Nimeshangazwa na kauli ya Waziri mwenye dhamana ya mitandao ya kijamii kuwa kura zipo mitaani sio mitandaoni

Nimeshangazwa na kauli ya Waziri mwenye dhamana ya mitandao ya kijamii kuwa kura zipo mitaani sio mitandaoni

Umeshaambiwa ni watanzania asilimia 16% tu. Muwege mnakuwa na akili ya kuelewa basi. Hivi nyie ndo kingwangala alikuwa anawazungumzia kumbe
Nadhani anamaanisha hiyo asilimia 16 ya wanaotumia mitandao baadhi yao wanakaa vijijini na anataka kusema kudhani ni wa mjini tu unakuwa 'umepotea boya' (lugha ya wavuvi wanapopoteza direction wakiwa ziwani au baharini baada ya boya waliloweka kama alama ya kutambua nyavu zao ziko sehemu gani kutoonekana).
 

Kauli zingine zinafikirisha sana.

Maana dunia ya leo kila kitu kipo kidijitali.

Maoni ya watu wananapiga kelele kupitia mitandao ya kijamii. Watawala wanaumia.

Hao hao wanaopiga kelele mitandaoni wanaishi mitaani.

Alafu waziri aliye na digrii anasema hawapigi kura.

Inashangaza.
Wameishiwa hoja wanabaki kuongea vitu vya hovyo! Bure kabisa!
 
Umeshaambiwa ni watanzania asilimia 16% tu. Muwege mnakuwa na akili ya kuelewa basi. Hivi nyie ndo kingwangala alikuwa anawazungumzia kumbe
Asilimia 16? Leo hii karibu kila kaya ina smartphone. Alafu ndio iwe 16%?
 
Na raia walipo mitandaoni ndo waliopo uraiani kwa kauli ya nape humu mitandaoni yeye anaona kuna robbot
Asilimia 16? Leo hii karibu kila kaya ina smartphone. Alafu ndio iwe 16%?
We unamjibu huyu ye Kila kitu awamu hii ni kizuri hata wakimpa mimba mke wake bado atapongeza
 
Nadhani anamaanisha hiyo asilimia 16 ya wanaotumia mitandao baadhi yao wanakaa vijijini na anataka kusema kudhani ni wa mjini tu unakuwa 'umepotea boya' (lugha ya wavuvi wanapopoteza direction wakiwa ziwani au baharini baada ya boya waliloweka kama alama ya kutambua nyavu zao ziko sehemu gani kutoonekana).
Yeye kafanya utafiti na wewe fanya utafiti ili uje na takwimu zako. Research Ina chapter 5 tu.
 

Kauli zingine zinafikirisha sana.

Maana dunia ya leo kila kitu kipo kidijitali.

Maoni ya watu wananapiga kelele kupitia mitandao ya kijamii. Watawala wanaumia.

Hao hao wanaopiga kelele mitandaoni wanaishi mitaani.

Alafu waziri aliye na digrii anasema hawapigi kura.

Inashangaza.
huyu dogo pamoja na makamba, hawakustahili kupewa cheo chochote. sasa ndio naanza kumwelewa bashite kwanini alimfanyia yale kipindi kile. jeuri sana na anapenda kuchukiza.
 
Nilichogundua baada ya kuangalia hii clip ni kwamba body language ya samia haiendani na wimbo anaouimba nape.

Maana yake ni nini..
1. Ameshatambua wanamdanganya sana na wanampaka mafuta kwa mgongo wa chupa.
2. Amegundua wapo kimaslahi zaidi na wanalinda matumbo yao.
3. Anajua huyo nape hamfai ila hakuna namna ya kumtoa..watamuendeshea fitina ambazo hataweza kupambana nazo..maana hilo ni zao la kinana na kikwete.
4. Huyu mama ni muumini wa mitandao toka siku alipotawazwa na anaiamini mitandao kuliko hao watu..kuambiwa apuuze mitandao inamchanganya sana maana anajua mitandao inafika duniani kwa haraka kuliko hao watu wa tandahimba..kuna wakati alipangua watu kwa kusoma mitandaoni tu.
5. Anaona kiza zaidi mbele kwenye safari yake ya kiuongozi kwa kushirikiana na hawa watu ambao mwanzoni alidhani watamfaa. Ni kama mwisho wa siku ama aamue kutogombea au apokee urais wa dhulma kwa maslahi ya kikundi kidogo cha watu fulani.

Kazi ipo..

Sent from my SM-A225F using JamiiForums mobile app
Waziri anaponda mitandao wakati na yeye ni Member wa majukwaa kadhaa!
 
Sasa kwa nini huwa wanazima mtandao??
 
Yeye kafanya utafiti na wewe fanya utafiti ili uje na takwimu zako. Research Ina chapter 5 tu.
1. Hujaelewa nilikuwa namwongelea nani, maana niliyekuwa namjibu siyo huyo ambaye wewe ni msemaji wake.
2. Kwa vile umenipeleka huko ambako sikuwa, ngoja tu niende huko anyhow. Hakuna utafiti wowote ambao umetajwa na msemaji. Katika maelezo yake ametaja tu hizo asilimia 16 za mtandaoni na asilimia 40 diaspora na hakuonyesha hizo asilimia zimetoka wapi (hajataja chanzo cha takwimu zake).
4. Hajaeleza pia amezitapaje - ni kwa bara tu au hata Zanzibar? Ni watumiaji wa mijini tu au hata wa vijijini? Hajaeleza ni kwa mikoa mingapi!
5. Kutaja tu idadi ya watumiaji wa mitandao siyo sifa ya kufanya utafiti.
6. Je, huo utafiti unaoutaja unaitwaje na ulifanyika lini - ni wa mwaka juzi, jana au mwaka huu?
 
1. Hujaelewa nilikuwa namwongelea nani, maana niliyekuwa namjibu siyo huyo ambaye wewe ni msemaji wake.
2. Kwa vile umenipeleka huko ambako sikuwa, ngoja tu niende huko anyhow. Hakuna utafiti wowote ambao umetajwa na msemaji. Katika maelezo yake ametaja tu hizo asilimia 16 za mtandaoni na asilimia 40 diaspora na hakuonyesha hizo asilimia zimetoka wapi (hajataja chanzo cha takwimu zake).
4. Hajaeleza pia amezitapaje - ni kwa bara tu au hata Zanzibar? Ni watumiaji wa mijini tu au hata wa vijijini? Hajaeleza ni kwa mikoa mingapi!
5. Kutaja tu idadi ya watumiaji wa mitandao siyo sifa ya kufanya utafiti.
6. Je, huo utafiti unaoutaja unaitwaje na ulifanyika lini - ni wa mwaka juzi, jana au mwaka huu?
Kumbuka yule ni waziri hivyo anawataamu wa kumpa tamwimu kila anapozitaka
 
Kumbuka yule ni waziri hivyo anawataamu wa kumpa tamwimu kila anapozitaka
Tunaongelea utafiti uliofanyika, hatuongelei waziri wala wataalamu alio nao. By the way, kuna takwimu zimetolewa na NBS (ambao ni authority wa takwimu Tanzania) na wanaonyesha kuongezeka kwa idadi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii. Au NBS haina watalaamu wa takwimu?
 
Back
Top Bottom