Nimeuziwa gari la urithi bila kuelewa, najinasuaje huu msala

Nimeuziwa gari la urithi bila kuelewa, najinasuaje huu msala

huyo mama kipindi chote alikuwa wapi ?kuna dalili ya watu kula deal hapo, iweje mtu auze gari halafu kadi OG awe bado anayo au hawakumaliza deni na kama hawakumaliza deni kadi ilibidi iwe kwa Wakili, aliipateje ?....Fanya hivi, likongoroe gari lote uza spear kisha kachukue lost report ukipenda vinginevyo wakija waambie sina gari na sijawahi kununua hilo gari sababu kuna dalili za kuanza usumbufu usiokuwa na msingi utakaokupotezea muda na gharama zako...bora hasara kidogo.
Niende moja kwa moja kwenye mada, mwezi wa 6, 2022 kuna jamaa aliniuzia gari Mkoa wa Mwanza (Crown 2010). Tukaandikishiana vizuri kabisa nikatoa hela nikapewa kadi, nikakamilisha taratibu kama bima nk sikuweza badilisha umiliki sababu ya kukosa nakala halisi za jina la mwenye kadi.

Basi katika kuvimba nalo mjini nashangaa juzi napigiwa simu na bi maza anayedai yeye ndo msimamizi wa mirathi nimeuziwa gari lake bila ridhaa yake na anakusaidia kunipeleka polisi kama mwizi wa gari.

Yule mama ana mkataba halisi wa mauziano ya gari yeye akiwa kama shahidi wa mume wake tena muuzaji akiwa ni yule ambaye jina lake lipo kwenye kadi.

Wakubwa nafanyaje kwenye hili? Nimevurugwa kabisa yule dogo aliyeniuzia simpati tena, maza mtu kasema ananipa mwezi mmoja niwe nimeshaamua.
 
huyo mama kipindi chote alikuwa wapi ? likongoroe lote uza spear kisha kachukue lost report ukipenda vinginevyo wakija waambie sina gari na sijawahi kununua hilo gari...bora hasara kidogo.
Kama mkataba wa mauziano upo, na mtoto wa mmiliki alisaini; hapo anaweza kujinasua, na kesi kuamia ndani ya familia. Tofauti na hivyo, mnunuzi ataonekana kaiba gari pamoja na kadi.

Wengi huwa tunanunua magari na kujisahau kubadilishi majina ya wamiliki wa mwanzo, hii huwa ni hatari.​
 
kama kadi inasoma jina la mtu anayeniuzia hapo mkataba wa yeye alinunua kwa nani hauna haja. Cha kujiridhisha je yeye ndiye aliyeandikwa humo kwa hiyo nitaomba vitambulisho vyake kikiwemo cha NIDA, kazi ili kulinganisha majina yaliyomo kwenye kadi ndiyo ya kwake au Lah...Na baada ya hapo mimi nitaendelea kutembea na Kadi na mkataba hadi nitakapobadilisha iliki huo mkataba unakuwa umefika mwisho wake wa matumizi labda itokee sintofahamu huko mbeleni ila na mimi nikitaka kuuza nitampa kadi tu na nitaandikishana naye ule mkataba wa mimi nilinunua wapi hautamuhusu na hautokuwa na tija kikubwa wakati huo majina yangu ndiyo yasome kwenye kadi.
Kama mkataba wa mauziano upo, na mtoto wa mmiliki alisaini; hapo anaweza kujinasua, na kesi kuamia ndani ya familia. Tofauti na hivyo, mnunuzi ataonekana kaiba gari pamoja na kadi.

