Nina mashaka Luteni Urio anaenda kuharibu ushahidi dhidi ya Mbowe na wenzake 3. Fact hizi hapa
Na kwa nini mbowe ahitaji ulinzi wa makomandoo na sio mabaunsa ambao hata yeye anaweza kuwapata maana zamani walikuwa watumishi .wake akiwa na bilicanas?

Je, hao makomandoo wangefanya kazi zipi kwake ambazo zingekuwa mpya tofauti na maisha yake ya siasa zaidi ya miaka ishilini?

Je, wajua komandoo mmoja anaweza kuwa na athali kubwa kwa nchi ambayo raia wengi hawana uelewa wowote wa kivita?
CCM ya Sabaya walipanga kumuua, na mara mbili au tatu wameenda kumuua wakamkosa wakampiga mlinzi risasi. Mabaunsa wanalinda watu wanasitumia bunduki
 
Mimi nauliza swali moja tu.

Je bastola za akina Adamoo ni za halali?

Yaani umiliki wake unasomeka kama nani ndie anapaswa kuwa nayo kimatumizi?

Kosa la kukutwa na silaha ya moto kinyume na sheria inasemaje?

Tuanzie hapo kidogo....
 
Aisee, kiukweli ushahidi wa kubumba wa mtu aliyekalishwa chini ili akaseme uongo kum - incriminate ndugu yake asiye na hatia ni rahisi mno kuugundua kwa sababu huwa unakosa uhalisia na siku zote huyu shahidi wa uongo hujisahau na hukosa consistency katika melezo yake....

Kwa mfano, huyu Denis Urio, kuna maelezo ya matendo yake mwenyewe au ya wale anaotaka wahukumiwe akiwemo Freeman Mbowe hayana uhalisia bali ni hisia zake tu na kwa namna yoyote hayathibitiki na mtu mwenye akili timamu hawezi kuàmini wala kufikiri kutendwa na mtu smart kichwani mwenye nia kutenda uovu mkubwà kama wa ugaidi...!

Najua (anaweza) kuendelea kumwaga pumba zake kesho...

Nakubaliana na wewe kuwa, kwa hakika kabisa, pengine huyu Denis Urio ndiye anayeweza kuwa shahidi wa hovyo zaidi wa upande wa mashtaka kuliko mashahidi wengine 11 wote waliotangulia anàyejaribu kuweka wazi (expose) udhaifu wa mashitaka haya...!!!

Ni afadhali hata Kingai au Mahita...!!

To cut it short, hii timu ya kubumba kesi hii ili kum - incriminate Ndg Freeman Mbowe wamefeli kwa kiwango cha juu sana maana hata mjinga kabisa aweza kujua ukweli huu mpaka hapa ilipofika...!!
Mtego utakuwa kwenye tarehe na mtirirko wa matukio wa wa shahidi vs wa polisi
 
1. Wakati akitoa ushahidi wake wote Mara kadhaa wakili aliyemuongoza alisita kuendelea kumuuliza na kuanza kuteta chini kwa chini ikionesha Kuna majibu Alitoa nje ya matarajio yao.

2. Kucheleweshwa ushaidi wake kwa siku moja ama kulikuwa na mashaka juu ya ushaidi wake kutoka kwa mawakili wa Serikali au yeye mwenyewe.

3. Amejalibu kutoa kauli za kumtetea Mbowe kuwa pesa alizotumiwa na Mbowe zilikuwa za nauli kwaajili ya kuifikisha walinzi kwa Mbowe na sio za kununua vifaa au vya Ugaidi au malipo ya kufanya Ugaidi.

4. Hoja ya Mbowe kuajili makomando wanne tu kwaajili ya kukata miti NI kiloja kabisa. Kwamba iliitaji kuwa na makomando ndio wakate miti.

5. Je, makomando wanne wanawezaje kukata miti na kuchoma vituo vya mafuta tanzania nzima NI swali gumu kabisa kulielezea.

6. Je, mawakili wanaamini uchomaji vituo vya mafuta na kukata miti ungeweza kuvutia maandamano au kuwatia watu woga na kujifungia ndani? Kama vibomu vya machozi tu na milio ya riasasi watu hujifungia ndani milipuko ya vituo vingevutiaje watanzania kuandamana.

7. Tanzania Ina makomando wangapi? Makomando hao wanne wangesaidia vip Mbowe na elimi yake hao makomando wanne tu kusimamisha nchi isitawalike na kudhibiti makomando zaidi mia watiifu serikalinj.

8. Urio lazma aoneshe baada ya kile alichopanga baada ya kuchomà vituo NI vipi mbowe angepewa nchi na
sio Wanajeshi kuchukua nchi.

