Nimepata mshtuko mkubwa Ubungo Bus Terminal leo alfajiri!

Nimepata mshtuko mkubwa Ubungo Bus Terminal leo alfajiri!

Choo kipo, ila ww inaonekana sio mtumiaji mzuri wa hii stend ya ubungo....ndio maana umepata huo mshtuko. Ila naungana na ww stend haieleweki yaan kwa mgeni anapata tabu sana kujua wapi pa kutokea na kama amefuatwa mfano ww hukujua mabasi ya kondoa wapi yalipo... Kingine ndio hiko pa kukosekana kwa mahali pa kupumzikia hakuna hata vibanda vya kupumzika au kujikinga na jua au mvua.....wale mawakala wa magar nao wanaboa sana yaan stend inashindwa na ile ya dodoma au mbeya au morogoro
Siku Nyingine Usilinganishe Msamvu Na Huu Upuuzi Wa Dar Au Mwanza Arusha Nitakupopoa Mawe Pamoja Na Kuwa Ujenzi Unaendelea Msamvu Ndiyo Stand Nzuri Kuliko Zote Tanzania
 
Nilienda hapo jana mdada ananikingia mikono nitoe kiingilio, niliwaza sana nalipia kitu gani hapo! Niliamua kumwambia huyo dada nasafiri na nikapitiliza bila cha kuonyesha tiketi wala nini, hivi pale mtu unalipia nini? Na wanaotoza hela hawaoni hata aibu!!!!
 
Narudia maoni yangu kwa Jiji kuhusu UBT ingawa nakiri kwamba mimi sio mtaalamu wa mipangomiji.
1. Jengeni terminal Kinondoni, Temeke, Ilala, Kigamboni na Ubungo yenyewe; ili mtu akitoka bara akate ticket ya kule aendako, sio aishie Mbezi halafu atafute usafiri wa kumfikisha Temeke, Kigamboni nk.
2. Lengo ni kupunguza msongamano kwenye terminal na miundombinu Jijini. Mtu anaetoka Mwanza na safari yake inaishia Kigamboni, kwanini alazimike kushuka Mbezi au Ubungo? Hamuoni kwamba ni usumbufu? Vilevile mtu yuko Kigamboni au Mbagala anaetaka kwenda Mbeya, kwanini asipate usafiri hukohuko wilayani na kupitia njia za mkato (ring roads) kuunganisha Mbezi au Kilwa road bila kuingia CBD?
Si hivyo tu, kuna wasafiri wa kupita (transit passengers) kwa mfano toka Kigoma kwenda Zanzibar, huyu naye munataka ateremkie Mbezi, halafu apande commuter bus au taxi hadi bandarini! Usumbufu wote wa nini?
3. Anzeni kuplani transit connectionability kikanda na kimataifa. Ili huko mbele MTU aunganishe toka Lusaka hadi Zanzibar au Temeke au Tangibovu. Haina tija kusafiri toka Mwanza hadi Dar kwa treni ya mwendo kasi halafu utumie masaa kibao kufika Tangibovu.
4. Anzeni kubuni multilevel, multipurpose terminal structures kwa maeneo husika, kwa kuzingatia mahitaji ya sasa na miaka 50-100 ijayo. Sio kwa staili ya zimamoto kama ilivyo sasa.
5. Lazima kuwepo coordination kati ya stake holders ili kuepusha viroja kama vya DRT-UDA pale Ubungo na Msimbazi.
6. Pamoja na hayo sidharau kazi mliyonayo, ni kazi ngumu inayohitaji ueledi, elimu na upeo mkubwa. Naamini mnajituma sana.
 
Management mbovu ni tatizo kubwa tanzania na africa kwa ujumla!!! ...naisubiri kwa hamu stendi mpya ya msamvu itakavyokuwa baada ya miaka mitano yangu macho
 
Narudia maoni yangu kwa Jiji kuhusu UBT ingawa nakiri kwamba mimi sio mtaalamu wa mipangomiji.
1. Jengeni terminal Kinondoni, Temeke, Ilala, Kigamboni na Ubungo yenyewe; ili mtu akitoka bara akate ticket ya kule aendako, sio aishie Mbezi halafu atafute usafiri wa kumfikisha Temeke, Kigamboni nk.
2. Lengo ni kupunguza msongamano kwenye terminal na miundombinu Jijini. Mtu anaetoka Mwanza na safari yake inaishia Kigamboni, kwanini alazimike kushuka Mbezi au Ubungo? Hamuoni kwamba ni usumbufu? Vilevile mtu yuko Kigamboni au Mbagala anaetaka kwenda Mbeya, kwanini asipate usafiri hukohuko wilayani na kupitia njia za mkato (ring roads) kuunganisha Mbezi au Kilwa road bila kuingia CBD?
Si hivyo tu, kuna wasafiri wa kupita (transit passengers) kwa mfano toka Kigoma kwenda Zanzibar, huyu naye munataka ateremkie Mbezi, halafu apande commuter bus au taxi hadi bandarini! Usumbufu wote wa nini?
3. Anzeni kuplani transit connectionability kikanda na kimataifa. Ili huko mbele MTU aunganishe toka Lusaka hadi Zanzibar au Temeke au Tangibovu. Haina tija kusafiri toka Mwanza hadi Dar kwa treni ya mwendo kasi halafu utumie masaa kibao kufika Tangibovu.
4. Anzeni kubuni multilevel, multipurpose terminal structures kwa maeneo husika, kwa kuzingatia mahitaji ya sasa na miaka 50-100 ijayo. Sio kwa staili ya zimamoto kama ilivyo sasa.
5. Lazima kuwepo coordination kati ya stake holders ili kuepusha viroja kama vya DRT-UDA pale Ubungo na Msimbazi.
6. Pamoja na hayo sidharau kazi mliyonayo, ni kazi ngumu inayohitaji ueledi, elimu na upeo mkubwa. Naamini mnajituma sana.
Unaelewa maana ya "terminal" mkuu?. Sijakuelewa hata kidogo unaposema kuwa kuwe na terminals kigambon,temeke,ilala sijui na wapi ili mtu wa kigamboni anayetaka kwenda Songea apande basi huko huko na aliyeko magomeni anayetaka kwenda Songea anapandia basi wapi?
 
hivi kwa bahati mbaya umeangusha buku katika sakafu ya choo cha ubungo utaokota? maana ile harufu mule ndani ukitoka lazima pua iwe inachoma choma
 
Back
Top Bottom