Nina kijana mdogo ameathirika naishi nae, anagegeda sana vibinti vya watu, nimsaidiaje?

Nina kijana mdogo ameathirika naishi nae, anagegeda sana vibinti vya watu, nimsaidiaje?

Madam LadyAJ kwa heshima yako tafadhali...Rudi njia kuu,epuka huo mjadala
Kwa heshima yako
Huyu ni msengere nyuma tuuu,kinuka mkojo,anatafuta wa kumkojoza huyu.m.k.u.n.d.uwake mchaafuuu,,halafu anautingisha na kuimba churaaaa,akachambeeeee kwanza we chichidodoooo
 
Wakuu Wasalaam
Leo nimekuja tupeane uzoefu na ushauri.Nina bwana mdogo naishi naye.Ana miaka 18 kwenda 19 ni wa kiume.Huyu alikuwa mtoto wa jirani yangu kijijini nilipokulia.Ule ujirani wa kijijini ni kama ndugu tu,sbb huyu bwana mdogo toka anazaliwa mpaka anakua namuona,kila nikienda likizo basi namuona.Maana kwao na kwetu ni uzio wa minyaa tu ndio uliotutenganisha.

Huyu dogo wazazi wake wote walifariki kwa UKIMWI.Bahati mbaya na huyu dogo alizaliwa na maambukizi.Amekuwa hivyo huku akipatiwa dawa kuanzia umri fulani mpaka leo.Kilichonifanya nimchukue na kukaa nae,kuna wakati nirirudi likizo nikakuta dogo amedhoofu sana,sbb ilikuwa ameanza kugoma kutumia vidonge,hii ni baada ya kukua na kupata akili kuwa anatumia vidonge vile sbb ameathirika.

Ilihitaji ushawishi sana kumfanya dogo aendelee kutumia hizi dawa.Maana alikuwa mkubwa na akiwa shule akawa amepata akili kuwa vile vidonge anavyopewa kunywa ni kwa sbb ameathirika.Hakupenda kunywa akisema bora atangulie tu.

Sasa kwa sbb mimi kidogo ananiheshimu jumlisha kuniogopa,wakati wote wa likizo nikamsimamia aendelee kutumia dawa,hatimaye maamuzi ya kuja kuishi naye nilipo.Ameendelea kuwa na afya njema na tulimtafutia VETA baada ya kidato cha nne kutokufanya vizuri,na hii ni kwa sbb ni kama amekata tamaa.Kabla ya hapo darasani alikuwa anafanya vizuri sana kule sekondari.

Sasa bwana mdogo nilianza kustukia kuwa kaanza mahusiano ya kimapenzi.Na hii ni baada ya siku moja kumsikia akiongea kwenye simu asijue kama mimi na wife tupo ndani.Nikajipa zoezi la kutaka kuujua ukweli kupitia simu yake.Nikakuta kweli msg kadhaa toka na kwenda kwa mpenzi wake.

Kifupi dogo kaanza kugegeda,na alivyo HB na afya kuimalika huwezi kujua kuwa ameathirika.Sasa naona hata hapa mtaani kama vibinti vinamshobokea na havijui background yake.Hii inanipa wasiwasi juu ya afya yake na hao anaowagegeda.

Nilijipa siku nikakaa nae,nikampa somo kuwa hayo mambo anatakiwa kuyapa kisogo,atazame kwanza afya yake,lkn pia akumbuke bila kinga atwaangamiza vijana wenzake.Yaani ilikuwa kama nimeharibu.

Dogo akawa anaona kama namnyanyapaa!Anasema yeye pia ana haki ya kuwa na mtu maana umri wa kuwa na mpenzi eti umefika.Mimi kumwambia hivyo eti ni kama namnyanyapaa.Basi akaongea na mambo mengi yaliyonitia uchungu,sbb sikuwa na nia mbaya,bali kumsaidia yeye na hao watakaogegedwa nae.

Mimi bado nataka huyu dogo aachane na mwenendo wa kugegeda,japo nilionana na mshauri mmoja akasema sehemu nyingi huwa wanawatafutia vijana/wenza walioathirika ili wawe pamoja na kujijua kuliko kupeleka kwa wengine.Ila mimi naona umri wa huyu bado kwanza,atulie na kujenga afya.

Toka nimwambie alizila kula siku nzima,siwezi kumkaripia sana sbb ya hali yake.Sipendi aendelee sbb anaweza kuathiri afya yake na wale anaoshirikiana nao.

JF hakiharibiki kitu,kwa mazingira kama hayo,nyie wananzengo wenzangu mngefanyaje?Nifanyaje ili nimsaidie huyu dogo na huyo aliyeanzisha nae mahusiano?Tupeane mawazo.
Pole sana mkuu,hapo inabidi uwe unafatilia cm zake kwa siri bila yeye kujua,ukikutana na sms za mapenzi,mtafute anae wasiliana nae umpe ushauri namna ya kuishi na dogo mwathirika,na umwelekeze tu asimnyanyapae ila umpasulie ukweli kuwa dogo ni mgonjwa,hapo utakuwa umemuokoa asiambukizwe maana dogo anaonekana jeuri
 
siyo kila unaetembea na mwathirika utaupata kupata hiv ni mpaka usugue kweli kweli patokee mchubuko wote wawili unaweza kusex na mwathirika kama umemwandaa vizuri ukamlainisha na kutokukamia mechi ukatoka salama mkuu..
Sasa jamaa anakuambia na suga haswa n akishafanya yke mara mbili tatu anatema ananza project mpya
 
Akimuudhi sana atawachanja na kuwaambukiza makusudi,mimi ningemtimua ..potelea mbali..unakumbatia nyuki mkuu!
kweli,ni hatari sana kuishi na mtu ambae haikubali hali yake
 
Acha ushamba bwana....

