Nimesikitishwa, huzunishwa na kufadhaishwa na uongo wa Kamati ya PAC! Escrow sio fedha za umma!

Nimesikitishwa, huzunishwa na kufadhaishwa na uongo wa Kamati ya PAC! Escrow sio fedha za umma!

Na sio hao tu, mshauri mkuu wa Rais kisheria (AG)amehusika sana.

Mtendaji mkuu katika wizara (katibu mkuu)ambaye ni mteule wa Rais ameshiriki.
Masaidizi mkuu wa Rais katika wizara anayeingia baraza la mawaziri(waziri) ameshiriki
Waziri wa fedha ameidhinisha malipo ya 'pesa binafsi''

CAG ameshirki kuchunguza pesa za 'watu binafsi''
Mkurugenzi PCCB ameshiriki uchunguzi wa pesa' binafsi''

Waziri mkuu ameelekeza uchunguzi ufanywe kwa ''pesa binafsi''

Mwanasheria mkuu alimkosa Kafulila kwa ngumi akitetea 'pesa binafsi''

Wote hao wanashiriki vipi kwa pesa za watu binafsi?
Mkuu Nguruvi 3,

Watu humu na wananchi kwa jumla, wameaminishwa kuwa fedha za escrow ni fedha za umma tena zimeibwa kama kwenye EPA, hivyo ni fedha chafu hivyo zimepitishiwa Stanbic na Mkombozi ili zitakatishwe!, hivyo sasa wana hasira sana baada ya kutajiwa hiyo mijizi yao, wanasubiri with great expectations mijizi yao isulubiwe, leo nilikuwa nasiliza interactive program moja ya live, kuna watu wanasema hawa jamaa wanyongwe without trio, ule ushahidi wa majina kwenye account unatosha!, jinsi ninavyoshambuliwa humu ni ushahidi wa jinsi watu walivyo na hasira, zilizo pelekea hata thinking yao kuwa ipaired!, watu wanasubiri amri tuu ya piga ua!, ila kwangu mimi inapotokea hawa ma great great thinkers wetu humu kama Nguruvi 3 na Mchambuzi, they cease to think, then kiukweli Tanzania sasa tunaeleke kusiko!, mfano leo wakati wa majumuisho, serikali ikizipangua hoja zote moja baada ya nyingine na ikikutikana escrow sio fedha za umma!, kisha mbunge mmoja kama Kesi akalianzisha kuelekea usawa wa spika, hata askari wote wa bunge hawataweza kuzuia

Where is Nguruvi3 and Mchambuzi the thinkers?!.

Pasco
 
Mkuu Nguruvi 3,

Watu humu na wananchi kwa jumla, wameaminishwa kuwa fedha za escrow ni fedha za umma tena zimeibwa kama kwenye EPA, hivyo ni fedha chafu hivyo zimepitishiwa Stanbic na Mkombozi ili zitakatishwe!, hivyo sasa wana hasira sana baada ya kutajiwa hiyo mijizi yao, wanasubiri with great expectations mijizi yao isulubiwe, leo nilikuwa nasiliza interactive program moja ya live, kuna watu wanasema hawa jamaa wanyongwe without trio, ule ushahidi wa majina kwenye account unatosha!, jinsi ninavyoshambuliwa humu ni ushahidi wa jinsi watu walivyo na hasira, zilizo pelekea hata thinking yao kuwa ipaired!, watu wanasubiri amri tuu ya piga ua!, ila kwangu mimi inapotokea hawa ma great great thinkers wetu humu kama Nguruvi 3 na Mchambuzi, they cease to think, then kiukweli Tanzania sasa tunaeleke kusiko!, mfano leo wakati wa majumuisho, serikali ikizipangua hoja zote moja baada ya nyingine na ikikutikana escrow sio fedha za umma!, kisha mbunge mmoja kama Kesi akalianzisha kuelekea usawa wa spika, hata askari wote wa bunge hawataweza kuzuia

Where is Nguruvi3 and Mchambuzi the thinkers?!.

Pasco


Too low!!!!
 
...Pasco kwanini unatetea hizo siyo fedha zetu, why and why? Pasco kama kweli unazungumza kizalendo embu have a mercy on us aisee, ili uthibitishe ur not one of them.
Mkuu Chagga King, kwa jinsi ninavyosoma moods za watu humu, just count me, one of them, I belong to the group la wafia ukweli, kuwa ukisema ukweli utauwawa, nitasimama na kweli!, kitu kizuri ni kuwa mwisho wa siku ukweli ndio utakaosimama, we have stop living a lie!, ndio maana siogopi kugombana na watu katika jambo ambalo mwisho wa siku tutakuja kupatana!.

