Nina wazo la kufanya hii 'project' kwa mwaka 2022

Nina wazo la kufanya hii 'project' kwa mwaka 2022

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Kauli mbiu ni kufanya uzalishaji vijijini, na kuleta mauzo mjini. Kwa yeyote atakayependa wazo langu, anaruhusiwa kulitekeleza; elimu haina mwisho.
Nitaanza hivi:-
  • Nitafungua kampuni yenye jina 'Equation x agricultural adventure'
  • Nitatafuta binti wa kazi mpambanaji kweli kweli mwenye cheti cha kilimo
  • Nitampiga semina ya wiki moja, ili aweze kuelewa ndoto zangu
  • Nitampa safari ya kutembelea vijiji 10 vyenye ardhi ya rutuba katika mikoa 2, kwa kuanzia.
  • Nitaingia mkataba wa miaka 2 au 5 kwa kukodi mashamba kwa kila kijiji nitakapofanikisha
  • Itakuwa vizuri kama nitapata kuanzia ekari 5 kwa shamba
  • Sehemu ambayo mkataba utaanzia miaka 5, nitapambana nichimbe kisima ili kilimo cha umwagiliaji kiwe rahisi.
  • Wafanyakazi wa shambani watakuwa wanakijiji, pamoja na mtaalamu mmoja atakayekuwa anawazungukia.
  • Nitalima zao la muda mfupi ambalo tayari soko lake nimeshaliona.
  • Mi nitakuwa napambana mjini pamoja na kujibana, huku fedha zangu zikiwa zinaenda kijijini kwenye kilimo
  • Baada ya mavuno, mazao yataletwa mjini kwa mauzo; nitatafuta kijana wa cheti cha mauzo.
  • Mafanikio yakiwa vizuri, nitaongeza wigo kwa kuongeza mikoa mingine.
  • Naimani, huu mradi utanilipa

Nawakaribisha kwa mawazo.

NB: Kuhusu wafanyakazi, nitawatengenezea mpango kazi wa kila siku, na kila siku jioni lazima wafanye presentation; ambaye atakuwa hajafanya chochote, ataenguliwa.
 
Ni wazo zuri sana ila kitachokukwamisha ni uaminifu tu
Soko la uhakika linaweza kupatikana ila unahitaji partners wa kuwepo kila wakati kwenye kila mradi wako
Kwa mwanzoni, nitaanza na vijana wawili wenye certificate; mmoja kilimo, mwingine mauzo; hawa kazi yao ni kuzunguka kwenye masoko na shambani. Kwa kila shamba kijijini, nitatafuta mzee mtu mzima moja ambaye atakuwa anaripoti kwangu kimawasiliano.
 
Very easy behind the keyboard
Inawezekana mkuu, kuna rafiki yangu nimekutana naye anafanya hii kazi; anawekeza m3 anapata hata zaidi ya mara 2. Jifunze kuwa karibu na waliofanikiwa, upate ujuzi. Ukiwa na marafiki wengi walioajiriwa hawatakusaidia kitu, zaidi za kukuambia kila kitu hakiwezekani, ndio maana wanazeeka kwenye kuajiriwa.
 
Too many unknowns..., sio kwamba haiwezekani but its not easy it needs dedication as there are ups and downs not plain sailing..., kwahio kama upo dedicated na unapenda unachofanya utachukua the rough with the smooth.... Kama una-enjoy the ride hata destination ikichelewe au usipofika bado unakuwa na furaha...
 
Too many unknowns..., sio kwamba haiwezekani but its not easy it needs dedication as there are ups and downs not plain sailing..., kwahio kama upo dedicated na unapenda unachofanya utachukua the rough with the smooth.... Kama una-enjoy the ride hata destination ikichelewe au usipofika bado unakuwa na furaha...
Tuangalie upande wa technicalities kwa nini ishindikane mkuu?
 
Inawezekana mkuu ila kwa kuanza punguza kwanza kuanzia vijiji, fanya kwa vichache tatu hadi tano na hizo ekari pia zisiwe nyingi sana ila miaka ni sawa koz kila mwaka unakuja na mafanikio yake kuanzia hali ya hewa mpaka soko, Kwakuwa sijui uwezo wako wa kimtaji yaani pesa naweza kusema gawa mtaji wako mara nne au tatu uingize mdogo mdogo, kwa mwanzo lazima utagonga loss za kutosha utakuwa na faida ya uzoefu tu ila mwisho na uhakika jembe halimtupi mkulima
 
Tuangalie upande wa technicalities kwa nini ishindikane mkuu?
Sijasema inashindikana lakini kuna unknowns za kutosha...

Upate wafanyakazi wachapakazi wenye experience na ujuzi na bado uwalipe na wewe kubaki na faida
Unalima hence yield ya mazao nayo ni unknown
Kuna investment utafanya ya kununua au kukodi vitendea kazi haujajua lini uta-break even na if uta-break even
Soko, hauna wala haujapata soko la uhakika kwahio hujui hicho utakachouza kama kitapata faida baada ya kuondoa matumizi..., hata kama kinalipa leo haujui kesho kama kitalipa

Ushauri anzia kwenye soko alafu rudi kwenye production.., hicho unachotaka kuuza kwanza nunua na uza kama middle men na unavyopata soko zaidi anza production mwenyewe....
 
