Nina maswali kadhaa kuhusu mwenge

Nina maswali kadhaa kuhusu mwenge

Mtafute omary mnyeshani ameuelezea kwa kina sana na jinsi unavyofanya kazi kichawi akiwa mshiriki wa kuitambikia nchi mkoa wa Lindi na eneo analijua
Ndio nani huyo na nitamtafutia wapi
 
Maswali yangu ni kama ifuatavyo:
1)Tukiachana na blah blah faida inayopatikana kwa kuukimbiza mwenge ni nini hasa baada ya mabilioni kuteketea kwenye ukimbizaji wa mwenge ni kitu gani kinapatikana.

2)Mwenge huwa unahifadhiwa wapi(Mkoa) na mahali gani(jengo)?

3)Kiongozi wa mbio za mwenge huwa anachaguliwa kutoka wapi?

4)Je mwenge ukianza kuzunguka ni kweli hauzimwi?

5)Kuna uvumi nimekuwa nikiusikia wanaokimbiza mwengi huwa wanadanji uvumi huu unatokana na nini?

6)Mwenge unapokuwa sehemu kuna takribani watu wanne au watano wanatengeneza duara kuuzunguka mwenge kwa karibu kiasi cha kuvuta ule moshi na wanakuwa hapo kwa muda mrefu wakiwa wameunganishana je maana yake ni nini na je ule moshi wanaouvuta kwa muda wote ule hauwezi kuwaletea madhara?

7)Je mwenge ni mmoja huo huo miaka yote au huwa unatengenezwa kila baada ya muda fulani?

8)Nini asili ya mwenge na ulianza rasmi lini na kwa nini unahusishwa na uchawi?

Nadhani maswali haya yanatosha pengine nikipata majibu ya maswali haya kutoka kwenu nitaongeza maswali mengine

Huwa nauona mwenge kama ni kitu ambacho kinaabudiwa kama ambavyo masanamu yanavyoabudiwaga vile watu wanavyoukusanyikia nawaona kama wapo kwenye ibada kwa mungu Tamuzi au baphomet
Nakala kwa Mohamed Said
Mwengu wa mwaka huu unzindua kila kitu hata kama kuna upigaji, au kitu kipo chini ya kiwango..... hauna mvuto kabisaa
 
Back
Top Bottom