Nimeshuhudia mtu akiwanga, hili limenitisha

Nimeshuhudia mtu akiwanga, hili limenitisha

Binadamu yeyote ana nguvu ya Mungu ndani yake mana ameumbwa kwa mfano wa Mungu.Ile nguvu ya Mungu iliyopo ndani yake inazuia ushirikina au uchawi/ulozi /uwanga kumuingia,mpaka yeye mwenyewe kwa kujua ama kutokujua afungue mlango kuruhusu uchawi/ulozi/ushirikina /uwanga huo umuingine.

Hii ni sawa na kusema Binadamu yeyote yule uchawi hauwezi kumdhuru kimpata mpaka yeye mwenyewe afungulie mlango wa kuruhusu kuingiliwa na uchawi kumpata.
Ni kwa namna gani basi binadamu huyu mwenye asili ya pumzi ya uhai kitoka kwa Mungu Roho ya Mungu yenye nguvu kubwa ndani yake pasipo hata yeye mwenyewe kujua nguvu aliyonayo anaweza kufungulia mlango kuruhusu kuingiliwa na uchawi kwa kifanya yafuatayo kwa kujua ama kutokujua....

1)HOFU,WASIWASI/WOGA ..mchawi au mwaga mshirikina mlozi huwa anakawaida ya kufanya vitendo vyake akishirukiana na roho chafu za majini anapokuja kuwanga kwako..anaweza akatoa sauti ya milioa ya KISHINDO kama nyayo za w
miguu ya watu wakitembea juu ya paa/dari ya nyumba/chumba chako,au SAUTI YA PAKA wanalia kama watoto wachanga ,au upepo mkali kimbunga chochote au kusikia watu wanatembea ndani au vyombo vinagongana au sauti za ajabu....LENGO la hivyo vyote ni ili wewe UPATE WASIWASI/HOFU/WOGA /UTETEMEKE....ukishaingia tu hofu woga wasiwasi kutetemeka ...TAYARI UNAKUWA UMESHAFUNGUA MLANGO wa yeye kupitisha ulozi na kukupata...mana utakuwa umeruhusu mwenyewe....BIBLIA IMEANDIKA NENO USIOGOPE ZAIDI YA MARA 366 sawa na siku za mwaka mzima ,ishi kila siku ya mwaka kwa miaka yote BILA KUOGOPA ...USIOGOPE....

2)njia nyingine ya kuruhusu kufungua mlango wa ushirikina kukupata ni kwenda kwa waganga wa jadi ..kuchanja chale,ibada za mizimu,matambiko,dawa za waganga wa kienyeji...kalumanzila..kupiga ramli ,kuoga ,kombe ,hirizi,wasoma nyota,kisomo kitabu cha yasin ,wapunga pepo....n.k
zipo nyingi acha niishie hapa..

HONGERA SANA KWA KUTOKUOGOPA umefanya vizuri sana,siku nyingine toka nje kwa ujasiri chukua jiwe piga hilo paka linalolia hapo kwenye dirisha lako ,kwa jina la Mungu piga bila hofu,kesho huyo paka mtu mchawi ataumwa yeye japo wewe uliona umepiga paka lakini umepiga mtu mwanga ,kesho ataugua na anaweza hata akafa.USIOGOPE.
Endelea kumwamini MUNGU sali kabla ya kulala,ishi maisha ya haki,toba ,jiepushe na dhambi,MUNGU ANATUSAIDIA.
Nmekuelewa vyema kabisa mkuu ahsante kwa ushauri mzuri.
 
Herini ya sikukuu ya Noeli, kwangu naona ilishakuwa mbaya kwa mfululizo wa yanayoendelea na hili lililonifanya niandike hapa muda huu.

Kwanza nianze kwa kusema sina utulivu kabisa usingizi umekata na hauwezi kuja kwahiyo kama ntakosea kwenye kuandika mnivumilie.