Inawezekana mkuu ila kwa kuanza punguza kwanza kuanzia vijiji, fanya kwa vichache tatu hadi tano na hizo ekari pia zisiwe nyingi sana ila miaka ni sawa koz kila mwaka unakuja na mafanikio yake kuanzia hali ya hewa mpaka soko, Kwakuwa sijui uwezo wako wa kimtaji yaani pesa naweza kusema gawa mtaji wako mara nne au tatu uingize mdogo mdogo, kwa mwanzo lazima utagonga loss za kutosha utakuwa na faida ya uzoefu tu ila mwisho na uhakika jembe halimtupi mkulima
Uko sahihi mkuu, kinachokwamisha kilimo ni kutegemea kilimo cha mvua, lengo langu ni kujikita maeneo yaliyokaribu na vyanzo vya maji. Nitatumia muda mwingi kupata shamba sahihi na watu sahihi. Kama watu wanatoka nchi ya mbali na kulima huku, kwa nini sisi tushindwe
 
Uko sahihi mkuu, kinachokwamisha kilimo ni kutegemea kilimo cha mvua, lengo langu ni kujikita maeneo yaliyokaribu na vyanzo vya maji. Nitatumia muda mwingi kupata shamba sahihi na watu sahihi. Kama watu wanatoka nchi ya mbali na kulima huku, kwa nini sisi tushindwe
Thats right ndo maana nikuambia usiwe na haraka sana na faida koz hayo yote unayoelezea ni utafiti tu na utafiti hauzalishi ila baada ya hapo lazima upate kitu cha kutosha mkuu kama hautaishia kwenye maneno tu nina uhakika wa wazo lako kufanikiwa kutegemeana na nguvu yako lakin koz sikufahamu
 
Sijasema inashindikana lakini kuna unknowns za kutosha...

Upate wafanyakazi wachapakazi wenye experience na ujuzi na bado uwalipe na wewe kubaki na faida
Unalima hence yield ya mazao nayo ni unknown
Kuna investment utafanya ya kununua au kukodi vitendea kazi haujajua lini uta-break even na if uta-break even
Soko, hauna wala haujapata soko la uhakika kwahio hujui hicho utakachouza kama kitapata faida baada ya kuondoa matumizi..., hata kama kinalipa leo haujui kesho kama kitalipa

Ushauri anzia kwenye soko alafu rudi kwenye production.., hicho unachotaka kuuza kwanza nunua na uza kama middle men na unavyopata soko zaidi anza production mwenyewe....
Kilimo kina changamoto nyingi sana, kuhusu soko mazingira yote nitayatumia; nita-email mazao yangu kwa nchi za jirani, fb, youtube na mitandao mengineyo
 
Thats right ndo maana nikuambia usiwe na haraka sana na faida koz hayo yote unayoelezea ni utafiti tu na utafiti hauzalishi ila baada ya hapo lazima upate kitu cha kutosha mkuu kama hautaishia kwenye maneno tu nina uhakika wa wazo lako kufanikiwa kutegemeana na nguvu yako lakin koz sikufahamu
Ni kweli mkuu,nikipata nguvu kazi sahihi, kazi itafanyika mkuu
 
Kilimo ni kizuri sana !! Ndo kinaniweka mjini !! Ila shamba linataka uwe karibu nalo aseee vingine project itakwama mapema sana !! Hiyo habari ya wewe kukaa mjini ukijibana huku shamba linaendelea ! Usimuamini mtu jombaa !
Ni kweli mkuu,ndio maana nataka nitumie nguvu kubwa kupata wasaidizi mkuu
 
Yaaah mkuu.....project iko vzr ....mimi mwenyew nawazia project kama hyo but mi nitajikita kwenye ufugaji zaidi.....

Everythng is possible
Yote inawezekana ukiamua, pia gharama za kijijini ziko chini
 
KILIMO CHA KWENYE MAKARATASI NA WHATSAPP KINALIPA SANA, INGIA KWENYE FIELD MWENYEWE UONE KAZI ILIPO

MAMBO YA UKO MJINI SHAMBA KIJIJINI UMEMUACHIA MTU MWINGINE KWA UAMINIFU UPI?
Ni kweli mkuu,nitajikita kwenye kupata mtu sahihi; nitaanza na wenye cheti kwanza
 
TZ hiyo haiwez fanya kazi, Uaminifu zero,
Si unaona Mzee Pinda anaingia front mwenyewe

Tafuta kijana aliyemaliza Kilimo SUA, mtengeneze kampuni ya kilimo, mgawane shea wewe 70% yeye 30%,
70% yako ikiwa initial investment za kununua mashamba, vifaa vya kilimo, gharama za kulima plus mshahara kwa huyo kijana (lets say 300,000Tsh per month)
Hapo kijana atajituma kama mfanyakazi na kama mwenye kampuni, then in 3-5years ndo muanze gawana faida.

At least it can work ila initial cost itakuwa juu, ukishindwa hii ingia front mwenyewe
 
Back
Top Bottom