Sio kila mbuz atakula kwa urefu wa kamba yake wengine hula kwa huruma ya mchungaj wake, wanawake wanajsahau mapema sana kama mlkua kwenye msoto ukipata Chanel anabadlka mpka unajiulza huyu kawaje na kama ulkua na pesa zkapata naul au kaz ikaisha utamwona visa vyake kila kukicha na mabeg yake mgongon kama ngoni migration Leo kwa Dada ake kesho kwao hatulii tena hata ukiongea hakuelew wala kukuskia kikubwa Mungu atupganie tu watoto wa kiume sis
Spikn from Exprienc
Umenena vyema lakini katika kununua vitu in bulk, usije ukafanya kosa la kununua mafuta ya kula mengi.Kama hununui vitu in bulk aisee utamlaumu bure. Hakikisha unanunua chakula kingi,mafuta,sukari na vingine ambavyo havihitaji kutoa hela mfukoni. Na ikiwezekana awe anakuwekea orodha ya vitu unanunua kwa wiki hapo hata elfu 2 kwa siku inatoboa. Muulize pia anamadeni uyalipe huenda pindi mambo hayajakaa sawa alikua anakopa kusupport au kaingia kwenye michezo ile ya vikundi vya wamama daily wanatoana.
Na pia mpe hela mara mojamoja afanyie mambo yake maana lazima kuna vitu alivikosa hasa nguo na vitu vingine vya wanawake na watoto kama unao....anahaki ya ku-upgrade kidogo na kama hujamuweka kwenye bajeti ata-upgrade kwa kuchakachua bajeti.
Mwisho muanzishie kibiashara hata kidogo atajichakachua humohumo
Sio kweli mchele, unga maaharage hajapanda kihivyo nikupe mfano mimi huwa naagiza mchele kutoka kilombero kilo ni gunia la kilo 100 ni 75,000tsh gharama ya kusafirisha mpaka tazara ni 26,000, Mahindi gunia 25,000 usafiri toka kibaigwa 16,000, huo mchele nitakula zaidi miezi 7 na mahindi ni mwaka mzima na napata na makande hapoUkweli maisha yamepanda sana vitu vimekuwa bei juu ila kama unataka kufanya maendeleo mwambie akupigie bajeti ya mwezi mzima kisha wewe angalia katika mshahara wako yaani asitake pesa mpaka mwisho wa mwezi...!! Ikishindikana hapo nunua vitu vyote mchele,unga,sukar,majani ya chai,gesi ao gunia la mkaa,maharagwe kilo 20, Kisha kwa siku acha elfu 3 acheze vicoba
Habarini wapendwa, nimeona watu kadhaa wamekuwa waki share kadhia anuai katika jamvi hili na ushauri mzuri umekuwa ukitolewa ambao nadhani umekuwa msaada kwao.
Moja kwa moja kwenye point. Mimi na wife tunaishi kwenye ndoa, namshukuru Mungu so far tunaishi vizuri sana. Leo nimeona nishare hili na watu wenye experience wanisaidie kwa ushauri na hekima zao.
Ni miaka miwili sasa tangu nimeoana na mke wangu na wakati tunaoana sikuwa na kazi japo nilikuwa na kibiashara kidogo. Kwa karibu mwaka mmoja wife alikuwa na nidhamu sana ya matumizi ya pesa, yaani elfu tano ilikuwa inatosha kabisa matumizi ya ndani kwa siku.
Cha ajabu baada ya kuwa nimepata ajira na thanks be to God mshahara wangu ni mtamu, wife amezidisha matumizi sana. Yaani tofauti na mwanzoni, kwa sasa elfu kumi haitoboi kwa siku.
Imefika wakati laki moja week haiishi, mwanzoni nilimshauri akakubaliana vema, lakini cha ajabu mabadiliko yalikuwa kidogo sana na niliporudia tena kumwambia kuhusu kupunguza matumizi ili tubane matumizi kwa ajili ya future yetu anakuwa mkali na anaona namunyanyasa baada ya kuwa nimepata ajira.