9. Je, urio hajaonesha chochote ambacho kinaonesha kuwa makomando wa Mbowe na yeye walivyojiratibu ualifu na ushaidi waliokuwa nao Kama vile kuambiwa siraha walizokuwa nazo.

10. Je, kwanini urio hakuchagua kusimama na makomando kwa kuweka nguvu kwao ya pesa na ata ajira serikalini upya ili waende kukusanya ushaidi wa ualifu na sio kuwaunganisha kwenye ualifu moja kwa moja.

11. Urio alionesha walijuana na Mbowe tokea 2009. Iweje Sasa Mbowe akate mawasiliano nae tu Mara baada ya kjmuunganisha na makomando. Yani akaacha kumwamini na kuanza kuwaamini makomando alikkutana nao chini ya mwezi na kuwashirikisha kwenye mipango hatari.
12. Kwanini wapelelezi walimuachia Urio jukumu la kutafuta watu wake mwenyewe na sio kumuandalia Kati ya hao watu makachero au kachero moja wapo ili akafanye Kazi na Mbowe ili wapate usibitisho kamili na usio na Shaka.
13. Kwa ushaidi wa Urio mtuhumiwa kamili alikuwa moja tu Mbowe. Hawa wengine NI watuhumiwa aliowafundisha uhalifu na kuwaingiza ni yeye.
14. Urio anakili pia kujua uadilifu wa watu alio mtafutia Mbowe afanye nao Kazi. Ndio maana akasema alijua wapo kwenye viapo na angewaambia kuhusu kufanya uhalifu wangekataa.
15. Urio pia anakili pia hao watu aliheshimiana nao na kujuana nao kitambo. Na aliwaalifu wakiona Kuna dalili ya uhalifu wamtaalifu. Akawakumbusha kuwa bado wapo kwenye kiapo. Hivyo yeye Kama kiongozi wao hakuwapanga kufanya ualifu. Je kwa mazingira hayo walithubutu vipi kuwa huru kumweleza moja kwa moja kuwa wanaenda kufanya uhalifu bila woga wowote Wala kuwashawishiwa kwake?.
16. Urio anasema hajui maana ya home boy.
17. Urio anaonesha pia kuaminiwa mwanzo na wapelelezi na kuachiwa kuratibu kilakitu. Lakini mwwishoni anaonesha kutoaminika Tena na kuombwa simu zake zichunguzwe. Maana Kama wangemuamini wasinge mnyanganya simu Bali waangemuomba namba zake za simu tu ili watafute ushaidi wanaoutaka. Kuchukua simu NI kutafuta ambayo hakuyasema.
18. Kwa kunyanganywa mawasiliano binafsi wakati yeye si muhalifu ilikuwa NI Kama kumtesa urio kisaikolkjia.
19. Urio anasema amejuana na Mbowe toka mwaka 2009. Toka wakati huo wote hajasema Mbowe kumshirikisha kwenye uhalifu wowote na kunachaguzi nyingi zimepita. Kwanini mwaka 2020 Tena Mbowe anashirikisha watu aliofahamina nao kwa siku chache mno. Chini ya siku 10.
20. Urio amejenga hoja tokea awali kuwa Mbowe aliitaji ukaribu na urio ili kupata mifumo ya ulinzi na kuwajua wanaoutaka kuhujumu chama kwa kutoa Siri.
Urio akija kesho mahakamani nishitueni. naona ushaidi wake unaegemea kumuondolea Mbowe shutuma.
Nyie mrukeruke ila kwa ushahidi wa upandewa mashtaka na weledi wa mawakili wa Mbowe- Mbowe ni mfungwa mtarajiwa
 
Na kwa nini mbowe ahitaji ulinzi wa makomandoo na sio mabaunsa ambao hata yeye anaweza kuwapata maana zamani walikuwa watumishi .wake akiwa na bilicanas?

Je, hao makomandoo wangefanya kazi zipi kwake ambazo zingekuwa mpya tofauti na maisha yake ya siasa zaidi ya miaka ishilini?

Je, wajua komandoo mmoja anaweza kuwa na athali kubwa kwa nchi ambayo raia wengi hawana uelewa wowote wa kivita?
Unaposikia makomando unafikiria ni watu wa aina gani? Komando akiacha kazi kazi anayoweza kupata uraiani ni ya ulinzi tu.
 
Na kwa nini mbowe ahitaji ulinzi wa makomandoo na sio mabaunsa ambao hata yeye anaweza kuwapata maana zamani walikuwa watumishi .wake akiwa na bilicanas?

Je, hao makomandoo wangefanya kazi zipi kwake ambazo zingekuwa mpya tofauti na maisha yake ya siasa zaidi ya miaka ishilini?

