Nimestushwa na Kauli ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Je ni kufilisika ki Maono kwa CCM?

Nimestushwa na Kauli ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Je ni kufilisika ki Maono kwa CCM?

Watu hawaoni hoja yako, wamekariri VETA.! Sasa kama Veta i mworabaini kuna sababu gani ya kuwa na Vyuo vya Kati na Vyuo vikuu? Yaani Engineer aende VETA kufundishwa na Fundi Mchundo!

Kazi ya Engineer si kuchomea (welding) au kufungua bolts and nuts, kazi ya Engineer ni nyingi ikiwemo ku design na kusimamia. Halafu hawataki kujibu hoja ya kwamba kwanini graduate wa SUA asipewe mkopo wa Trekta eti aende Veta! kuna ujuzi gani wa Kilimo VETA ambao SUA haupo!

Sina uhakika kama Waziri Mkuu alishauriwa vema kabla hajasema. VETA ilianzishwa kwasababu ya kupata Watalaam wa kada ya kati na ambao hawakuweza kupata nafasi za kuendelea na masomo.

Wahitimu wa ''University' wakifurika VETA, huyu wa Form 4 au 6 hatapata nafasi tena kwasababu wa Chuo kikuu atakuwa bora huko VETA! Je hapo watakuwa wame solve tatizo la ajira?




JokaKuu
Engineer huyo mwenye degree hata kushika drill au grinder hawezi kuitumia

Ova
 
Nimekuuliza specific, Daktari wa Meno (DDS) au Medicine (MD) au Nurse wanakwenda veta kupata ujuzi gani?

Mtu aliyemaliza Kilimo SUA, au Mass communication anakwenda veta kupata ujuzi gani?
Daktari au Nurse wajitolee ili wapate ujuzi. Siwezi kuwa nna hospital niajiri tabibu hawezi kushona hata kidonda.
Wa SUA akalime kuna mashamba ya kutosha nchi hii.
 
Wa sua wakalime wawezeshwe na serikali
Daktari atabaki kuwa daktari

Ova
Ndiyo hoja ya mleta mada kwamba, kuwepo na mazingira ya watu kujiajiri. Mleta mada akasema mikopo nafuu kwa mfano, Madaktari ili waweze kuwa na '' Vi Aga Khan'' au ''Hindu Mandal.'' Hivi baadaye vitaajiri wanaokuja! kwanini tunadhani hatuwezi ni hadi watu kutoka nje?

Sasa mtu kasomea ''Journalism'' halafu unampeleka VETA ni ili iweje! Mtu kasomea Vertenary unampeleka VETA ili iweje! Mtu kasomea Civil Engineering unampeleka VETA iweje! Mtu kasomea material managament unamepeleka VETA ili nini! Mhitimu wa Bcom anakwenda kupata ujuzi gani VETA

Kauli ya PM haikuwa na mantiki kabisa. Ni kama serikali imeishiwa mbinu! ni kauli inayo disturb sana
 
Wanataka nesi nae aende kujifunza Rejeta inavofanya kazi, kumwaga injini oil
Aisee
Kikubwa vijana wawe na skills
Ukubali ukatae,waliyopitia veta
Wanapeta mitaani kuliko hao wenye degree...
Wenye degree wakimaliza tegemeo lao kubwa ni ajira serikali na sekta binafsi

Ova
 
Daktari au Nurse wajitolee ili wapate ujuzi. Siwezi kuwa nna hospital niajiri tabibu hawezi kushona hata kidonda.
Wa SUA akalime kuna mashamba ya kutosha nchi hii.
Hoja yako ni kwamba waende VETA. Sasa ujuzi gani wataupata huko VETA?

Kumbuka, hoja ni kauli ya Waziri Mkuu kwamba waende VETA na wewe ukasema yupo sahihi.
Ninakuuliza, Daktari na Nurse wanakwenda VETA kupata ujuzi gani?
 
Kujenga barabara nazo we need Mchina...Karine ya 21 . what a shame ?hivyo vyuo vinakazi gani ?
Kwanza Majaliwa K Majaliwa ni K aache ngeseu kabisa kafazama yeye na Chama Cha Maboga wameshindwa kubuni namna ya kuwasaidia vijana wasio na ajira halafu anakuja na ngeseu wa aina gani kemamaku zake ngesem kabisa
 
kwanza kuzingati na kutekeleza kwa vitendo mawaidha aliyoyatoa waziri mkuu dhidi ya graduates wasaka ajira mtaani kupata ujuzi veta na kujiari,

Lakini pili,
graduates waje seketa ya kilimo na ufugaji biashara ambayo ina ajira za uhakika na kutosheleza waTanzania wote.

