makabila zikue, utashi wa watu upungue, kwa wastani waongeaji wa kiswahili wajue maneno 20,000 tu.

Utasema Kiswahili kina maneno 20,000 kwa sababu ndiyo yanayotumika au 200,000?

Kwa fikra zako unataka tukubali Kiswahili kina maneno 20,000 kwa sababu hayo ndiyo yanayotumika, bila kujali kwamba "maneno yanayotumika" na "maneno yote" ni vitu viwili tofauti.
 
Back
Top Bottom