Je, wajua komandoo mmoja anaweza kuwa na athali kubwa kwa nchi ambayo raia wengi hawana uelewa wowote wa kivita?
Hawa makomandoo wa kubeba matofali siku ya uhuru wana tofauti gani na mgambo? hawana athari zozote
 
Mimi nauliza swali moja tu.

Je bastola za akina Adamoo ni za halali?

Yaani umiliki wake unasomeka kama nani ndie anapaswa kuwa nayo kimatumizi?

Kosa la kukutwa na silaha ya moto kinyume na sheria inasemaje?

Tuanzie hapo kidogo....
Thibitisha kwanza kama ile bastola ni ya Adamoo au alikutwa nayo. Leteni finger print. Baba acha kuwa mpumbavu. Fikili deeper between lines
 
"nilitumiwa na mbowe tsh 500000 kwenye kutoa haikutoka yote ikatoka 499,999" nimeutafuta sana huu mtandao ambao hauwasilishi kodi tra, gharama zake ni sh 1 tu! Hauna tozo wala vat
Kesi ya kutunga ni aibu kubwa sn, wameamua kutumia wachaga vichaa kumfunga Mbowe ionekane amefungwa na wachanga wenzake
 
Na kwa nini mbowe ahitaji ulinzi wa makomandoo na sio mabaunsa ambao hata yeye anaweza kuwapata maana zamani walikuwa watumishi .wake akiwa na bilicanas?

Je, hao makomandoo wangefanya kazi zipi kwake ambazo zingekuwa mpya tofauti na maisha yake ya siasa zaidi ya miaka ishilini?

Je, wajua komandoo mmoja anaweza kuwa na athali kubwa kwa nchi ambayo raia wengi hawana uelewa wowote wa kivita?
Na kwa nini miaka yote Mbowe na wengine wakati wakifanya siasa, serikali haikuwahi kuwashambulia kwa risasi viongozi wa upinzani au kuwavunja miguu kama walivyomfanyia Lisu na Mbowe katika kipindi hiki ambacho baada ya matukio hayo Mbowe akaamua kutafuta ulinzi madhibuyi zaidi?

Au kwa nini miaka yote viongozi wa upinzani na wanaharakati wakosoaji wa setikali hawakuwahi kutekwa, kupotezwa na kuuawa kama ilivyokuwa ikitokea wakati wa awamu ya 5 ambapo Mbowe anaona umuhimu wa kutafuta walinzi professional?
 
Komando mmoja ni sawa na wanajeshi wa kawaida 100,sasa komandoo wanne sini sawa na wanajeshi 400?.
Ninyi ambao hamna elimu yoyote ya mambo ya kivita ndiyo huwa mnalishwa huo upumb.avu.

Kwenye vita, wewe peleka makomandoo 4, mwezio apeleke wapiganaji wa kawaida 100, uone kitakachotokea. Mnalishwa ule upumb.avu wa waigiza sinema, nanyi mnaamini.

Hadhi ni tofauti na uwezo. Hadhi ya brigedia mmoja ni Askari 5,000. Wewe unaamini uwezo wa askari 5,000 wa kawaida wa kupigana ni sawa na brigedia mmoja?
 
Mimi nauliza swali moja tu.

Je bastola za akina Adamoo ni za halali?

Yaani umiliki wake unasomeka kama nani ndie anapaswa kuwa nayo kimatumizi?

Kosa la kukutwa na silaha ya moto kinyume na sheria inasemaje?

Tuanzie hapo kidogo....
Unaposema bastola za akina Adamoo unamaanisha walikutwa na bastola zaidi ya moja, unaonekana akili yako imeshikiliwa mahali si bule
 
Na kwa nini miaka yote Mbowe na wengine wakati wakifanya siasa, serikali haikuwahi kuwashambulia kwa risasi viongozi wa upinzani au kuwavunja miguu kama walivyomfanyia Lisu na Mbowe katika kipindi hiki ambacho baada ya matukio hayo Mbowe akaamua kutafuta ulinzi madhibuyi zaidi?

Au kwa nini miaka yote viongozi wa upinzani na wanaharakati wakosoaji wa setikali hawakuwahi kutekwa, kupotezwa na kuuawa kama ilivyokuwa ikitokea wakati wa awamu ya 5 ambapo Mbowe anaona umuhimu wa kutafuta walinzi professional?
Zile risasi walizopigwa akina Slaa Arusha kwenye maandamano! Na risasi walizopigwa akina Mbowe Kinondoni bahati mbaya zikamuua binti mpita njia! Ni ajabu yote hayo hauyajui.
 
Back
Top Bottom