Ninaposema Mwafrika kapunjwa akili na Mungu kwa makusudi kabisa muwe mnaelewa. Rejea ajali ya ndege Bukoba 06/11/2022

Ninaposema Mwafrika kapunjwa akili na Mungu kwa makusudi kabisa muwe mnaelewa. Rejea ajali ya ndege Bukoba 06/11/2022

Hiyo haiwezi nyenyua ile ndege hata ikiwa tupu.

Ile ATR 42 ikiwa tupu ni 11.7T
Helicopter hiyo ya Airbus ni 5.T lift capacity
Sawa mtaalam.
Basi ingekuwepo around pamoja na divers waokoe watu.
 
Habari

Mimi nitazungumzia vitu vichache tu kati ya vingi vilivyojitokeza jana ambavyo vinaonyesha ufinyu wa akili wa viongozi wetu ambao ndio wanawakilisha uhalisia wa wananchi.

1. Ziwa Victoria pamoja na ukubwa wake na umuhimu wake kiuchumi serikali haijaweka boti angalau 4 za dharura kwaajili ya kufanya uokoaji na dharura.

2. Kuajiri kwa uchache Askari na maafisa wa jeshi la zimamoto na uokoaji pamoja na kuwapa vitendea kazi vichache . Jeshi la zimamoto na uokoaji lina watumishi wachache sana na vitendea kazi pia vichache. Hakuna KITUO CHA jeshi la zimamoto na uokoaji kando ya ziwa ili kudeal na dharura za ziwani.

3. Viongozi haraka wamekimbilia kutoa majibu ya sababu ya ajali ile ndani ya masaa machache ili kulinda ugali wao. Ni wazi Mwafrika kakosa utu na ni mbinafsi asiyekubali kuachia nafasi.

Maelfu wanavushwa na vivuko hapa Tanzania kila siku huku pembeni kuna kiboti kidogo cha uokoaji kinachoweza kuokoa watu 10-20 huku kivuko kina maelfu ya abiria. Hili nalo muende mkalitizame. Na ajabu zaidi kiboti hicho kidogo cha uokoaji kimepark pembeni hakina hata habari.
Tena muda mwingine hicho kiboti kidogo cha uokoaji kilichopaki pembeni hata mafuta hakina yaani ikitokea ajali hakiwaki...... Sisi ni bado saana mkubwa.!
 
Hii ajali ukiangalia kwa upana na marefu yake. Ni ajali ya kukosa uwajibikaji. Yani tumerudi kule tumetoka. Jiulize angekuwa hai Mzee Magu.... End
Mama anayesufiwa anatoa tamko la kijana mwokoaji aajiriwe Jeshi la maji, badala ya kutafakari wapi palikuwa na tatizo kwenye uokoaji na bila kuwa na vifaa !! Angetoa tamko la kununua boti ya mwendo Kasi ya uokoaji tungemwelewa.
Kwa hiyo kijana akiajiriwa ndio kifaa cha uokoaji ikitokea tatizo lingine si ndio!! Ama kweli Kuna aliyeturoga na alishaondoka zake!!
 
...Na Ajali Ile ya Meli pale Mwanza Miaka Michache nyuma inaelekea haikufundisha lolote licha ya Matamshi Kadhaa ya Kisiasa yalitolewa wakati ule!!
Mkuu, hilo ndilo kinaloumiza, ungetembea baada ya ajali ya Mv Bukoba, vitengo vya ukoaji na boti maalumu kwa ajili ya kazi hiyo ningeanzishwa Mwanza, Bukoba na Kigoma, ili kukabiliana na ajali zinatokea katika ziwa Victoria na Tanganyika.
Ni kweli ajali haina kinga, lakini ikitokea inabidi itupe somo.
Kwangu mimi ndio hapo naona uzembe wa serikali, sio hii ya Mama Samia tu, bali tokea nyuma.Mungu libariki taifa letu.
 
Naomba kufahamishwa kazi ya wanajeshi wetu wa Navy tafadhali.
Wanajeshi wanahusikaje hapo??? Uliza kazi ya jeshi la zima moto na uokozi linakazi gani? Kusubiri moto?? Uliza tena vituo vyao kwa nini vipo mjini peke yake? Ziwani na vijijini hakuna majanga??? Ziara ikatizwe.
 
Wanajeshi wanahusikaje hapo??? Uliza kazi ya jeshi la zima moto na uokozi linakazi gani? Kusubiri moto?? Uliza tena vituo vyao kwa nini vipo mjini peke yake? Ziwani na vijijini hakuna majanga??? Ziara ikatizwe.
Mimi nimeuliza swali maana yake sikuwa nafahamu. Ila tayari nimeshaelimishwa. Asante
 
Tuendelee tu kuwa waoga kwa kisingizio cha amani lakini ukweli ni kwamba siku tunavamiwa na jeshi la nchi nyingine tunaweza tukateketea kama kuku.
Yaan mnamaanisha siku tunavamiwa tunakufa km Kuku huku wao wakiwa wamekaa tu pembeni wanatuangalia tu tunavyokufa wakiwa wanasubiria amri kutoka juu au sijaelewa mkuu?
 
Yaan mnamaanisha siku tunavamiwa tunakufa km Kuku huku wao wakiwa wamekaa tu pembeni wanatuangalia tu tunavyokufa wakiwa wanasubiria amri kutoka juu au sijaelewa mkuu?
😀😀 hilo nalo linawezekana.
Au wanaweza wakaja vitani bila silaha
 
😀😀 hilo nalo linawezekana.
Au wanaweza wakaja vitani bila silaha
Duuuh alafu wananchi wakaanza kujipambania na silaha za kijadi, itakua kubwa kuliko hio itavunja rekodi dunia nzima
 
Rescue facilities siyo boti tu...na ukitaka kuweka kila sehemu ni ghali kwetu sisi,siami kwamba hakuna patrol boats Viktoria..lakini moja itasaidia nini!?
Unaambiwa kila Halmashauri ina Kamati ya Maafa

Serikali inatenga Fungu kwa ajili ya Maafa na kila Halmashauri inapewa Fungu lake

Nini kazi ya hili Fungu?

Na kusipotokea Maafa hilo Fungu linakwenda wapi?

Hili swali kuna mdau aliwahi kuhoji

Sasa hili Fungu sijaelewa linatengwa kwa ajili ya kuokoa watu wanapopatwa na Maafa na kabla ya watu kupatwana Maafa au linatengwa kwa ajili ya kuzikia marehemu baada ya Maafa?

Yaan utaambiwa, 'Serikali itagharamia Mazishi', Pesa ya kugharamia Mazishi inatoka kwenye lile Fungu la Kamati ya Maafa kutoka Halmashauri lililotengwa na Serikali
 
Mimi lawama zote nawarushia CCM maana ndiyo Serikali inayoongoza nchi.
Serikali ya CCM inaona ma Toyota VX V8 ni muhimu kuliko uhai wa mwananchi.

Kiongozi wa CCM anakurupuka na matamko ya kisiasa, aache watu wa plane crash investigation wafanye kazi yao.

Hii nchi msishangae kusikia Black box imeibiwa ili tu kufanya uchunguzi wa kitaalamu usifanyike kumlinda PM na kauli yake asije akaumbuka.
Kwani PM alisemaje mkuu?
 
Back
Top Bottom