Nimeshangaa kumuona Profesa mmoja maarufu wa pale UDSM akisali sala ya Bikira Maria

Nimeshangaa kumuona Profesa mmoja maarufu wa pale UDSM akisali sala ya Bikira Maria

Haya shikilia hapa kwanza. Je, 54 AD na 90 AD zilikuwa bado ni nyakati za Yesu? Kama enzi za Yesu zilikuwa zimeshapita, hayo sio mapokeo?
Kwahiyo mimi leo nikiandika kuhusu kifo cha Nyerere yatakuwa ni mapokeo au facts? Walioandika habari za Yesu walikuwa mashuhuda (isipokuwa Luka) hivyo sio mapokeo bali ni facts.
 
Kwahiyo mimi leo nikiandika kuhusu kifo cha Nyerere yatakuwa ni mapokeo au facts? Walioandika habari za Yesu walikuwa mashuhuda (isipokuwa Luka) hivyo sio mapokeo bali ni facts.
Inategemea na umri wako maana Nyerere amefariki miaka 23 iliyopita. Kama ulikuwa na akili timamu wakati akipigania uhuru miaka hiyo ya 1950s na ulishuhudia, basi sio mapokeo.

Lakini kama umesoma katika historia kuwa alikuwa akipigania uhuru miaka hiyo ya 1950s, basi hayo kwako ni mapokeo. Sasa baada ya maelezo hayo ujipime, kama harakati za kupigania uhuru za Nyerere kwako ni mapokeo au ulishuhudia ukiwa na akili za mtu mzima miaka hiyo

NB: Mimi miaka hiyo nilikuwa sijazaliwa, kwangu harakati za uhuru nikiziandika nitakuwa ninaandika mapokeo
 
Inategemea na umri wako maana Nyerere amefariki miaka 23 iliyopita. Kama ulikuwa na akili timamu wakati akipigania uhuru miaka hiyo ya 1950s na ulishuhudia, basi sio mapokeo. Lakini kama umesoma katika historia kuwa alikuwa akipigania uhuru miaka hiyo ya 1950s, basi hayo kwako ni mapokeo. Sasa baada ya maelezo hayo ujipime, kama harakati za kupigania uhuru za Nyerere kwako ni mapokeo au ulishuhudia ukiwa na akili za mtu mzima miaka hiyo
NB: Mimi miaka hiyo nilikuwa sijazaliwa, kwangu harakati za uhuru nikiziandika nitakuwa ninaandika mapokeo
Huo ulikuwa ni mfano na nimeongelea kuandika kuhusu kifo cha Nyerere na sio harakati za kupigania uhuru. Mimi kwa umri wangu nikiandika juu ya kifo cha Nyerere itakuwa ni facts kwasababu nilikuwa kijana mwenye kujitambua miaka ile.

Sasa tukirudi kwenye hoja yetu, walioandika kuhusu Yesu Kristo walikuwa ni mashuhuda kwahiyo yale sio mapokeo. Na kimsingi jambo lolote linaloitwa mapokeo linatokana na tamaduni za watu na sio neno la Mungu. Mambo mengi ya roman catholic ni mapokeo ya kipagani yaliyoingizwa kuanzia miaka ya Constantine.

Mbaya zaidi Luther alipokuja kuhoji roman catholic wakagoma kutubu ila wakaamua kuongeza vitabu ambavyo vinashabikia mambo yao ya upotofu hali wakijua kwamba hivyo vitabu vyote vilikataliwa na wayahudi na pia vilikataliwa na mabaraza ya kanisa la mitume na church fathers.
 
kasome kwanza Luka 1:26-28, Luka 1:39-45, Luka 1:8, Wafilipi 2:8-11
Mtoa mada kanyofoe kwanza vifungu hivi kwenye Biblia(yaani Biblia yako ije ambayo haina haya maandiko) alafu ndio uje na msimamo wako tumalize ubishi😀😀
 
Mtoa mada kanyofoe kwanza vifungu hivi kwenye Biblia(yaani Biblia yako ije ambayo haina haya maandiko) alafu ndio uje na msimamo wako tumalize ubishi😀😀
Viweke hapa hivyo vifungu halafu iweke na ile sala ya maria awaombee sasa na saa ya kufa kwenu tuone kama vinaendana.
 
Mimi kwa umri wangu nikiandika juu ya kifo cha Nyerere itakuwa ni facts kwasababu nilikuwa kijana mwenye kujitambua miaka ile.
Watoto wako nao watayachukuliaje maandiko yako, kwamba walishuhudia kifo cha Nyerere au kama mapokeo kutoka kwa mzazi wao?
 