Pasco
 
kuna mdau mmoja anaitwa Nkwesa Makambo, kazungumza vizuri sana, ni kama alikuwa na mawazo kama yangu, hata ningekuwa bungeni ningeuliza swali hili, wanaposema zile fedha hazikuwa za umma walimaanisha nini, maana zile fedha zilikuwa zina "hang" kwenye account ya escrow zilikuwa bado hazijalipwa kwa mtu yoyote, si IPTL wala Tanesco alikuwa anazimiliki kwa wakati huo, lakini TANESCO alikuwa ananafasi kubwa ya kuwa na right kwenye hizo fedha maana IPTL alikuwa bado hajatimiza obligation ya kwenye contract yao hivyo hakuwa entitled na hizo fedha mpaka pale atakapo fulfil obligation.

mfano IPTL ange breach contract asingeweza kuzidai, so hizo fedha zilikuwa ni subject to..., na kama zilikuwa ni za IPTL kwanini hazikulipwa kwenda kupitia kwenye account ya IPTL moja kwa mmoja?. naomba usiseme kuwa walikuwa hawaaminiani maana tayari walikwisha kuwa na dispute, kimsingi zile fedha ni mali ya umma, na hata kama zingekuwa ni za IPTL kwanini zigawiwe kiholela hivyo?, kama siyo kuwa kulikuwa na mchezo mchafu?,

kingine ni kuwa, issue ya IPTL siyo kuhusu fedha za kwenye acc ya escrow, maana kuna kukiukwa kwa kanuni za mikataba tokea 1994 kuwa hiyo kampuni haikuwa na sifa ya kushinda zabuni ya kusambaza umeme Tz, hapo napo kuna mchezo mchafu ulifanyika na bado watu wote waliohusika walitakiwa wawajibishwe, sijui kwanini hili halikutiliwa maanani na PAC, Kwahiyo mkuu Pasco jaribu kuliangalia hili jambo kwa jicho la tatu, usiwe biased kiasi hicho, kama una hoja thabiti kuwa zile fedha siyo za umma jaribu kuiwasilisha hapa.

mtazamo wangu kwa sasa, sisi wananchi tuchukue hatua, hizo drama za bungeni tuachane nazo, sisi wananchi ndo tuwe waamuzi wa mwisho, nadhani muafaka tutaupata na siyo kuwategemea hawa wanasiasa ambao wanakila aina ya ila kuweza kuchakachua.

Chagga King from Umbwe Klm.

Mkuu kama vile ulikuwa nami kichwani aisee....sina la kuongeza zaidi Ya kusema Ubarikiwe sana..👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏
 
Mkuu kama vile ulikuwa nami kichwani aisee....sina la kuongeza zaidi Ya kusema Ubarikiwe sana..👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏




Mkuu hoja za PAC ni za wabunge wote kwa maana kamati ni ya bunge na inafanya kazi kwamujibu Wa kanuni...

kamati imechambua hoja za CAG... kamishna mkuu Wa TRA na Mkurugenzi Wa PCCB.....

Bahati mbaya Sana Muhongo hajathubutu hata chembe kugusa au kuongelea maoni ya watu hao watatu ambao ni agents wa serikali....

Ni mtu dumb tu anaweza shabikia kinachofanyika bungeni na baadhi ya wabunge kwani wabunge walipaswa kuhoji serikali na si mashambulizi kwa PAC maana hoja ni yao....

kwa Mara ya kwanza wabunge kuifurumua kamati badala ya serikali but wanaonunua watu cheap kupindisha taratibu wataigharimu nchi hii.....

Wengi kwa mazoea tu na upogo Wa akili waliishambulia PAC Kama ukawa ilihali kuna wanaCCM 19 hivi kesho hao wajumbe watakaa pamoja wakaelewana??

Tanzania inachagizwa Sana na watu Wa low profiles Kama akina Lusinde wanaopewa 30 minutes kuongea upuuzi ambao mawaziri wameupigia makofi ilhali watoto wao wakifanya Kama ya Lusinde naamini watawapiga......

Watu mazuzu...
mataahira...mazezeta....wapenda pombe...ngono..

majungu.....ubwabwa na kila aina ya ushenzi wanatufanya tugharimike Sana....

50 years after independence hatujafikia uchumi Wa kati halafu watunga Sera na wafanya maamuzi wetu ndo style ya kina Lusinde...

TOO LOW!!!!!!!!!!!!
 
Mkuu Mchambuzi, hakuna mahali popote Rais wa JMT, ametakiwa kuidhinisha malipo, bali hiyo ni initiative ya Gavana wa BOT, kujiridhisha jee awareness ya Mkuu wa Nchi kuhusu jambo hili!.

