Nimeshangazwa na kauli ya Rais kudharau msimamo wa Waziri wa Kilimo juu ya kuzuia uagizaji wa sukari nje

Waziri hana mamlaka ya kuweka sera kama yake waziri anatekeleza yanayoamuliwa na baraza la mawaziri au sera ya serikali. sasa ajibu aliambiwa na nani hatununui sukari ya Uganda au ilikuwa uamuzi wake yeye
Kama hajakuelewa hapa basi hawezi elewa tena.
 
Tatizo mmatafsiri vibaya neno Nonsense.Nonsense kwa kiswahili maana yake ni kitu ambacho hakiingiii akilini,sasa hili neno linaubaya gani?.
Acha uongo. Nonsense ni upuuzi.
 
Tunalinda viwanda vya ndani vyenye uwezo mdogo kwa gharama kubwa sana na kwa kubebesha mzigo wananchi. Sukari ikiingia kutoka Brazil bei yake haitazidi TSH. 1800, ukilinganisha na bei ya sasa ya TSH 2600 hii si kulinda viwanda vya ndani bali ni rushwa. Mambo ya monopoly yalishaisha zamani! Kwanini tunalinda viwanda vya sukari tu na vingine vinashindana na vya nje kama kawaida. Natamani kujua viwanda vya sukari vinamilikiwa na nani maana vilibinafsishwa.
 
Hoja ya Fimbo ya asali imesimama. Wakati mwingine sio lazima 2+2=4.
 
Museveni hana.viwanda vya kuzalisha sukari nyingi, Uganda wanaagiza sukari kutoka Brazil na hivyo wanakua na excess ya sukari kutoka Brazil na ndio hiyo wanataka kutuuzia.
Sasa kwa nini sisi wenyewe tusiagize kutoka Brazil, hangaya anafeli sana
Kama utaweza thibitisha hilo utakuwa sahihi.
 
Hivi wakati wa tumbua tumbua ulikuwa umezaliwa?
Wakati waziri mkuu anadhalilisha kwenye kikao chake mwenyewe na wafanyabiashara ya korosho ulikuwa hospital?

Mwacheni mama afanye kazi , acheni chokochoko za kipuuzi!
Binadamu ameumbwa kusahau lkn Wacha tuishi nao hawa ndg zety
 
Heri sisi tuliona na kusikia lakini kwa nchi hii sitegemei kuona kiongozi yoyote yule kujiizulu maana uwezo wa wakufukiri kwa watumishi wetu siyo wa kiuwajibikaji
 
Na kwakuongezea tu Museven ndio mmiliki wa viwanda vya sukari huko Uganda karibia vyote
 
Huyo waziri zaidi ya nonsense kwelikweli, alitakiwa awe ameachia ngazi hadi sasa lakini lilivyo zoba hadi sasa liko ofisini
 

Hapo hapo mnaongelea kutunza mazingira ukame au global warming wakati unapromote Sukari iliyosafirishwa kutoka Brazil kuhuka mito, bahari kibao mpaka Tanzania badala ya iliyozalishwa hapa nyumbani.

Hivi haya mambo huwa mnayaelewa lkn au mnajiropokea tu mkisikia wengine wanasema ?

Kwa nini Sukari ktk Brazili iuzwe rahisi hivyo ? Au ndiyo maana ya kufungua nchi huko ?

Chuki mbaya sana !
 
Report ya sukari 2015 ilionyesha Tanzania tuna uhaba mkubwa wa sukari tokea 1989.
Pia solution sio kuagiza bali ni kuviwezesha viwanda vizalishe zaidi.
Athari za kuagiza Sana ni kubwa kiuchumi kuliko za kuzalisha wenyewe ndani.
Chini nimeweka kipande Cha report ya sukari 2015
 
Mimi nitakujibu hapo kwenye haya yako ya kwanza,hivi unajua wafanyabiashara wengi wa kanda ya Ziwa Mwanza,Mara,Geita,Shinyanga na Tabora mizigo yao kama nguo,viatu na mingine wananunua Uganda,wakati hiyo mizigo inapita Dar
Hiyo issue ya hao wafanyabiashara naijua vizuri lkn sitabishana nawe baada ya kuacha takwimu na kuongelea nguo. Jamaa kasema hakuna viwanda huko mimi nikaonyesha kuwa vipo na wanabakiza maana wao wanahitaji tani 360,000 tu kwa mwaka. Hii ndiyo issue ya muhimu hapa
 
Tutaletewa sugar Brazil zilizo kwisha muda wake zikiwa na package kutoka Uganda , tuta agizaje sukar kutoka nje wakati viwanda vina jengwa bagamoyo vya Azam naNssf vyote anaenda kuviua kwa faida ya wa chuuzi
Juzi kati nilikutana na vijana wale wa dampo wazungusha mchele kwa wafuga kuku mtaani, uko kwenye viroba vimeshonwa vizuri ila ume expire!

Kuangalia kile kiroba kimeandikwa Pakistani

Yani hebu imagine hii nchi tunaagiza mchele toka pakistani?

Hii ni laana ama nini?
 
Mkuu unahisi wewe una taarifa sahihi kuliko Rais wa Nchi?????
Hapo unamaanisha raisi hawezi kukosea? Kama raisi ana taarifa zote kuhusu nchi inakuwaje huwa anakosea kosea Sana? Mfano alisema wenzake na mbowe wamehukumiwa.
Lakini pia kuhusu suala la sukari ni kweli Uganda wao wanaagiza Brazil, hata Kenya waliwahi kukataa hili kwa kuwa wanachofanya ni ujanja.
 
Prof kwa kulinda heshima yake, bora akae pembeni. Dunia kizungumkuti sana.

Huku mnasema wawekezaji njooni. Huku mnawapiga sindano ya ganzi
Hawa maprofesa huwa wanaona shida gani kujiuzulu ili kulinda hehima zao
 
Kongore Mkuu uko vizuri kwa fact hizo akirudi huyu mpiga kelele atakuwa punguani..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…