Watoto wako nao watayachukuliaje maandiko yako, kwamba walishuhudia kifo cha Nyerere au kama mapokeo kutoka kwa mzazi wao?
Mimi sikuwepo wakati wa mkutano wa Berlin lakini uwepo wa ule mkutano ni fact na sio mapokeo.

Maandiko yaliyoandikwa na mashuhuda sio mapokeo bali ni taarifa na historia.

Mapokeo ni tamaduni za watu ambazo zinataka kufanywa sheria na hatimaye kuzipinga hata sheria za Mungu.
 
Mapokeo ni tamaduni za watu ambazo zinataka kufanywa sheria na hatimaye kuzipinga hata sheria za Mungu.
Kama definition yako ya mapokeo ni hii, basi tuishie hapa kwa ishu ya 'mapokeo' maana tunaelewa tofauti
 
Kuheshimu haimaanishi kuwa upotofu usisemwe!

Sent from my 2201116TG using JamiiForums mobile app
Kwako ni upotofu.. lakini kwao si upotofu..
Mfano Kuoa wanawake zaidi ya mmoja kwa wakristo ni upotofu but kwa Islam si upotofu...
Hivyo basi imani ya mtu kwake si upotofu.. anacho amini ndicho na Haoni kama amepotoka.
 
Moja kati ya mambo ambayo yapo wazi kabisa katika biblia ni maelekezo ya namna maombi yanatakiwa kufanywa. Agizo la maombi lipo very open.

Yesu Kristo alisema mara nyingi sana kwenye injili ya Yohana kwamba tuombe kwa jina lake. Mtume Paulo ameandika tufanye yote katika jina la Yesu Kristo.

Sasa profesa ambaye ameandika paper kibao na amefanya literature review za kutosha ameshindwa kusoma biblia kufahamu tunapaswa kuomba kwa jina gani?

Hakuna sehemu hata moja mitume waliomba kwa jina la Maria. Yule Maria mama wa Yesu alikaa pamoja na mitume na walijazwa Roho Mtakatifu pamoja na wakanena kwa lugha.

Maria alimzaa Yesu lakini hakumzaa Mungu. Kuna tofauti kati ya Yesu na Kristo. Maria sio mama wa Mungu bali ni mama yake Yesu. Yesu ni mwanadamu na Kristo ni Mwana wa Mungu.

Hivyo Yesu Kristo ni Mungu na mwanadamu kwa wakati mmoja. Asomaye na afahamu.

Hiyo ni imani ya kanisa katoliki. Ambalo linatawala dunia miaka nenda miaka rudi..

Sasa unashangaa kwa huyo mtu mmoja?

Tupo bilioni 1.6
 
Hata historia ya kanisa huifahamu. Kuna tofauti kati ya catholic (kanisa la ulimwengu) na roman catholic (mkusanyiko wa wapagani wanaojiita kanisa).

Constantine ndio aliyeanzisha roman catholic ambayo ilikuwa corrupt tangu inaanza na kipindi inaanzishwa tayari biblia ilishakuwa iko kamili ikiwa na vitabu 66 alivyovifanyia compilation Jerome.

Sio kweli, Marko imeandikwa AD 54 na injili ya mwisho ya Yohana inakadiriwa ilikuwa imeshaandikwa kufikia AD 90.

Nyaraka ndio ziliandikwa mapema zaidi maana Paulo alikufa mwaka 64AD na hapo alikuwa ameshaandika zote zakwake hadi mtume Petro tayari alikuwa amewahi kuzisoma kabla hajaandika nyaraka zake na ukumbuke mtume Petro naye alikufa around AD 64 na 66.

Kwahiyo nyie mmeamua kufuata yale yasiyoandikwa ambayo hayajulikani?,[emoji23] Hebu acheni uasi, mnaongeza maneno na hukumu yenu inaongezeka.
Wewe ni mweupe kweli, Constantine alianzisha Kanisa kivipi wakati alikuta Kanisa? Aliundaje? Alipounda hilo Kanisa, Kanisa Katoliki ambalo lilikuwepo tayari liligawanyika au aliteua maaskofu wake wapya kikazaliwa kitu kipya?

Huu uongo ndio ambao wana theolojia nguli wakitafiti na kugundua ni uongo wanaacha na uprotestant! Ni uongo mwepesi sana. Naomba ujibu maswali yangu hapo bila kurukaruka, straight to the point.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Nilidhani unashangaa professa kusali kabisa.

Yani mtu amesoma halafu bado anaamini akifumba macho kuna invisible man hewani huko juu ya mawingu anamsikiliza na atakuja kumsaidia???

