Nimepewa kiwanja na Baba mkwe wangu naombeni ushauri nikijenge au nikiache kwa muda ila yeye amesema nijenge

Ushaanza ujenzi
 
Mtego huo, mwanaye akianza kukuendesha usishangae
 
Usiogope Cha msingi muangalie usoni umwambie Leo upo kesho unaweza kuwa haupo tuandikiane kuwa nimenunua hiki kiwanja kwa kiasi kadhaa kutoka kwa ndugu flani kistaraabu tu akikataa basi jua ulikuwa mtego Mali za mzee ni Mali za familia yake sio yako
 
Kichukue na kabadilishe hati fasta isome majina yako
 
Depends kama yeye ameweza kukupa zawadi na wewe pesa unayo unaweza na wewe kujenga hata la kutokea likitokea unakuwa umejengea watoto wako au babu yao hata akiwepo inakuwa ni mali yao..., hata ukifukuzwa watoto Wako / Wajukuu zako wana sehemu pia...

Ila kama hiki ndio cha kwanza unajichanga kuna risk fulani inaweza kutokea (hakuna ajuaye kesho); hata akisema kwanini hujengi huku utasema kwanza kilikuwepo hiki najenga nikijichanga zaidi tutasaidiana kujenga na huko... Busara / Wisdom is the key kuweza kuishi vizuri na watu...
 
Mjengee nyumba mkeo hilo eneo, hati ibadilishwe jina liwe la mkeo na mfanye kama asset ya kuchukulia mikopo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