Nimeona clip ya Mtanzania mwenzetu Joshua Mollel anauawa na Hamas. Inatia hasira kuona tulipiga kura kuwaunga mkono
NILIKUWA UPANDE WA HAMASA KWA KUSEMA KUWA WANATETEA ARDHI YAO ILA KWA UNYAMA HUU HAPANA KWA KWELI HAUKUBALIKI NA BADO SERIKALI YETU IPO KIMYA..

Endelea kupumzika Joshua
Hujawahi kua upande wa hamas toka uumbwe
Ila tufanye ulikua upande wao unadhani kutoka kwako kutawazuia kuendeleza mapambano yao
Pole kwa familia ya mollel na taifa kwa ujumla
Hamas endeleeni kutetea haki zenu ipasavyo
 
HAMAS ni mgambo walioasi na kutwaa eneo la Palestine, ndiyo maana PLO wanasubiri Israel wamalize operesheni yao halafu Palestine Authority irudi tena kutawala eneo la Palestine la Gaza lililotwaliwa na vikaragosi vya Iran yaani HAMAS.


Viongozi wakuu wa vikundi vya PLO, PFLP n.k vinasubiri siku hiyo ifike waondokane na HAMAS. Kiongozi wa PLO Mahmoud Abbas na baraza lake wanataka kuwa kiongozi wa Palestine moja isiyo na magaidi, Palestine moja iliyokuwa na ukanda wa Gaza na Ukanda wa Magharibi.

HOTUBA YA BW. YASSER ARAFAT ILIYOBATIZWA (KAMA ISHARA YA AMANI) TAWI LA MZEITUNI

Hotuba ya kiongozi wa PLO mwaka 1974 mbele ya Umoja wa Mataifa mwezi November 1974 mara baada ya Palestine moja kukaribishwa kuwa na mwanachama katika Umoja wa Mataifa

View: https://m.youtube.com/watch?v=SQrbPhrPJ7I
(interpretation from Arabic)

Huna unalojua
Hamas ilikaa pale kwauchaguzi halali kabisa mnaoita wenyewe wakidemokrasia
Suala la hamas kufutwa endeleeni tu kuliota maana halitakaa litokee
 
Hamas ilikaa pale kwauchaguzi

10 August 2023
Last Thursday, Abbas ordered the removal of 12 of the 16 regional governors in the West Bank and Gaza. The four governors fired in the Gaza Strip only had a symbolic role, since the PA was violently booted from the coastal enclave in 2007 by Hamas.

Baada ya ushindi huo kwa ahadi kibao, HAMAS imeteka nyara mfumo wa uchaguzi na kuutupilia mbali zoezi la uchagazi hivyo sasa wakaazi wa ukanda wa Gaza hawana tena nafasi ya kupiga kura kwakuwa HAMAS haiamini ktk demokrasia.
Early January, 2021 Palestinian President Mahmoud Abbas issued a decree announcing parliamentary and presidential elections, making it the first Palestinian vote in 15 years. Scheduled to be held in May and July in the West Bank and Gaza strip, these elections appear as a strong signal to the international community that the Palestinian Authority is speeding up its democratic transition. But some remain sceptical as to what this vote will really achieve. We asked Dr. Alaa Tartir, Palestinian researcher, his view on this decision and on the possible outcome : READ MORE : Political Parties READ MORE Will Upcoming Elections Bring Any Change to the Palestinian People?
 
Nimesikiliza mpka mwisho na kinachoonekana ameuwawa kwa sababu ya Lugha Gongana na walimistake kwamba yeye katoka somalia

wengine wanasema hapo na wengine wanasema As-hab" yaanu (أصحاب) Maana yake wanasema ni Mole kutoka Kwa waisrael na anaammbiwa ajitete kama ni kweli kipindi bado hajajibu kuhusu Tuhuma ya kuwa Alshaba kutka somalia Kuna mwengine alidakia kusema Kuwa... Mash" (مش), yaani hapana huyu ni As -hab yaani..
Huyu ni mshirika wa Israel ..

So mabishano yalikuwa ni lugha gongana kama angekuwa anajua lugha nahisi asingefariki maana walijua israel wametuma Watu kupelelza

SO SAD ...KWAKWEL
Sijajua kama umetafsiri sawa sawa ama laah
Ila mwanzo ulivyokuja na kukurupuka hapa???
 
inaumiza sana kwa wanachotendewa wapalestina mtu anafanyiwa uovu na unyama wa hali ya juu akijaribu kujitetea anaonekana gaidi.hakika inaumiza sana kwa anachofanyiwa mpalestina
Wanafanyiwa nn..wakat kila kitu wanapewa free na Israel kuanzia umeme maji chakula..lakin tamaa ndoinawasumbua na roho mbaya za kigaid
 
Hujawahi kua upande wa hamas toka uumbwe
Ila tufanye ulikua upande wao unadhani kutoka kwako kutawazuia kuendeleza mapambano yao
Pole kwa familia ya mollel na taifa kwa ujumla
Hamas endeleeni kutetea haki zenu ipasavyo
Sawa mkuu, Yote unayosema ni mawazo yako na yanalindwa na katiba kwahyo nayaheshimu sana..
Shukrani
 
Niliwahi kusema hapa kwamba Rais alipiga kura kuwaunga mkono Hamas kwa msukumo wa dini wengi mlitoka povu. Kuna video inasambaa ktk mtandao wa X inatisha sana. Moyo wangu unavuja damu mtanazania mwenzetu alitokea shambani na kibaiskeli chake maskini ya Mungu. Anakamatwa najitetea lkn haeleweki kisha anapigwa risasi alaf wanashangilia huku wakisema Alakh akbar.

Kijana mdogo anazimishwa ndoto zake na wajinga wachache alaf et leo Rais anapiga kura kuwatetea wauwaji. Rais Samia damu hii utaijibia... Ulishindwa kuzuia wasimuue lkn hata kulaani mauwaji ya watanzania wenzako umeshindwa? Badala yake umewaunga mkono wauwaji.

Video hyo inaogofya sidhani kama inafaa kuwa shared hapa. Kama unataka unaweza kuingia mtandao X imesambaa sana. Inatia huruma.

R.I.P mdogo wetu
Mbona walioko madarakani wanauwa kila siku? Au Kifo cha mbali kinauma zaidi? Mawazo yuko wapi? Azory yuko wapi? Bint mdogo aliuwawa kinondoni akiwa ndani ya daladala hana hatia yoyote ila wako wapi waliomtoa uhai wake? Tunapaswa kusikia uchungu kwa mauaji ya binadamu yoyote si lazima awe mweusi kama wewe, mjerumani aliuwa wahenga wa nchi hii lakini hata kujali hakuna, huenda tukabadili namna ya kufikiri mambo yetu
 
Nilikuwa naona kama wanaonewa ila baada ya kuona hii clip ni bora Israel waendelee kugeuza Gaza yote kuwa vifusi tuu..
Naam kwa sisi Wakristo wanachokifanya Wazayuni tunakielewa hasa ukizingatia waliasisi hilo kwa manabii, hata dhambi alizotubebea Yesu ilikuwa ni mauaji waliyoyatekeleza wao, kiufupi wanachokifanya ni faraja sana
 
Dah! Mimi ni muislamu safi ila kwa hili napata mashaka sana na hii dunia yetu. Utu umepotea, sasa huyu dogo maskini ya Mungu anamakosa gani jamani.
Mtume Muhammad alipigana jihad nyingi hakuwahi kuruhusu wasio wapiganaji kuuwawa sasa hawa wanatanguliza jina la Allah kivipi.
 
Back
Top Bottom