JITU BANDIA
JF-Expert Member
- Feb 5, 2023
- 2,868
- 6,453
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kifo haisomewi chifuMbona hiyo ndio kazi walio iomba mkuu, yes hatuombei wafe lakini kufa haimaanishi basi waondolewe vitani.
Kuna jamaa hua anapenda kusema kwamba "usinitawaze kabla sijamaliza ku..ya".Kifo haisomewi chifu
Kupata vichekesho kama hivi huwa mnabonyeza ngapi?Na Kagame siyo wa mchezo mchezo. Ni Putin wa Afrika huyu, akiamua kumung'oa mama jua halizami.
Nakubaliana na nadharia hiyo kama potential future risk ambayo inabidi itafutiwe suluhisho. Namna moja wapo ni nationalism propaganda na ulinzi jamii ambapo Tanzania ilikuwa vizuri sana kipindi cha Nyerere kwenye nationalism thinking. Kuna uzembe wa effort siku hizi hasa zama hizi za mass media ambapo people are easily swayed by external influences (hata humu JF if the government is not careful) kuna wengi wana agenda tofauti na siasa za Tanzania na wanawajaza wanasiasa fikra za hovyo (hayo sasa matatizo ya teeth).Bahima Empire,Plundering and piracy ya resources ndio msingi mkubwa wa mauaji ya raia wasio na hatia..
Hatuwezi kuwa salama kama nchi ikiwa tutabariki uharamia wa rasilimali kwa wenzetu (DRC) wenye impact kubwa kwenye uchumi wetu..Logistics infrustructure and trade.
Tukizembea na kujizima data ipo siku M24 wataingia Ngara,Geita,Kahama,Biharamulo..
Well saidNakubaliana na nadharia hiyo kama future risk ambayo inabidi itafutiwe suluhisho. Namna moja wapo ni nationalism propaganda na ulinzi jamii ambapo Tanzania ilikuwa vizuri sana kipindi cha Nyerere kuna uzembe siku hizi hasa zama hizi mass media.
Lakini huko Congo lazima tuwe na objective what are we aiming for, hatuwezi ipenda East Congo- kushinda wa-Congo wenyewe, vinginevyo tunajipa kazi ya kudumu isiyo na lazima.
Serikali ya Congo ndio inatakiwa kuwa na long term strategy ya himaya zake Tanzania na wengine ni jukumu letu kuwasaidia kufikia adhma yao. Lakini aiwezekani kumsaidia mtu ambae hayupo serious. Nchi aina vita yoyote lakini inashindwa ku-commit ata robo ya jeshi lake kulinda eneo lao, nchi aina jitihada wala mpango wa nationalism propaganda, raia wenyewe wa maeneo hayo wanaongea kiswahili kushinda Lingala (if anything we should claim the region).
Kama nchi lazima tujiulize what’s the end game tunaisaidia Congo to attain what goals na sustainability ya wao kuilinda hiyo himaya ikoje; vinginevyo tunaji commit on indefinite peacekeeping mission.
Hakuna nchi duniani isiyo na mąkabila ya mpakani, kushindwa kulinda mipaka ya nchi yako ni uzembe tu. We can do business with whoever manages to control east Congo that’s our interest better still tunaongea nao lugha moja.
Who knows labda wakishaimega Congo uongozi utaachana na ushirikiano wa Kagame na kuangalia matumbo yao now that wako free ku trade na dunia wenyewe bila ya kutumia mgongo wa Rwanda either way we still win new trade partners.
Sisemi Tanzania iache kusaidia Congo but what is the end game, lazima tuelewe na mikakati yao kulilinda hilo eneo wao wenyewe, vinginevyo ni fruitless endeavour kwa upande wetu.
Kwa sasa anaenufaika na hayo madini ni Kagame rebels can’t trade on their own.Well said
Vikwazo vya kununua silaha dhidi ya DRC vina affect kwa kiwango kikubwa uwezo wa kijeshi..
Further hatuwezi kudharau Influence of western powers with regards to critical minerals exploitation..France,Belgium,UK..
Hiyo vita sio ya kuisha leo wala kesho provided M23 wana support ya nchi jirani. Adui (makundi yote ya waasi) wakizidiwa wanauwezo wa kupotea haraka kama walivyo na uwezo ku-mobilise jeshi haraka hali ikitulia na kulianzisha tena.
Tanzania na wasaidizi wengine waipe Congo ultimatum msaada wa kijeshi uende sambamba na serikali ya Congo kuwekeza heavily kwenye jeshi lao kulinda mipaka yao na kuli-control hilo eneo. Awawezi kuli-control hilo eneo ifike wakati tuache fate ichukue mkondo wake kama ni annexation ya eneo let it be aitokuwa nchi ya kwanza kumegwa kwa sababu ya serikali kushindwa ku-control eneo.
Bila ya Congo kutoa road map ya adhma yao ya kuli-control hilo eneo miaka 20 baadae bado tutakuwa tunapeleka askari wakati wenyewe huko Kinshasa wako busy kuboresha mikorogo na kukata mauno.
Ifike hatua lazima Tanzania ione seriousness ya Congo kutaka kulinda himaya zake yenyewe kabla ya kuji-commit kuwasaidia miaka zaidi ya 20 ya kuwasaidia inatosha kama wenyewe hawana mpango wa kuweka strong military presence huko. Kwani sisi nani alitusaidia Amini alipoitaka Kagera si wenyewe tulilinda eneo letu.