Ipo hivi nilikuwa ndotoni ghafla nikashtuka muda ilikuwa saa 04:24 , nilivyoshtuka naona reflections za mwanga wa moto, nikajua labda ni mwanga wa taa za gari lakini moyo ukasita kuliamini hilo kwa kuwa mwanga wa gari huwa ni mkali zaidi,

Nikiwa bado kitandani nashangaa zile reflections ghafla zikaanza kumove na kupotea, nikasogeza kapazia kidogo nione nje kinachoendelea. Nimeona moshi unafoka na nikapigia mstari majibu yangu kuwa ule ni moto.

Moyo ukapiga paa!! Nikazungusha macho upande wa pili wa dirisha nikaangalia kwa kunata bila kupepesa macho kama sekunde 40 na kushuhudia mtu kwa mbali kama kapigwa na butwaa akitazama uelekeo wangu kama vile ameniona (ni kama mita 10-15 kutoka nyumba ilipo) ila sikumtambua ni nani kutokana na giza.

Baada ya kuona vile nikarudishia pazia nimefanya maombi na ninaamini nipo salama ila hili limenishtua kwa kiasi fulani.

Wakuu nifanye nini zaidi?

Kuna madhara yeyote kushuhudia hilo?
Mshana Jr muongozo wako ni muhimu mkuu nna taharuki kwa lililotokea.
Unaishi wapi na maeneo gani? Ninachojua, Dar sehemu za uswazi na hata wakati mwingine sehemu zenye watu wa heshima, hizi ni drill za kawaida sana wakati wa usiku. Mimi niliwahi kuishi uswazi na mambo kama haya wala hayashangazi. Hao ni wahanga wa waganga wa kienyeji wakitekeleza maagizo na hawana madhara yoyote. Ishi bila wasiwasi.
 
Ushauri bei ya tochi zile za mwanga mkali IPO chini sana, tena ni za kucharge. Siku nyingine mmulije usoni na full light 🚨, atapagawa na kuzilahi, Kisha Nenda mpelekee moto.
Ngoja niitafute hiyo tochi
 
Unaishi wapi na maeneo gani? Ninachojua, Dar sehemu za uswazi na hata wakati mwingine sehemu zenye watu wa heshima, hizi ni drill za kawaida sana wakati wa usiku. Mimi niliwahi kuishi uswazi na mambo kama haya wala hayashangazi. Hao ni wahanga wa waganga wa kienyeji wakitekeleza maagizo na hawana madhara yoyote. Ishi bila wasiwasi.
Wahanga wa waganga wa kienyeji si ndio hao hao wachawi? Au kuna tofauti
 
Tukio umeanza kuliona saa 4:24. Huu muda ulimaanisha saa nne usiku au saa kumi usiku/alfajiri?.
Kama ni saa kumi na dakika 24 alfajiri na wewe umeandika na kupost saa kumi na dakika 25, naweza kuamiani sasa ulimwengu wa kiroho upo fasta sana kuliko huu wa mwili
 
Wahanga wa waganga wa kienyeji si ndio hao hao wachawi? Au kuna tofauti
Hao ni mafala tu wanaliwa fedha. Unakuta mtu ameambiwa fanya abc ili utajirike etc. Mimi nilishawahi kuona mpaka dada mrembo kabisa anaoga njia panda uchi wa usiku wa manane. Bibi mmoja niliona anasugulia makalio yake kwenye mti akiwa uchi. Haya yasikutishe hata kidogo.
 
Tukio umeanza kuliona saa 4:24. Huu muda ulimaanisha saa nne usiku au saa kumi usiku/alfajiri?.
Kama ni saa kumi na dakika 24 alfajiri na wewe umeandika na kupost saa kumi na dakika 25, naweza kuamiani sasa ulimwengu wa kiroho upo fasta sana kuliko huu wa mwili
Saa 10 alfajiri, nmekuja kuandika humu saa 11 .
 
