Nina mtaji wa laki moja. Je nifanye nini ili niwe napata angalau elfu mbili kwa siku?

Hii biashara ya nyamanyama za mbuzi
kuna faida kubwa mno afanye utafiti vzr,
ikimshinda aingie kwenye matunda nako atalala hata na msimbazi
 
Umeandika kama motivesheno spika
Binadamu sisi ni wavivu sana WA kufikiria ujue ..
Ngoja nikupe practical example ya jibu langu .
Mtaji 100,000/=
Makazi ninayoishi : Karibu na stand ya mabasi
Watu wengi maeneo hay ni ( abiria , wapiga debe)
Swali la kujiuliza ni moja tu nifanye kitu Gani kuwaboreshea Hawa watu shughuli zao au kazi zao kulingana na tabia zao?

1.Abiria ( kundi hili wanapenda vinywaji, vyakula, na vitu ambavyo ni simple sana . Sasa hapa nikianza na idea ya kuuza maji Tafuta deri na mabarafu unaweka maji yanakuwa baridiiii Caton moja ya maji unainunua 9000 zipo chupa 12 ukiuza buku buku unatoka na 12000 faida 3000 .. Uza soda za kopo pia faida ni 2000 -3000 kwa Caton moja. Hapo unahitaji Caton 4 tu thamani ya elfu 40000 kutengeneza faida ya tsh 10000.

2. Wapiga debe (wengi wa Hawa watu wanatumia vinywaji vikali chukua chupa kubwa break down weka kwenye ujazi wa kawaida uza kwa Bei rafiki , wanapenda sigara nk.)
Hapa mpaka jua linazama uko hoi ila pia una maokoto
 
Haya ndio maneno sasa, ukiona mpaka mtu kaja humu ndani kuomba msaada ujue akili yake ishafika mwisho kuona fursa.
 
Haya ndio maneno sasa, ukiona mpaka mtu kaja humu ndani kuomba msaada ujue akili yake ishafika mwisho kuona fursa.
Sio poa yaani hapa kwenye kuumiza kichwa Kuna advantage sana sababu kama wazo ulilianzisha mwenyewe ni rahisi kumodify na kuongeza mambo ya msingi kuongeza faida tofauti na wazo la kucopy.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…