Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Usisikitike kimsingi pengine alitupia vitu bila kula sababu unaijua nakwann hamkuchukua hatuaKinachosikitisha ni kuwa sitamwona wala kuongea naye tena kwa sababu ya kitu kidogo kinachoitwa pombe; alikuwa ni toka nitoke wangu.
Nashukuru kunitia moyo nisisikitike. Ila kuhusu kunywa bila kula ndiyo tabia mbaya inayosikitisha; alikuwa na financial support kubwa sana kiasi cha kuweza kupata chakula cha aina yoyote anayohitaji lakini yeye alipenda pombe zaidi.Usisikitike kimsingi pengine alitupia vitu bila kula sababu unaijua nakwann hamkuchukua hatua
Uko sawa na G- msigwa anarafikiake mbinga huko anaitwa John chapombe balaa akija kufa nae atalalamika
Unaweza fikiri msukule wake ,akienda ruvuma hawezi rudi bila kumtafuta msela wake ,hatakama atakuwa kuchoma mkaa au kafata pombe vijiji vya jirani
Madhara ya vita sio lazima yatokee vitani. Vitani watu wanafanya mengi, wanafanyiwa mengi na wanaona Mengi. Inaweza kuchukua muda ... Kutafakari, kuapata maoni/maoni mapya nk.Ninakubaliana na wewe kumfichia aibu yake, lakini sidhani kama kuna anyemfahamu personally hapa, kwa hiyo hii nji habari kwa watu wote wanaoweza kupata cha kujifunza kuhusu ndugu wenye tabia hizo. Elewa kuwa ni ndugu yangu toka nitoke; kwa hiyo usidhani ninaandika kwa furaha.
Tabia ya pombe haikutokea vitani; aliporudi alitulia na kujenga familia yake vizuri; huu unywaji wa hovyo ni tabia ya aliyejenga ukubwani.
Umekumbuka shuka kumekucha.Jana nimepoteza kaka yangu niliyekuwa namfuatia; yeye alikuwa anaishi kijijini ambako ameishi tangu aliporudi vitani mwaka 1980. Alikuwa mtu mzima sana; kinachonisikitisha zaidi ni sababu ya kifo chake.
Alikwenda kunywa pombe za kienyeji na kendelea kunywa kwa siku mbili mfululizo bila kula; aliporudi nyumbani baada ya siku hizo akaenda kulala na hakuamka tena.
Ndugu yangu huyo alikuwa na matatizo sana ya kuhimili pombe kiasi kuwa ukoo wote ulimkatia tamaa; kwa bahati mbaya sana yeye ndiye aliyekuwa amebaki mkubwa peke yake kwenye ukoo huko kijijini, kwa hiyo hakukuwa na mwenye sauti juu yake. Nimeanza kufikiri kuwa huenda mimi ningekuwapo mara kwa mara pale kijijini huenda asingepotoka kufikia kiasi cha kupoteza maisha yake kwa njia ya aibu namna hiyo.
Ukiwa na ndugu mwenye tabia za marehemu kaka yangu, jitahidi uwe unatenga muda wa kumshauri mara kwa mara kuhusu pombe asitumbukie kwenye janga lililotufika sisi.
Kazi ya Mungu haina makosa
Mungu ampumzisha roho yake anakosatahili
Alirudi akaenda kulala moja kwa moja; mke wake alikuwa amezowea tabia hiyo ila safari hii inaonekan ilikuwa zaidi.Hakuwa na familiya ya kumuhudumia alipo rudi? Kwa nini hawakumpa chakula, supu, juice za ku dilute pombe? huyo alikufa kwa njaa.
PTSDMfichie aibu yake, sio kuitangazia Dunia. Huenda ni madhara ya vita. Vita vina mambo mengi!
Hapana, una miss point kubwa hapo. Elewa hakuna mwana JF anayemfahamu marehemu na wala jina lake halijatanjwa kuweza kusema nimedhalilisha. Point kubwa hapo ni lile somo litokanalo na nature ya kifo chake ambalo linawahusu watu wote.marehemu anangwi ndugu ulichokifanya hujaonyesha ukomavu na kupevuka kiakili
pole na msiba MUNGU awape moyo wa uvumilivu kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wemu