Pasco

Ukiruhusu tumbo likutawale IPO siku mavi yanayokaa tumboni yatakuendesha.
 
sasa wewe ile riport niya cag au ya pac watu wazima naelimu zenu mbona mnachanganya pac walikuwa wanalifaa tuu sio kutunga mengine tofauti na riport ya takukuru na cag msipotoshe ukweli
 
kuna watu humu ndani nilikuwa nawaheshimu sana kwa michango yao iliyojaa hekima na busara kumbe si lolote..wewe Pasco uoni aibu kutetea ujinga inamaana tra,cag,na takukuru ni waongo wote hawa waseme uongo acha kuwa msaliti wewe facts zote za tanesco,Tra,Pccb na Cag ni za uongo...???umejishusha sana tena sana...!
 
Pasco, unavyosema hivyo pia uwe mkweli kusema IPTL wamekuwa wanaovachaji unit price ya Umeme wanaouza kwa Tanesco isivyo kihalali ikimaanisha ni wizi. Kwa maana kwamba watumiaji wa umeme tumekuwa tukiibiwa na IPTL bila kujijua.

Hivyo basi IPTL na washirika wao walistahili kuwa wameshtakiwa kwa wizi kitambo kirefu kabisa.

Watanzania tuwe na utu!
 
kaka umemaliza kabisa!
Hayo ndiyo maswali niliyomuuliza hapo juu post 3, pasco nini maana ya fedha za umma, ndio maana nimemuuliza tanesco wanatengeneza pesa???

nchii hii tutaendelea kuwa maskini mpaka siku ya mwisho;

PASCO UMENISIKITISHA SANAAAA..
Mkuu, humjui Pasco ndo mana unasikitika. Sisi wengine hatupi shida kabisa huyo...Tunaelekea kwenye Chistmass kile kipindi chetu cha 'Christmass na PPR' karibu kitakuwa hewani
 
Last edited by a moderator:
Pasco kinacho bishaniwa hapa sio huduma ya umeme imepatikana au haikupatikana hii sio issue.
Kinachobishaniwa ni fedha iliyokuwa inaingizwa katika akaunti ya escrow kuwa ni ya serikali au ya kampuni binafsi.Hiyo ndiyo hoja mjadala.
Kwa vyo vyote vile capacity charges ni lazima na componet ya vat.
Swali ambalo sijaona mtu ye yote akiuliza ambalo ni la msingi,sana,Je! Wakati IPTL wanawapelekea tanesco bills za capacity charge zilikuwa na vat?Kama zilikuwa na vat,hiyo vat ni mali ya nani.
Mimi binafsi kuwa iptl ilikuwa ni tatizo tokea imeanza,na kwa wale wenye kumbukumbu vizuri benki ya dunia iliwahi kutuonya juu ya mitambo ya iptl kama itaipelekea taifa kupata hasara.
 
Mim Mtanzania wa kAwaida sana ntabak najiuliz kwanin watu wagawane hela ovyoovyo,walikuwa na hisa huko?! mbona mnataka kutyfanya ss manyanga'u.

Kama ndani ya chaa chenu kuiba hela ni kawida nakatumia wingi wenu kurifunika hili basi poa kwetu sisi huu ni mtaji tena mtaji mkubwa ulioletwa katika mda mwafaka.

Nilitegeme itikadi za vyama zitawekwa chini ili masrh ya nchi yatangulie but uhmmm hata siwaelewi nyie wenzangu....
Okay poa funiken kumbe taktana kitaaaaa..
 
Pasco, kwahofu kuwa huenda tumekuwa impaired ndio maana tunauliza utusaidie.
Katika hojazako hapo juu , hujajibu hoja zetu ambazo ni hizi

1.Kama sipesa za umma, ile kodi iliyopaswa kuchuliwa si ya umma?

2. Kamanipesa binafsi
a) Mwanasheria mkuu wa serikali anaingije hapo

b)Katibumkuu anawakutanisha vipi wafanyabiashar katika ofisi ya umma?

c)Katibu warais anaidhinisha vipi malipo ya wafanyabiashara?

d)Wazirimkuu anaagizaje uchunguzi wa account za wafanyabiashara?

e)CAGanakwendaje kuchunguza account binafsi?

f)Wazirianaingije katika biashara zisizo za umma?

g) Viongoziwa serikali wanapataje mgao kwa kuzingatia maadili ya kazi zao?

h)Taarifa yaCAG na PCCB ni za uzushi na uongo?

i) Nanianaweza kutupa ukweli kuhusu suala hili?

j)Kwaniniserikali isyohusika ihahe kutaka kuzuia mjadala unaohusu wafanyabiashara?

k)Mwanasheriamkuu anatoaje maamrisho ya kulipwa wafanyabiashara binafsi?