*najuwa!!!!!
*kwa ha vitabu vya mungu!!!!!
*zambi!!!!
*kwa acha awagawie!!!!

We jamaa ni mshamba kweli.... Utadhani mwanaume wa mikoani

[HASHTAG]#Chief[/HASHTAG] Eng

hatuna neno "mwanaume" katika lugha ya kiswahili bali tuna neno "mwanamume" .........usipende kurekebisha wenzako hali na wewe hujui vizuri...........
 
hatuna neno "mwanaume" katika lugha ya kiswahili bali tuna neno "mwanamume" .........usipende kurekebisha wenzako hali na wewe hujui vizuri...........


Na wewe nae acha UBOYA...

Mwanaume ni LAHAJA ya pwani ya Lamu..
Mwanamume ni LAHAJA ya Kingazija...

Mimi natumia LAHAJA ya pwani ya Lamu..

Kumbe na wewe mshamba tuu!!!

[HASHTAG]#Chief[/HASHTAG] Eng
 
Hapa pagumu...

Tatizo kijana kama vile hajajikubali ingawa ana haki ya kuwa na mpz ila hana haki ya kuambukiza mtu
 
Huyu kijana akirudishwa kwao ndio atazidi kuambukiza kama kuwakomoa wengine, inaonekana ameshakata tamaa, na hivi anaishi town basi akifika kijijini videmu vitamshobokea balaa. Ni afadhali abakie naye amtafutie washauri wa saikolojia wamsaidie.


asante..ni mtazamo wako!

kwangu mimi ningemrudisha tu.
 
Haijalishi atajisikia vibaya au vipi,lazima ukae nae chini kwa Mara nyingine na kumwambia ukweli kuwa afanyalo sio vizuri unless anatumia kinga,lakini pia kama anataka kuanzisha mahusiano basi awe muwazi kwa huyo mpenzie juu ya hali yake,hatua nyingine zifuatwe iwapo atakaidi,anatakiwa afikiria maisha ya wengine pia,vipi ingekuwa Yeye afanyiwa hivyo angejisikiaje,pia anatakiwa afanyiwe cancelling.
 
huo siyo ushauri mkuu kwani kule kijijini hamana mabinti?cha msingi dogo apelekwe apewe ushauri nasaha msiangalie tuu kua anaambukiza maana uwezo huo hana kwa kua anatumia dawa sema kumshauri kua anapofanya ngono zembe pia anachukua maambukizi mapya kwa hiyo wale virus watakua wengi na watajenga usugu wa dawa muwe mnasoma kabla ya kutoa ushauri unapoathirika ukawa unatumia arvs huwezi muambukiza mtu maana wale wadudu wamelewa wamelala ila sasa ukifanya na ambaye hatumii dawa na ni muathirika apo unachukua maambukizi mapya na pia unapofanya sana kinga inashuka maana kwa umri wa huyo dogo utakuta anapiga bao zaidi ya tatu ...cha msingi apewe elimu ale vizuri aache mawazo ,afanye zoezi,apate mwathirika mwenzie anaetumia dawa afanye ngono kama kawaida bila madhara ataishi miaka mingi sana ....ukimwi siyo ugojwa...........
Aisee huu ushauri umenipa matumaini,nilianza kukumbuka ad vichenchede vyang nilivyopiga peku,dah!!!Siludiii tena
 
Haijalishi atajisikia vibaya au vipi,lazima ukae nae chini kwa Mara nyingine na kumwambia ukweli kuwa afanyalo sio vizuri unless anatumia kinga,lakini pia kama anataka kuanzisha mahusiano basi awe muwazi kwa huyo mpenzie juu ya hali yake,hatua nyingine zifuatwe iwapo atakaidi,anatakiwa afikiria maisha ya wengine pia,vipi ingekuwa Yeye afanyiwa hivyo angejisikiaje,pia anatakiwa afanyiwe cancelling.
Asante kwa ushauri
 
Nafikiri ushapata ushauri wa kutosha.

Niache nipite mkuu.

Maana ushauri wangu
Hutauweza ni lazima
Uwe na roho ngumu
Sana kuukubali na
Kuufanyia kazi ushauri wangu.
 
Ha ha ha hio simple sana, Huyo dogo mrudishe Bush kisha muwezeshe maisha kama kumfungulia mradi kama duka ama kilimo na ufugaji au mpe boda boda kisha mueleze ukweli kuwa kadri anavyojiingiza kwenye mapenzi ndivyo anavyo fupisha maisha yake. Kwakuwa ni mtu mzima ushauri haulazimishwi na ukiendelea kumfuga hapo kwako yatakayokukuta usimlaumu yeyote. Muwezeshe akaishi maisha yake mbali na hapo
 
Back
Top Bottom