Nimemnunulia mama yangu mzazi zawadi ya nguo Mke atokwa na maneno makali ya dharau

Mkeo ana matatizo lakini pia wewe hukupaswa kumnunulia mama yako nguo wewe sio mume wa mama yako kama baba yako yupo hai ulipaswa umpe yeye hela ndo amnunulie mkewe next time hela zote unazotuma kwenu tuma kwa baba yako
Uko sahihi kabisaaa. [emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
 
Unakosea Sana kumnunulia nguo mama yako ,,

Wewe si mume wake kwamba unayajua mahitaji yake vizuri.

Wala mama yako sio mwanao.

Mpatie mama pesa aangalie vipaumbele vyake,, wala mkeo hapaswi kujua.
True
 
Wewe ndio mume wa mama Yako?
 
Utamnunuliaje mama yako nguo mbele ya mke wako?wanawake huwa hawapendani hata iweje.Ungelitoka na Mama yako kwend adukani kumnununulia nguo pasipo na mke wako kujuw alakini wewe inaonyesha umekwend anao wote wawili kuwanunulia nguo pamoja au umnunulia nguo Mama yako wakati mke wako anaiona hataweza kufurahi hata siku moja.Wanawake huwa wan wibu w akijinga sana jifunze kutokana na makosa uliyoyafanya usirudie tena .
 
Ni kweli Tena sana
Kiukweli mama ni mtu wa kupendwa sana haijalishi ni wa mume au wako haijalishi ana mapungufu kiasi gani

Kunamtu alisema tabiambaya za mkwe wake nikamuuliza angekuwa ni mamayake na madhaifu hayo angemtenga?akabaki kimya

Imagine asingemlea vizuri kumfundisha tabia njema kumsomesha had wew mke kumuoona wa maana,hizo zote ni nguvu za huyo mama

Mungu atusaidie sana
 
Wanawake wachoyo na wenye roho mbaya mnawatoaga wapi? FUKUZA MBWA HIYO
Kabisa my Wii
Mm kma ni mbaya ningempa yangu kabisa au ningemrudisha dukani tukachague nyingine kwaajili yake
Km anauwezo amjengee hata nyumba ni mamayake angemuua mm angenijua huyo mume angemuacha awe chokoraa ningempenda kweli
 
Mkuu kaa Kwa kutumia usiwaambie dada zako(mawifi zake) hakuna Rangi ataacha kuiona Tena ghafla tu hii ligi Huwa ni kubwa mno hakuna aliye wahi shinda Kwa mawifi zake otherwise wewe Mme usimamie nae bega Kwa bega😂😂😂

Hapo issue ni ndogo tu usiruhusu wife ajue Yale yte unayowafanyia ndg zako. Ila wewe unayofanyia ndg zake hata kama umewapata vocha ya jero mwambie.
 
Kataa ndoa wamefika hapa?

Au wamewaachieni dunia iwafunze?
 
Sisi wanawake hatupendanagi hiyo ni nature mama ni mtu muhimu na mke pia angalia jinsi gani ya kuwahudumia pasipo kusikiliza maneno kutoka kwa yeyote mama ana nafas yake na mke ana nafas yake
 
Kabisa my Wii
Mm kma ni mbaya ningempa yangu kabisa au ningemrudisha dukani tukachague nyingine kwaajili yake
Km anauwezo amjengee hata nyumba ni mamayake angemuua mm angenijua huyo mume angemuacha awe chokoraa ningempenda kweli
Kuna wanawake wana roho mbaya za ajabu, sasa mama wa mumeo si ndio wa kumfurahia kwa kuzalia mwanaume wa moyo wako..
 
Kiongozi mke inabidi ajue nafasi yake, yaani kitendo tu cha kumuwazia mabaya mzazi wako ni kosa la jinai, achilia mbali kutamka tena mbele yako.

Jitahidi kutumia busara, hekima na nafasi yako kama mwanaume kumuweka sawa wife.

Maana kwa mazingira hayo hata ikitokea siku mama amekutembelea kwako inaweza kutokea aibu kubwa.
 
Acha ujinga na kutaka kujionyesha kwa mkeo. Ukitaka kumnunulia mama yako mzazi nguo au kitu Fanya mwenyewe kwa wakati mwingine. Kamnunulie nguo kisha mpelekee bila ya mkeo kujua. Si lazima mkeo ajue. Kama hujui umnunulie nini mchukie mdogo wako/dada yako wa kike mwende naye akusaidie kuchagua. Tafuta siku pia kwa ajili ya mkeo. Umeskia?
 
Mimi na ndugu zangu ni damu damu, ikiwa mke wangu huwapendi ndugu zangu yaani mama, na wadogo zangu jiandae kuishi bila mimi.
 
Ni hao wake zenu sio wanawake wote tuko hivyo acheni kujumuisha, mlipata magaidi tulieni nayo lakini sio kutupondea na wengine wenye roho za kimalaika
 
Tena sio kurrudisha tuu kwao na matege na magumu ya kumsindikiza.
Aache ujinga bwana.
Hela yako anakupangia matumizi🙄🙄🙄🙄
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…