Nimwombe Rais Samia awaondoe haraka wanajeshi wetu kule DRC Congo. Mnapigana na nchi ya EAC

Nakubaliana na nadharia hiyo kama potential future risk ambayo inabidi itafutiwe suluhisho. Namna moja wapo ni nationalism propaganda na ulinzi jamii ambapo Tanzania ilikuwa vizuri sana kipindi cha Nyerere kwenye nationalism thinking. Kuna uzembe wa effort siku hizi hasa zama hizi za mass media ambapo people are easily swayed by external influences (hata humu JF if the government is not careful) kuna wengi wana agenda tofauti na siasa za Tanzania na wanawajaza wanasiasa fikra za hovyo (hayo sasa matatizo ya teeth).

Lakini huko Congo lazima tuwe na objective what are we aiming for, hatuwezi ipenda East Congo- kushinda wa-Congo wenyewe, vinginevyo tunajipa kazi ya kudumu isiyo na lazima.

Serikali ya Congo ndio inatakiwa kuwa na long term strategy ya himaya zake Tanzania na wengine ni jukumu letu kuwasaidia kufikia adhma yao. Lakini aiwezekani kumsaidia mtu ambae hayupo serious. Nchi aina vita yoyote lakini inashindwa ku-commit ata robo ya jeshi lake kulinda eneo lao, nchi aina jitihada wala mpango wa nationalism propaganda, raia wenyewe wa maeneo hayo wanaongea kiswahili kushinda Lingala (if anything we should claim the region).

Kama nchi lazima tujiulize what’s the end game tunaisaidia Congo to attain what goals na sustainability ya wao kuilinda hiyo himaya ikoje; vinginevyo tunaji commit on indefinite peacekeeping mission.

Hakuna nchi duniani isiyo na mąkabila ya mpakani, kushindwa kulinda mipaka ya nchi yako ni uzembe tu. We can do business with whoever manages to control east Congo that’s our interest better still tunaongea nao lugha moja.

Who knows labda wakishaimega Congo uongozi utaachana na ushirikiano wa Kagame na kuangalia matumbo yao now that wako free ku trade na dunia wenyewe bila ya kutumia mgongo wa Rwanda either way we still win new trade partners.

Sisemi Tanzania iache kusaidia Congo but what is the end game, lazima tuelewe na mikakati ya wa-Congo kulilinda hilo eneo wao wenyewe, vinginevyo ni fruitless endeavour kwa upande wetu.
 
Well said

Vikwazo vya kununua silaha dhidi ya DRC vina affect kwa kiwango kikubwa uwezo wa kijeshi..

Further hatuwezi kudharau Influence of western powers with regards to critical minerals exploitation..France,Belgium,UK..
 
Well said

Vikwazo vya kununua silaha dhidi ya DRC vina affect kwa kiwango kikubwa uwezo wa kijeshi..

Further hatuwezi kudharau Influence of western powers with regards to critical minerals exploitation..France,Belgium,UK..
Kwa sasa anaenufaika na hayo madini ni Kagame rebels can’t trade on their own.

Lakini tukiwaacha wakiweza annex na kupata independence yao they won’t need Kagame to trade. But still they will need our road and ports.

We don’t lose nothing, wanao loose ni Congo, Rwanda na Uganda we only gain another independent state trading partner.

Ifike wakati wa-Congo watueleze mipango yao ili kuendelea kusaidia au tuache fate ichukue mkondo wake.
 

..SADC wanatakiwa kwenda KIVITA na kufukuza waasi wote.

..baada ya hapo eneo hilo lilindwe na askari wa SADC na kuwe na demilitarized zone ktk mpaka wa DRC na Rwanda.

..Na vita hiyo wasiachiwe Tanzania, Malawi, na South Africa, peke yao. Nchi zote za SADC ziamue kwa kauli moja kumtetea mwanachama mwenzao.
 
Once that objective has been achieved what next, for that region?

SADC wabaki huko permanent, maana wakitoka tu na waasi wanarudi upya. Warudishwe tena SADC kufanya kazi ile ile. Uoni kama ni cycle ambayo aiwezi kuisha, mwenye uwezo wa kuimaliza ni Congo mwenyewe au annexation tu.

Embu ingia YouTube tafuta documentary ya vita huko uone namna serikali ya Congo ambavyo hawapo serious. Hayo maeneo wamewaachia ‘have a go heroes’ low military officers kupambana na waasi wao wenyewe serikali kuu hawaja commit strong army presence maeneo hayo.

Sasa nchi ambayo border zake zote zipo salama wanauwezo wa kupeleka askari wengi na silaha huko lakini hawapo tayari kufanya hivyo utawasaidia mpaka lini. The only way kuna shida kubwa huko ni kwa sababu serikali ya Congo aipo fully committed kupambana na waasi. Utawasaidia mpaka lini.

