Nina milioni 5 nataka ninunue IST niifanye Uber

Nina milioni 5 nataka ninunue IST niifanye Uber

Hali kwasasa changamoto kidogo sasa nina kihela changu kama milioni 5 hivi sijui ninunue ist nifanye uber niendeshe mwenyewe sijui itanilipa
Naona Watu wengi wanakukatisha tamaa,ushauri wangu,kama hiyo fedha haitoshi nunua hata Bajaj ubaki na hela ya mafuta.
 
Kwa milioni tano ni ngumu kupata IST ya maana ili ufanye uber, pia biashara ya uber ni ngumu kwa sasa.

Ushauri wangu tu, chukua nusu ya hiyo pesa (2.5m) nunua pikipiki (boxer?) halafu fanyia biashara wewe wenyewe, hiyo hela nyingine weka akiba tu, wakati unapiga miche miche za bodaboda kuna deal za biashara zingine unaweza ukazijua then ukaitumia hiyo pesa iliyobakia kama mtaji. Kwa boda upo uhakika wa kulaza sio chini ya elfu 10 kwa siku.

Ushauri mwingine unaweza ukanunua bajaj used kwa hiyo milioni tano halafu ukapiga mwenyewe hiyo biashara, na kuwa na uhakika wa kulaza sio chini ya elfu 25 kila siku.
Noted
 
Naomba aliye kwenye hii game au alikuwepo ndio aje hapa atupe abc hili mtu unaamua kusuka au kunyoa kuliko wale ambao tumesikia toka kwa watu wengine ebu aje mtu hapa atuelezee kwa. Ufasaha kuwa hilo jambo gumu ugumu ni hivi na hivi au jambo zuri uzuri uko hivi na hivi itatusaidia wengi sio mimi peke yangu.asanteni
 
Hii bz za uber sijui aba kuna jamaa alinielezea nikabaki nashangaa wanapataje faida au labda sikuelewa vzr
Yaan mtu unamtoa ubungo had ununio kwa buku 4 😦😦😦
Ukirud bila mtu inakuaje na mafuta unaweka mwenyewe na folen hiz
 
Hii bz za uber sijui aba kuna jamaa alinielezea nikabaki nashangaa wanapataje faida au labda sikuelewa vzr
Yaan mtu unamtoa ubungo had ununio kwa buku 4 😦😦😦
Ukirud bila mtu inakuaje na mafuta unaweka mwenyewe na folen hiz
Hiyo pikipiki ? Tuma hapa screenshot inayoonesha hiyo bei kwa safari hyo
 
Fanya uber /bolt kwa malengo na kukomaa itakulipa sana ukikomaa huko..
!

Wanaosema hailipi wengine hata kuifanya hwajawai,

Wengine ni roho za kimasikini wanakatisha tamaa ili wawe wachache.

Wengi wanaosema hailipi ni waliowapa watu magari!
 
Vipi kuhusu vits au basi nipambane nipate japo ist niongeze ata ifike 7 au 8m naweza kupata ist mkuu ila madalali sasa ndio shida sana
Kama unaweza kupambana kuongeza toka 5 -7-8 kwann usiendelee kupambana tu mbona kama inakulipa? Au me sjaelewa unatoa wap hzo za kuongeza au unataka Acha kaz sehemu
 
Nimesikiliza Kipindi cha Power Breakfast Asubuhi ya Leo Clouds Fm, Madereva wa Uber na Bolt Wanalia Kamisheni Kushushwa Toka Kulipwa Tshs 950 kwa Kilometer hadi Tshs 450 kwa Kilometer
.
Mdau Anasema kwa Siku Kama Una-drive Uber au Bolt kwa Upande wa Gari, Mafuta Ukiweka Tshs 35.000 Kama Litres 15 hivi Unaweza Kuingiza Kuanzia Tshs 100.000 (Ukikomaa Haswa)
.
Mgawanyo wa Asilimia Wenye Mtandao wanachukua 30% na Dereva anachukua 70%
.
Hapo Inamaana Ukitoa 30% ya Tshs 100.000 ni Tshs 70.000, Ukitoa na Petrol 35.000 Utabaki na 35.000. Hapo Kuna Kula, Kunywa Car Wash na Mengineyo, na Abiria Akiripoti au A-Comment Kuwa Gari yako Chafu Unalo
 
Back
Top Bottom