Baada yakutupatia majibu, tuseme kuwa hoja ya hukumu ya wananchi inaepukika vipi ikiwaleo

  1. Hatujui nani alichukua pesa za radar? Je haikuwabiashara halali kama Escrow?
  2. Meremeta, EPA, Tangold zimeishia wapi?
Wapiunachora mstari kati ya utulivu na Amani? Na kinachofuata baada ya hapo ni nini

China wamefanikiwakupunguza rushwa kwa kutandika watu madini ya Zambia.
Hata sisitumeiga mambo mengi ya taifa ya magharibi kama demokrasia,utawala wa sharia n.k.

Kuna tatizogani tukijaribu mwendo wa China ili kuondoa uozo huu unaosambaa?

Mbonawachina wametujenga reli, kiwanja cha michezo n.k. Tatizo lipo wapi tukijaribuutaratibu wao unaowafanya wawe ‘uchumi mkubwa wa pili duniani''
Kwanini tusijaribu madini ya Zambia yanayopatikanakwa urahisi tu nchini.
 
Pasco, Umeanza toka juzi unahangaika, uzuri huko kwote unakopita watu tulishapita, anyway you can not be like Dr. Stockman, wewe una real njaa....we know about African Politics, A pure African journalist like you, you are vulnerable to money inducement, na hiyo ndio inakufanya unahangaika na keyboard hapa..

When we depend to the journalists to make a Whistle blowing, then you find out that Only the citizens are agitating,...Very Sad
 
Last edited by a moderator:
Siku hizi fedha za mtu binafsi zinakaguliwa na Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za serikali?!!!! Mwanasheria mkuu alipata wapi madarka ya kuamuru malipo yafanyike. Hukumu ya overcharging ya capacity charge in favour of Tanzania tumeombwa tu recalculate tujue ni fedha kiasi gani tunaweza kurudishiwa tangu mwaka 2004 tz wameingia mitini kwa sababu watu walikuwa wmeshapiga tayari. Mtumishi wa umma unagawawi mabil ya fedha tena ungali madarakani watu badala ya kuhojiwa na kuwajibishwa li chama hili lillilo oza linasema siye hayatuhusu labda alipewa mchango wa harusi... What a shame....! Jana yamepigwa na ushahidi wa kutosha yanatoa mimacho tuuuu ooooh lete hiyo barua tuione kama ni halali Oooooh What a shame!!!!! Shame on you!!!!!!!!!!
 
Pasco, unaomba tuelewashane wakati tayari umeshatoa hitimisho!! Tangu mwanzo hata kabla ya PAC kuwasilisha kamati msimamo wa Kafulila umekuwa kwamba ndani ya akaunti ya ESCROW kuna fedha ya TANESCO (umma). Hakuna aliyewahi kusema kwamba pesa yote ni ya umma. Kumbuka kwamba hela yote imetokana na shauri mahakamani. Badala ya kuilipa IPTL pesa ilikuwa inakwenda kwenye hii akaunti hadi shauri lingeamuliwa ili kujua kiasi halisi ambacho IPTL walistahili. Mahakama ikaamua kwamba ni kweli kwamba TANESCO walikuwa wanalipa pesa nyingi zaidi kuliko uhalisia. Sisi tukapewa nafasi ya kukokotoa mahesabu ili tuchukue cha kwetu na kinachobaki kiende IPTL. Tumeshindwa au tusema tumekaa kufanya hivyo kwa sababu hiyo pesa tulishaipiga, haipo. Ndio hizo akina Ruge wamezigawa kama njugu. Sasa utasemaje kwamba hakuna pesa yetu pale?

Hata kitendo tu cha akina Ruge kugawa hela ovyo kinakwambia kwamba ile haikuwa pesa yao. Katika hali ya kawaida kama ile ingekuwa pesa yao walioipata kihalali ingewezekanaje waigawe ovyo namna hiyo? Matarajiri wa Tanzania ni Rostam, Bakhresa na Mengi, mbona hatujasikia wakigawana fedha bararani namni ile? Na kwa nini waliogawiwa wote ni wanasiasa, viongozi na watu wenye mamlaka fulani? Kwa nini Ruge hakwenda kugawa hizi fedha kwa wanafunzi wetu waliokosa mikopo kama kweli ana roho nzuri kiasi hicho?

Haya, wewe unaona ni sawa watu kugawana pesa kama maembe kama walivyofanya? Nchi za wenzetu hata kuingia na dola 10,0000 wanakuzuia lazima utoe maelezo ya kutosha na vielelezo kibao. Hapa kwetu watu wanagawana pesa kwenye rambo wewe unaona ni sawa hiyo? Pasco please!!
 
Back
Top Bottom