Kweli sisi bado tuna unyani fulani ndani yetu.
Ndomaana wanasema DNA ya Binadamu na ya nyani vinapishana 2% tu
Tatizo watu hawapendi kuambiw ukweli kuwa dini zililetwa na wakoloni ili kututawala huo ndio ukweli
 
duuuh!!!, kweli jukwaa sasa hivi limevamiwa!!!!. na wasiosali kabisa atawachapa viboko!!??!!
 
Wewe ni mweupe kweli, Constantine alianzisha Kanisa kivipi wakati alikuta Kanisa? Aliundaje? Alipounda hilo Kanisa, Kanisa Katoliki ambalo lilikuwepo tayari liligawanyika au aliteua maaskofu wake wapya kikazaliwa kitu kipya?
Alichofanya Constantine ni kutangaza kwamba ukristo umekuwa imani official ya roman empire hivyo kila mtu ni lazima awe mkristo.

Matokeo ya hili tamko ni kuingizwa katika kanisa watu wasiokuwa na imani ndani ya Kristo Yesu. Hapa ndio matendo ya upagani yakaanza kushamiri katika kanisa lililokuwa ndani ya roman empire.

Baada ya hapo maaskofu wa Greece wakajitenga na kukataa mwelekeo wa kanisa la rome yakazaliwa makanisa ya orthodox. Pia wakati ule Alexandria pia kanisa lilikuwa kubwa nalo lilipinga mwenendo wa kanisa la rome.

Mambo ya ajabu yakaanza kuingizwa kwenye kanisa la rome (roman catholic) na yakazidi kukua mpaka kipindi cha reformation cha martin luther. Mbaya zaidi badala ya roman catholic kutubu walichokifanya ile miaka ya 1500s ni kuingiza vile vitabu vilivyokataliwa na wayahudi na mabaraza ya kanisa pamoja na early church fathers ili tu kulinda mapokeo yao.

Hii haimaanishi kwamba maaskofu wote waliokuwepo rome kipindi cha Constantine walikuwa waasi, hapana. Wengi waliendelea kuwa waaminifu kwa Mungu na maandiko ya biblia lakini walizidiwa na uwepo wa watu wengi walioingia ghafla kwenye kanisa. Na shida kubwa ilikuwa wale matajiri na viongozi wa kiserikali ambao walitaka waonekane bora na kubadilisha mafundisho ya kikristo.

Kwahiyo mabadiliko yaliingia taratibu kuanzia kipindi cha Constantine na kanisa la roman empire likazidi kupoteza mwelekeo na kuwa genge la wapagani ambao walikuja kugeuka na kuwa na mapapa wengi tu waliokuwa wanaua wakristo kwa maelfu.

Hii ndio roman catholic iliyopo sasa hivi isiyokuwa hata na aibu inamuomba Maria awaombee kinyume kabisa na maandiko ya biblia. Hii ndio roman catholic yenye masanamu ndani yake. Roman catholic inayoombea wafu kinyume na biblia.

Niishie hapa.
 
No wonder mnapenda kumuita mama wa Mungu wakati mnajua fika maria hakumzaa Mungu bali alitumika tu kutengeneza mwili.
Bikra Maria hakutumika bali alishiriki umwilisho wa Mwana wa Mungu na alimzaa kwa uchungu na kumnyonyesha huyo Yesu ambaye ni Mtu kweli na ni Mungu kweli.

Mtu unayeweza kusema alitumika ni Yusuf baba mlishi wa Yesu. Yeye alikuwa mtu wa kupewa maelekezo tu na kutii. Huyo ndo aliyetumika. Lakini Maria hakutumika bali aliteuliwa na Mungu kushiriki ukombozi wa wanadamu.
 
Hiyo tu? Haishangazi, bora huyo anaitawa profesa kwa kusoma elimu ya kidunia. Shangaa anayeitwa profesa wa dini kama hiyo na anaamini kitu ambacho nh hadithi tu zisizo na uhalisia
 
Dini ni mfumo wa mahusiano kati ya Mungu na mwandamu.

Nisuala la hiari na kuamini, sasa sidhani kama kuna umuhimu wa kuingilia Imani ya mtu mwingine kama wewe hakudhuru kwa Imani yake.
Hakupigii makelele na wala hakufanyi ushindwe kupata mlo wako.

Nadhani mtu anaehangaika na Imani za watu wengine ambao hawajahangaika na Imani yake anakua anashida ya kutaka kila mmoja awe na Imani kama yake na huo ni udikteta kwenye nchi yenye Uhuru wa kuabudu.
Na hawa watu wa aina hii tunawafehemu.
 
Back
Top Bottom