Naomba kwa haya machache, wenye ushauri na uzoefu wa ndoa munisaidie namna ya kufanya.
Asanteni sana
“Aquila non capit muscas”
Ukweli maisha yamepanda sana vitu vimekuwa bei juu ila kama unataka kufanya maendeleo mwambie akupigie bajeti ya mwezi mzima kisha wewe angalia katika mshahara wako yaani asitake pesa mpaka mwisho wa mwezi...!! Ikishindikana hapo nunua vitu vyote mchele,unga,sukar,majani ya chai,gesi ao gunia la mkaa,maharagwe kilo 20, Kisha kwa siku acha elfu 3 acheze vicoba
Pole sana na hongera kwa kuajiriwa na kupata mshahara mnono.Kwa issue ya mkeo,nakushauri mwambie ,akupe mchanganuo wa matumizi ya nyumbani kwa siku.Hii itawezekana kwa kupanga ratiba ya chakula kuanzia J3 Hadi.pili,hivyo mtapata matumizi ya wiki then zidisha Mara wiki nne.Vilevile akupigie mahesabu ya matumizi yake binafsi, malipo ya housegiri(Kama yupo) na vitu vingine ambavyo vipo nje ya ratiba ya chakula. Ukishajua kiasi gani kinatumika kwa mwezi ,mpe hiyo hela yote kila mwisho wa mwezi.Kama kutakua na dharula ambayo imeingilia bajeti atakujulisha ili uweze kuisolve.Ukimnunulia vyakula vyote ukaweka ndani kunawezekano tatizo lisiwe solved kwa maana anaweza akavitumia hovyo ,akagawa na hata kuviuza na bado akakwambia kwamba vimeisha hivyo utalazimika kununua vingine hivyo gharama ya matumizi kuwa juu. Mimi familia yangu Ni ya watu wanne,matumizi kwa siku Ni sh.15000/= hii inacover kila kitu except Kodi,umeme ,maji matibabu na Ada ya watoto.
Miaka2 sio sasa. Umeskia bei ya mafuta ña vyakula ilivyopanda?
Halafu wewe unaweza kuwa mwanaume bahili hadi kwa mkeo kweli!?
Kumbe na wewe unajua kuwa bei ya vitu imepanda plus tozo? Ajabu na kweli!
Kwahiyo sababu ya kuishi mbali mbali ni nini? Biashara?Hapana kiongozi siyo mtumishi
Mkuu mleta mada, kuwa mkweli ujibu swali la wakuu.
"TATIZO LILIANZIA PALE ULIPOMUONESHA SALARY SLIP"
JE NI KWELI ULIMUONESHA SALARY SLIP??
Uwe muwazi
Unayafungia unakua unawamiminia kwenye chupa ya lita moja kwisha mchezoUmenena vyema lakini katika kununua vitu in bulk, usije ukafanya kosa la kununua mafuta ya kula mengi.
Mimi nilikuwa natoka safari nahakikisha nimeleta madumu ya lita 5 kama matano na ninaweka ndani. Baada ya muda ambao hutegemei, unaambiwa mafuta yameisha.
Matumizi mabaya ya mafuta kwenye chakula ni tatizo kubwa kwenye familia zetu, hata umwambie house girl vipi, yeye haelewi.
Usije ukanunua mafuta mengi kwenye nyumba yako. Utauwa familia yako.
Baada ya hapo nilijaribu hilo swala, lakini nikaja kugundua hata ufanye nini kama house girl haelewi umuhimu wa kutokuweka mafuta mengi kwenye msosi, yote yanakuwa kazi ya bure.Unayafungia unakua unawamiminia kwenye chupa ya lita moja kwisha mchezo
Mpaka umeme umepanda!!!Mkuu gharama za maisha zimepanda.
1. Mchicha ulikuwa fungu 1 TSH Mia 2 sasahivi Ni buku
2. Mafuta ya kula Lita ilikuwa Elfu 3 sasahivi Lita Tshs elfu 5
Bado Nyanya ,vitunguu na viungo vingine mkuu Hana matumizi mabaya Bali gharama za maisha zimepanda sana