Ndio maana kama nchi lazima tujue mafanikio ya msaada wetu huko tunapimaje kama kuwatwanga M23 sio kazi, shughuli ni kuhakikisha awaibuki tena huko mbele tukiondoka. Juzi tu Kenya kawatwanga M23 wakakimbia baadhi ya maeneo waliyokuwa wanashikilia. Baada ya Kenya kutoka tu maeneo waliyoyaacha M23 baada ya kuchezea kichapo wamerudi wameyachukua tena.

Uoni huu ulinzi ni shughuli ya kutwanga maji kwenye kinu ni kama kuwaendekeza wa-Congo tu ambao wao wenyewe hawapo serious.
 
Mama yetu mpendwa nakuomba uwaondoe haraka watoto wa taifa letu wanaopigana na M23 kule DRC.damu yao inamwagika kwa sababu gani?
Wewe utakuwa na maslahi ya huko huko kama huoni tatizo linatokana na nani.
Lakini kwa kuungana na wewe kiaina fulani, ni wakati mwafaka DRC isimame kulinda maslahi yake yenyewe.
Huku kulialia na kukimbilia kwa majirani kutafuta msaada ni ujinga mkubwa sana.
Li nchi lote lile, tena tajiri kubwa litalizwaje na ki-nchi kama Rwanda!

Tanzania isipokuwa makini, inaweza kuwa kwenye mkumbo huo huo unaousumbua DRC. Viongozi tulio nao sasa hivi hawana upeo wa kujuwa hatari kubwa inayotunyemelea sasa hivi.
 
Mwamba akiongea hacheki
Hivi pk Ana machawa 😄

Ova
 
Lah!
Umetiririka vizuri kiasi huko juu, halafu ukaja kufuta kila kitu huku mwishoni. Unasema "Kenya waliwatwanga M23"; ni M23 wa wapi hao waliotwangwa na Kenya?

Ninakubaliana nawe juu ya DRC kuchukuwa jukumu kubwa la kuhakikisha usalama wa nchi yao upo imara. Si sawa kulaumu serikali iliyopo sasa ya Tshekedi, kwani imeonyesha kujali swala hilo kuliko serikali zilizopita.
Ninakubaliana nawe kwenye swala la hao waasi kukimbia na kwenda kujificha, kwa sababu tayari walikwishafanya hivyo hapo 2012 walipochakazwa na jeshi letu wakakimbilia Uganda na Rwanda kwa wafadhiri wao, na kwenda kujiimarisha zaidi.

Kagame sasa hivi anatamba, na usidhani ataishia huko DRC, kwa sababu himaya anayoitaka ni kokote jirani kuliko na watu wa asili yake; kama Uganda na eneo kubwa la Kagera yetu, Geita na hata Kigoma. Tatizo linaanzia kwake.
 
Mwamba akiongea hacheki
Hivi pk Ana machawa 😄

Ova
"Mwamba"? Nenda kamkumbushe habari za rafiki yake Kikwete usikie atakacho kwambia. Sasa anafanya kila juhudi kumweka mfukoni Samia!
 
Mbona kagame ameongea lugha rahisi sana inayoeleweka juu ya uwepo wa M23? Ni nini M23 wanachopigania ?
 

..nakubaliana na hoja zako zote ila hoja ya annexation ya sehemu ya DRC inanipa ukakasi.

..serikali ya DRC itawajibika kuweka mifumo ya kiutawala na kiulinzi baada ya SADC kuwafukuza hao wanaitwa waasi.

..pia kuwepo kwa demilitarized zone mpakani kwa DRC ili nchi yeyote isipate kisingizio kwamba jirani anapanga kumvamia.

NB:

..Eastern DRC ni shamba la Bibi la Kagame na Museveni. Wamekuwa mabilionea kwa kuiba madini ya DRC. Maokoto wanayoyapata DRC ndio yanawezesha kung'ang'ania madarakani.
 

View: https://m.youtube.com/watch?v=g8RyEDJeM3I
Ukiingia YouTube kuna video mpaka za hao M23 wenyewe kusema wanaachia maeneo, kuna video za wananchi kutoamini wakijua ni swala la muda tu watarudi.

Ukiingia YouTube kuna unlimited narrative and perspectives you want to hear on what Kenya achieved in short space of time.
 
Mkuu 'imhotep' usichanganye mambo na kuweka uongo usiokuwa na miguu ili kunogesha unakokupigania wewe. Biafra na DRC havina uhusiano wowote. Ni wakati sasa mwambieni kiongozi wenu Kagame kuwa hamuwezi kuwa nyinyi watu tofauti na wengine. 'Model' mnayoifuata ya wayahudi ni tofauti kabisa na haya mnayoyasukuma nyinyi.
Kubalini, kuishi na watu wengine mnaoishi nao, msijione nyinyi mnayo haki au utofauti wowote na raia wengine mnaoishi nao mitaani.
 
much know who knows nothing! about EAC intelligence,

much know who lacks intelligence!

KAGAME NI BABA WA INTELIJENSIA, KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA!

Kaa ukilijua hili kuanzia sasa! Na hata milele!
Kaa kimya wewe ndo hujui kitu Rwanda Haina hata fund za kufinance hiyo intelligence huo ujinga kawambie walevi wenzako wa kahawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…