Nimekuwa nikiumizwa na historia yangu ya nyuma natamani kumwambia ukweli mpenzi wangu lakini nahofia ataniacha

Umepiga kwenye mshono.
 
Hapa nachanganyikiwa kuna wengine wanasema ni heri ninyamaze naweza nikamwambia akashindwa kuvumilia
Unachanyikiwa nini? Hamna namna ataacha kujua maana inaelekea ulikuwa maarufu. Ukinyamaza na akija kujua hasira zake zitakuwa zaidi maana atakuona muongo na mtu ambae humtakii mema. Atafikiria jinsi alivyokuwa anachorwa wakati yeye anaona amepata.

Ukimwambia sasa halafu akakukubali, hamna kitu atakachosikia baadae kitambadilisha msimamo. Na wewe utakuwa huru zaidi kuliko hii ya sasa ya kuishi kwa uoga. Ukiifanya siri, watu wenye nia mbaya wataweza kuitumia ili kukuingiza zaidi kwenye mkenge kwa kuhofia siri kutoka.

Amandla...
 
Sema maisha
Sema maisha uliyoishi kwa uhalisia ili upate ushauri utakao kufaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…