Kuhusu utajiri kwenye sekta hizi, ni wa wazi na wa uhakika zaidi tena bila uchawi wala ushirikiana.

Hakuna haja kwa vijana kupoteza muda kwa kuzurura na kuchakaza viatu mijini na bahasha za kaki hali ya kua ajira nyingi za uhakika zipo shambani 🐒
Sawa Senior , ila mimi naamini somedays you will understand…… for now endelea kula matunda ya kutumikia wananchi
 
Ndiyo hoja ya mleta mada kwamba, kuwepo na mazingira ya watu kujiajiri. Mleta mada akasema mikopo nafuu kwa mfano, Madaktari ili waweze kuwa na '' Vi Aga Khan'' au ''Hindu Mandal.'' Hivi baadaye vitaajiri wanaokuja! kwanini tunadhani hatuwezi ni hadi watu kutoka nje?

Sasa mtu kasomea ''Journalism'' halafu unampeleka VETA ni ili iweje! Mtu kasomea Vertenary unampeleka VETA ili iweje! Mtu kasomea Civil Engineering unampeleka VETA iweje! Mtu kasomea material managament unamepeleka VETA ili nini! Mhitimu wa Bcom anakwenda kupata ujuzi gani VETA

Kauli ya PM haikuwa na mantiki kabisa. Ni kama serikali imeishiwa mbinu! ni kauli inayo disturb sana
Hao wanaosoma civil engineering
Kwenye hivyo vyuooo,kuna wengine hata kushika drill au grinder machine hawawezi

Ila theoretical wako vzr

Ova
 
Ujuzi utaomuwezesha kupata ajira. Nikihitaji graphic designer natafuta form four leaver mwenye uwezo wa kutumia adobe photoshop/Illustrator, sihitaji mavyeti yako ya udsm.
🤣 Nesi Akomee na graphic design au sio . MUFILISI
 
Hoja yako ni kwamba waende VETA. Sasa ujuzi gani wataupata huko VETA?

Kumbuka, hoja ni kauli ya Waziri Mkuu kwamba waende VETA na wewe ukasema yupo sahihi.
Ninakuuliza, Daktari na Nurse wanakwenda VETA kupata ujuzi gani?
Huyo mngese asikuumize kichwa
 
Hao wanaosoma civil engineering
Kwenye hivyo vyuooo,kuna wengine hata kushika drill au grinder machine hawawezi

Ila theoretical wako vzr

Ova
Sawa kazi yao siyo hiyo! wao ni ku design na kusimamia. Kushika grinder ni wale wa Technical college na kwa bahati mbaya VETA!

Ni lazima muelewe maana ya Degree na malengo yake kitaaluma !
 
Niliajiriwa kwa sababu nilikuwa nna ujuzi. Mimi niliajiriwa tangu nipo chuoni wakati huo kuna watu mtaani graduates waliachwa.
Majaliwa ana point kwa sababu hupewi ajira kwa kuwa una vyeti nenda veta kapate ujuzi.
Mpuuzi mmoja wewe
 
Sawa kazi yao siyo hiyo! wao ni ku design na kusimamia. Kushika grinder ni wale wa Technical college na kwa bahati mbaya VETA!

Ni lazima muelewe maana ya Degree na malengo yake kitaaluma !
😄 aise ....
Hizo technical college miaka ya nyuma ndizo zilitoa waandisi mahiri kuanzia wa ujenzi,magari,ndege,umeme
Kwa sahv hamna kitu
Tukubali tu elimu yetu imechezewa mahali
Na kama serikali inatakiwa sasa kutengenezea watu fursa mazingira bora mfano kwenye kilimo nk

Ova
 
😄 aise ....
Hizo technical college miaka ya nyuma ndizo zilitoa waandisi mahiri kuanzia wa ujenzi,magari,ndege,umeme
Kwa sahv hamna kitu
Tukubali tu elimu yetu imechezewa mahali
Na kama serikali inatakiwa sasa kutengenezea watu fursa mazingira bora mfano kwenye kilimo nk

Ova
Toa Ushauri , tufunge vyuo?
 
Back
Top Bottom