Wengi huwa tunanunua magari na kujisahau kubadilishi majina ya wamiliki wa mwanzo, hii huwa ni hatari.​
 
kama kadi inasoma jina la mtu anayeniuzia hapo mkataba wa yeye alinunua kwa nani hauna haja. Cha kujiridhisha je yeye ndiye aliyeandikwa humo kwa hiyo nitaomba vitambulisho vyake kikiwemo cha NIDA, kazi ili kulinganisha majina yaliyomo kwenye kadi ndiyo ya kwake au Lah...Na baada ya hapo mimi nitaendelea kutembea na Kadi na mkataba hadi nitakapobadilisha iliki huo mkataba unakuwa umefika mwisho wake wa matumizi labda itokee sintofahamu huko mbeleni ila na mimi nikitaka kuuza nitampa kadi tu na nitaandikishana naye ule mkataba wa mimi nilinunua wapi hautamuhusu na hautokuwa na tija kikubwa wakati huo majina yangu ndiyo yasome kwenye kadi.
Tatizo linaonekana, jina la muuzaji (mtoto) halipo kwenye kadi; hapo mtoa mada inabidi atafute njia ya kujinasua, pia asipate hasara.
 
Binafsi ningebadilishana mtoto na gari. Ningemwambia wala usihofu mama, gari nakuletea na kuhusu mwanao ule msemo wa asiyefunzwa na mama yake utafanya kazi

Baada ya hapo jioni yake yeye ana gari, mm nina kibali cha kukamata na mazingira ya kupokelewa nimeyatengeneza.
 
Tatizo linaonekana, jina la muuzaji (mtoto) halipo kwenye kadi; hapo mtoa mada inabidi atafute njia ya kujinasua, pia asipate hasara.
Itakula kwake..mtu anakujaje kukuuzia kitu ambacho umiliki wake ni wa mtu mwingine, kupenda vitonga sometime kuna-cost.
 
tafuta wakili mzuri akushauri na akupe angle za kusimamia , uzuri kadi original unayo na mkataba wa mauziona unao. hiyo ni kesi yao huko nyumbani
 
Huyo mama na mwanae ni washenzi na matapeli.
Unamalizana nao kimjini tu mamaye zao. Hakuna kumuachia Mungu wala kuiachia jamhuri. Ni ugaidi vum vum
 
Hapa tafuta mteja muuzie hata kwa bei ya hasara. Maza akikutafuta kuhusu gari mruke futi mia. Kuwa hamjawahi kufanya biashara ya kuuzina gari na yeye.
 
Sikuona umuhimu maana mkataba wa maudhiano upo tena tulipitia ofisi ya mwenyekti wa mtaani kwao dogo, sikuwa na shaka maana ni mkazi wa huo mtaa na gari amekua akilitumia yeye tangu 2017 mzee wao alipofariki, baada ya kufariki nyumba na gari vya Mwanza alibaki navyo dogo mama yao akaenda Kuishi ARUSHA (Haya ni maelezo ya ufupi kutoka kwa majiriani wa mtaa baada ya kupeleleza kidogo)
Unanuaje Mali kama hiyo bila kupata taarifa zote kulihusu gari? Unanuaje Mali kama hiyo bila kumtumia wakili au mahakamani?
 
Sikuona umuhimu maana mkataba wa maudhiano upo tena tulipitia ofisi ya mwenyekti wa mtaani kwao dogo, sikuwa na shaka maana ni mkazi wa huo mtaa na gari amekua akilitumia yeye tangu 2017 mzee wao alipofariki, baada ya kufariki nyumba na gari vya Mwanza alibaki navyo dogo mama yao akaenda Kuishi ARUSHA (Haya ni maelezo ya ufupi kutoka kwa majiriani wa mtaa baada ya kupeleleza kidogo)

Kesi rahisi hiyo kaka, i hopemkataba una picha na maelezo ya jamaa aliyekuuzia na mashahidi wote,kadi unayo pia.
Kipindi cha mauziano aliyekuuzia alitoa nakala ya kitambulisho chochote?

Sasa hapo inabidi wewe uwahi, kule serikali ya mtaa/ kata toa taarifa , pita polisi,tafuta mwanasheria settle down nae.

Hapo unapindua meza na inakua kesi ya utapeli wa Mama na mwanae.
 
Chakukushauri tufuta mwanasheria mbobevu wa hizi kesi mweleze kila kitu kinagaubaga, A-Z atajua namna ya kukusaidia hii kesi nina uhakika ushindi upo kwako.
 