Hao ni mafala tu wanaliwa fedha. Unakuta mtu ameambiwa fanya abc ili utajirike etc. Mimi nilishawahi kuona mpaka dada mrembo kabisa anaoga njia panda uchi wa usiku wa manane. Bibi mmoja niliona anasugulia makalio yake kwenye mti akiwa uchi. Haya yasikutishe hata kidogo.
Sawa mkuu siogopi kitu
 
Herini ya sikukuu ya Noeli, kwangu naona ilishakuwa mbaya kwa mfululizo wa yanayoendelea na hili lililonifanya niandike hapa muda huu.

Kwanza nianze kwa kusema sina utulivu kabisa usingizi umekata na hauwezi kuja kwahiyo kama ntakosea kwenye kuandika mnivumilie.

Ipo hivi nilikuwa ndotoni ghafla nikashtuka muda ilikuwa saa 04:24 alfajiri, nilivyoshtuka naona reflections za mwanga wa moto, nikajua labda ni mwanga wa taa za gari lakini moyo ukasita kuliamini hilo kwa kuwa mwanga wa gari huwa ni mkali zaidi,

Nikiwa bado kitandani nashangaa zile reflections ghafla zikaanza kumove na kupotea, nikasogeza kapazia kidogo nione nje kinachoendelea. Nimeona moshi unafoka na nikapigia mstari majibu yangu kuwa ule ni moto.

Moyo ukapiga paa!! Nikazungusha macho upande wa pili wa dirisha nikaangalia kwa kunata bila kupepesa macho kama sekunde 40 na kushuhudia mtu kwa mbali kama kapigwa na butwaa akitazama uelekeo wangu kama vile ameniona (ni kama mita 10-15 kutoka nyumba ilipo) ila sikumtambua ni nani kutokana na giza.

Baada ya kuona vile nikarudishia pazia nimefanya maombi na ninaamini nipo salama ila hili limenishtua kwa kiasi fulani.

Wakuu nifanye nini zaidi?

Kuna madhara yeyote kushuhudia hilo?
Mshana Jr muongozo wako ni muhimu mkuu nna taharuki kwa lililotokea.
Potezea hiyo mambo isikufanye mtumwa.
 
Herini ya sikukuu ya Noeli, kwangu naona ilishakuwa mbaya kwa mfululizo wa yanayoendelea na hili lililonifanya niandike hapa muda huu.

Kwanza nianze kwa kusema sina utulivu kabisa usingizi umekata na hauwezi kuja kwahiyo kama ntakosea kwenye kuandika mnivumilie.

Ipo hivi nilikuwa ndotoni ghafla nikashtuka muda ilikuwa saa 04:24 alfajiri, nilivyoshtuka naona reflections za mwanga wa moto, nikajua labda ni mwanga wa taa za gari lakini moyo ukasita kuliamini hilo kwa kuwa mwanga wa gari huwa ni mkali zaidi,

Nikiwa bado kitandani nashangaa zile reflections ghafla zikaanza kumove na kupotea, nikasogeza kapazia kidogo nione nje kinachoendelea. Nimeona moshi unafoka na nikapigia mstari majibu yangu kuwa ule ni moto.

Moyo ukapiga paa!! Nikazungusha macho upande wa pili wa dirisha nikaangalia kwa kunata bila kupepesa macho kama sekunde 40 na kushuhudia mtu kwa mbali kama kapigwa na butwaa akitazama uelekeo wangu kama vile ameniona (ni kama mita 10-15 kutoka nyumba ilipo) ila sikumtambua ni nani kutokana na giza.

Baada ya kuona vile nikarudishia pazia nimefanya maombi na ninaamini nipo salama ila hili limenishtua kwa kiasi fulani.

Wakuu nifanye nini zaidi?

Kuna madhara yeyote kushuhudia hilo?
Mshana Jr muongozo wako ni muhimu mkuu nna taharuki kwa lililotokea.


Mchawi akamatwa live na kamera ya CCTV.
 
Back
Top Bottom