Let them annex it kama wa-Congo wameshindwa kulilinda eneo lao inatosha, watasaidiwa mpaka lini.
Iła M23 lazima nae atiwe adabu kipindi hiki kwa kuuwa askari wa Tanzania, lazima ajue sumu aionjwi.
Once that objective has been achieved what next, for that region?..SADC wanatakiwa kwenda KIVITA na kufukuza waasi wote.
..baada ya hapo eneo hilo lilindwe na askari wa SADC na kuwe na demilitarized zone ktk mpaka wa DRC na Rwanda.
..Na vita hiyo wasiachiwe Tanzania, Malawi, na South Africa, peke yao. Nchi zote za SADC ziamue kwa kauli moja kumtetea mwanachama mwenzao.
Wewe utakuwa na maslahi ya huko huko kama huoni tatizo linatokana na nani.Mama yetu mpendwa nakuomba uwaondoe haraka watoto wa taifa letu wanaopigana na M23 kule DRC.damu yao inamwagika kwa sababu gani?
Lah!Ndio maana kama nchi lazima tujue mafanikio ya msaada wetu huko tunapimaje kama kuwatwanga M23 sio kazi, shughuli ni kuhakikisha awaibuki tena huko mbele tukiondoka. Juzi tu Kenya kawatwanga M23 wakakimbia baadhi ya maeneo waliyokuwa wanashikilia. Baada ya Kenya kutoka tu maeneo waliyoyaacha wamerudi wameyachukua tena.
"Mwamba"? Nenda kamkumbushe habari za rafiki yake Kikwete usikie atakacho kwambia. Sasa anafanya kila juhudi kumweka mfukoni Samia!Mwamba akiongea hacheki
Hivi pk Ana machawa 😄
Ova
Once that objective has been achieved what next, for that region?
SADC wabaki huko permanent, maana wakitoka tu na waasi wanarudi upya. Warudishwe tena SADC kufanya kazi ile ile. Uoni kama ni cycle ambayo aiwezi kuisha, mwenye uwezo wa kuimaliza ni Congo mwenyewe au annexation tu.
Embu ingia YouTube tafuta documentary ya vita huko uone namna serikali ya Congo ambavyo hawapo serious. Hayo maeneo wamewaachia ‘have a go heroes’ low military officers kupambana na waasi wao wenyewe serikali kuu hawaja commit strong army presence maeneo hayo.
Sasa nchi ambayo border zake zote zipo salama wanauwezo wa kupeleka askari wengi na silaha huko lakini hawapo tayari kufanya hivyo utawasaidia mpaka lini. The only way kuna shida kubwa huko ni kwa sababu serikali ya Congo aipo fully committed kupambana na waasi. Utawasaidia mpaka lini.
Ndio maana kama nchi lazima tujue mafanikio ya msaada wetu huko tunapimaje kama kuwatwanga M23 sio kazi, shughuli ni kuhakikisha awaibuki tena huko mbele tukiondoka. Juzi tu Kenya kawatwanga M23 wakakimbia baadhi ya maeneo waliyokuwa wanashikilia. Baada ya Kenya kutoka tu maeneo waliyoyaacha M23 baada ya kuchezea kichapo wamerudi wameyachukua tena.
Uoni huu ulinzi ni shughuli ya kutwanga maji kwenye kinu ni kama kuwaendekeza wa-Congo tu ambao wao wenyewe hawapo serious.
Lah!
Umetiririka vizuri kiasi huko juu, halafu ukaja kufuta kila kitu huku mwishoni. Unasema "Kenya waliwatwanga M23"; ni M23 wa wapi hao waliotwangwa na Kenya?
Ninakubaliana nawe juu ya DRC kuchukuwa jukumu kubwa la kuhakikisha usalama wa nchi yao upo imara. Si sawa kulaumu serikali iliyopo sasa ya Tshekedi, kwani imeonyesha kujali swala hilo kuliko serikali zilizopita.
Ninakubaliana nawe kwenye swala la hao waasi kukimbia na kwenda kujificha, kwa sababu tayari walikwishafanya hivyo hapo 2012 walipochakazwa na jeshi letu wakakimbilia Uganda na Rwanda kwa wafadhiri wao, na kwenda kujiimarisha zaidi.
Kagame sasa hivi anatamba, na usidhani ataishia huko DRC, kwa sababu himaya anayoitaka ni kokote jirani kuliko na watu wa asili yake; kama Uganda na eneo kubwa la Kagera yetu, Geita na hata Kigoma. Tatizo linaanzia kwake.
Mkuu 'imhotep' usichanganye mambo na kuweka uongo usiokuwa na miguu ili kunogesha unakokupigania wewe. Biafra na DRC havina uhusiano wowote. Ni wakati sasa mwambieni kiongozi wenu Kagame kuwa hamuwezi kuwa nyinyi watu tofauti na wengine. 'Model' mnayoifuata ya wayahudi ni tofauti kabisa na haya mnayoyasukuma nyinyi.Hii inaenda kuwa kashfa kama ile ya Biafra tulisapoti wrong side katika History badala kujikita kwenye kupatanisha.
Col. Ojukwu hivi aliwahi hata kuja Nchini kutembelea makaburi ya Askari wetu kweli?
Au alikuwa anakaa kwenye Mahoteli ya hali ya juu na kubadilisha Wasichana Warembo huko Abidjan?
Kaa kimya wewe ndo hujui kitu Rwanda Haina hata fund za kufinance hiyo intelligence huo ujinga kawambie walevi wenzako wa kahawa