Nimevaa sana mitumba ya kurusha, kutumia simu kioo kimepasuka miaka miwili, kutembea kubana nauli, niliyaogopa mapenzi, n.k, Umasikini ulaaniwe

Nimevaa sana mitumba ya kurusha, kutumia simu kioo kimepasuka miaka miwili, kutembea kubana nauli, niliyaogopa mapenzi, n.k, Umasikini ulaaniwe

round kick

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2025
Posts
345
Reaction score
1,145
Nikikumbuka maisha niliyowahi kuyaishi siwezi kuja kumuombea hata adui umasikini, Ni hali inayoaibisha, kukunyanyasa, kushusha heshima, kukutesa, n.k.

  • Nimevaa sana mitumba ya kurusha, kiatu unaenda kutafuta lisaa zima uone chenye nafuu
  • Simu imepasuka kioo miaka miwili sina pesa ya kubadili kioo
  • Kuna muda unatembea ili ubane nauli
  • Ombea usiumwe, shughuli inaanza unafika hospitalini huna Bima na mifuko imetoboka, ndio hapo unaanza kutafuta mizizi na mitishamba maporini
  • Nilipokuwaga mdogo nilikuwa nashangaa mtu anafikaje 30 hana nyumba wala gari, Nilitubu !!
  • Mapenzi ya kudumu yalikuwa kitendawili, ukiwaza wajibu wako kama mwanaume utamlishaje na utamtunzaje nguvu zinakuisha, commitment inapungua.
 
Umaskini unaaibisha, unanyanyasa, unashusha heshima, unatesa, katika kitu siwezi kuja kumuombea hata adui yangu basi ni umasikini, Looh !!

  • Nimevaa sana mitumba ya kurusha, kiatu unaenda kutafuta lisaa zima uone chenye nafuu
  • Simu imepasuka kioo miaka miwili sina pesa ya kubadili kioo
  • Kuna muda natembea ili nibane nauli
  • Mapenzi ya kudumu yalikuwa kitendawili, Ilikuwa inafikia muda natafuta mlango wa exit maana ni aibu huwezi kumpa mwanamke hata pesa ya matunzo,
Dogo,
Tumia pesa ikuzoee iwe inakutembelea
 
Pole
1000006259.jpg
 
mleta mada wala usiwe na wasiwasi maana wengi wetu ni sawa na wewe, tena ogopa sana sisi tukio kwenye mitandao ya kijamii, wengi wetu miguuni mwetu tume vaa yebo yebo , wengine hata hazujui tutakula nini jioni ya leo.


kwa kweli umaskini ni mbaya mno, vita yake kuishinda ni ngumu mno. kama ni laana basi moja ya laana mbaya kuwepo duniani ni umaskini.
 
Umaskini ni laana na fedheha
Umaskini unaaibisha, unanyanyasa, unashusha heshima, unatesa, katika kitu siwezi kuja kumuombea hata adui yangu basi ni umasikini, Looh !!

  • Nimevaa sana mitumba ya kurusha, kiatu unaenda kutafuta lisaa zima uone chenye nafuu
  • Simu imepasuka kioo miaka miwili sina pesa ya kubadili kioo
  • Kuna muda unatembea ili ubane nauli
  • Ombea usiumwe, shughuli inaanza unafika hospitalini huna Bima na mifuko imetoboka, ndio hapo unaanza kutafuta mizizi na mitishamba maporini
  • Mapenzi ya kudumu yalikuwa kitendawili, Mwanamke unakuta anakupenda ila hata kumpa pesa ya vizawadi au matunzo huna, sizungumzii zile level za kuhonga / vizinga bali kutimiza wajibu as a man, hata mahari ya laki 4 huna.
 
Umaskini unaaibisha, unanyanyasa, unashusha heshima, unatesa, katika kitu siwezi kuja kumuombea hata adui yangu basi ni umasikini, Looh !!

  • Nimevaa sana mitumba ya kurusha, kiatu unaenda kutafuta lisaa zima uone chenye nafuu
  • Simu imepasuka kioo miaka miwili sina pesa ya kubadili kioo
  • Kuna muda unatembea ili ubane nauli
  • Ombea usiumwe, shughuli inaanza unafika hospitalini huna Bima na mifuko imetoboka, ndio hapo unaanza kutafuta mizizi na mitishamba maporini
  • Mapenzi ya kudumu yalikuwa kitendawili, Mwanamke unakuta anakupenda ila hata kumpa pesa ya vizawadi au matunzo huna, sizungumzii zile level za kuhonga / vizinga bali kutimiza wajibu as a man, hata mahari ya laki 4 huna.

kiongozi tulia kwanza ueleze kwa utuo imekuwaje uko? umepatwa na nini? maana naona unatoa siri za kambi. kwanza unataka kwenda wapi au umeshinda bet?
 
Back
Top Bottom