Kalikopee mkopo kwa wale jamaa wa mwezi mmoja, weka bondi ndinga upoze machungu.
Mkuu Wakopeshaji wapo makini sana, labda apate waliozubaa.

Kama Kadi haina jina lako bai awe anakufahamu sana au upelekwe na Mtu wanayefahamiana nae nje ndani.
 
Kiufupi hapa tayari kuna mgogoro, kama Mama anamuacha Mwanaye aliyekuuzia anakutafuta wewe moja kwa moja hiyo tayari ni familia ya "mchongo", hivyo kaa mkao tu.

Ingekuwa ni zile familia zenye hofu ya Mungu Mama angejiridhisha tu kuwa Mwanaye kauza Gari basi angeachana na wewe wakapambana wao wenyewe huko.
 
Niende moja kwa moja kwenye mada, mwezi wa 6, 2022 kuna jamaa aliniuzia gari Mkoa wa Mwanza (Crown 2010). Tukaandikishiana vizuri kabisa nikatoa hela nikapewa kadi, nikakamilisha taratibu kama bima nk sikuweza badilisha umiliki sababu ya kukosa nakala halisi za jina la mwenye kadi.

Basi katika kuvimba nalo mjini nashangaa juzi napigiwa simu na bi maza anayedai yeye ndo msimamizi wa mirathi nimeuziwa gari lake bila ridhaa yake na anakusaidia kunipeleka polisi kama mwizi wa gari.

Yule mama ana mkataba halisi wa mauziano ya gari yeye akiwa kama shahidi wa mume wake tena muuzaji akiwa ni yule ambaye jina lake lipo kwenye kadi.

Wakubwa nafanyaje kwenye hili? Nimevurugwa kabisa yule dogo aliyeniuzia simpati tena, maza mtu kasema ananipa mwezi mmoja niwe nimeshaamua.
NAANDIKA KWA HERUFI KUBWA

KAMA UNAYO MIKATABA YOTE YA MAUZIANO YA GARI NA KADI ORIGINAL UNAYO NJOO DM KWA MAMBO MAWILI

1,IJUMA TATU UKAFANYE TRANSFER KWA JINA LAKO LIWE KWENYE UMILIKI WAKO

2, NJOO NA PICHA DM ZA GARI KAMA IKO VIZURI HATA LEO NIKUPE HELA ILA TU UWE NA DOCUMENTS OG THE REST NIACHIE MIE

NAWAPENDAGA SANA HAWA WATU WENYE UTAPELI WA KISHAMBA SABABU TUNAKUTANA NAO SANA KWENYE BIASHARA ZETU.
 
Kiufupi hapa tayari kuna mgogoro, kama Mama anamuacha Mwanaye aliyekuuzia anakutafuta wewe moja kwa moja hiyo tayari ni familia ya "mchongo", hivyo kaa mkao tu.

Ingekuwa ni zile familia zenye hofu ya Mungu Mama angejiridhisha tu kuwa Mwanaye kauza Gari basi angeachana na wewe wakapambana wao wenyewe huko.
Huyo mama naona ni wale wa mama wanakuwaga waswahili swahili hawanaga dogo wale
 
NAANDIKA KWA HERUFI KUBWA

KAMA UNAYO MIKATABA YOTE YA MAUZIANO YA GARI NA KADI ORIGINAL UNAYO NJOO DM KWA MAMBO MAWILI

1,IJUMA TATU UKAFANYE TRANSFER KWA JINA LAKO LIWE KWENYE UMILIKI WAKO

2, NJOO NA PICHA DM ZA GARI KAMA IKO VIZURI HATA LEO NIKUPE HELA ILA TU UWE NA DOCUMENTS OG THE REST NIACHIE MIE

NAWAPENDAGA SANA HAWA WATU WENYE UTAPELI WA KISHAMBA SABABU TUNAKUTANA NAO SANA KWENYE BIASHARA ZETU.
Okoa jahazi kiongozi
 
Back
Top Bottom