Ninavyowafahamu wateule wapya wa Rais Samia kwa historia yao ya nyuma na uhusiano wao na viongozi wa leo

Ninavyowafahamu wateule wapya wa Rais Samia kwa historia yao ya nyuma na uhusiano wao na viongozi wa leo

Kwa January umenena kweli IQ ndogo,pozi lake la kierevu🤣🤣🤣.

Huyu Hana tofauti na Kikwete yeye hujiona ni rais bora zaidi kuwahi kutokea ktk nchi hii kisa wazungu wanaikubali mpaka leo😂😂😂.
 
JPM alijaribu kuharibu hizi circle za madaraka kwa kuleta walau akili mpya lakini sasa tunarudishwa mule mule tena kwa lazima.

Ina maana hii nchi hakuna brain nyingine za kuongoza hadi turudie makosa haya haya kila mwaka?
Naamini mama anaambiwa amchague nani na amtumbue yupi. Kwa ufupi kuna nguvu kubwa inayohakikisha mama anatimiza matakwa ya hiyo nguvu. Kumrudisha fisadi na msanii Makamba? Angalia mkuu wa mkoa Dar? Nani asiyejua ngivu hiyo? Tunasubiri naye Membe aletwe kundini
 
Wote walioteuliwa wanafahamika kwa sura na kwa tabia. Sababu za kuteuliwa kwao ndo vigumu kuzitambua. Hapa nitajaribu kuzitaja kadri ninavyowafahamu.

Tuanze na Stergomena Tax
Huyu ni mtu mwenye elimu nzuri, mwanamke ambaye ktk wengi walioko baraza, hatuna wanawake wenye uwezo. Ana matatizo yake ya elimu ya u-daktari lakini haina shida. Tutegemee atumie Masters yake na siyo Ph.D uonayo kwenye jina. Kwa tamaa ya kuwa na akina mama, ameweza kuuzika kiurahisi kwa wizara ambayo kazi yake ni kusoma bajeti tu!

Ashantu Kijaji
Ni msomi, aliyeanzia kwenye akademia. Akiwa naibu waziri hakufanya vibaya na ana tabia ya kupenda maendeleo ktk jimbo lake sana, kwa kuwasikitikia viongozi wa serikali wasiojali maisha ya walio chini. Ni kiongozi mzuri ambaye haijulikani ni kwa nini hakupanda baada ya kuwa Naibu wa wizara ya fedha. Akiwa mwanamama, anastahili kujaribiwa.

Januari Makamba
Ana uwezo mdogo ambao hufichwa na ushujaa wake wa ku-pozi kama mwerevu. Hakustahili kuingia tena ktk baraza, lakini kuna nguvu kubwa ya urafiki. Ni misheni tauni sana na nasaha za internet kwa wingi ili aonekane ni msomi. wapo akina Rostam, wanufaika wa wizara yake na bado wanapenda kunufaika. Yupo na mstaafu JK anayemkumbuka kwa kuamini atapanda kulinda maslahi yake. Nishati ni wizara ambayo inawanufaisha watu kupitia umeme migodini, mafuta, na vituo vya hovyo hovyo na ukwepaji kodi ktk sekta hii. Ameingizwa ili kazi iendelee. Tutalizwa tu!

Makame Mbarawa
Ni waziri wa kuteuliwa miaka mingi, akitokea Pemba ambako CCM kwao ni ndoto kushinda kihalali. Amekuwa akiteuliwa ili kulinda nafasi ya Pemba. Alikuwa waziri mzuri kwa misingi yake ya kutokea akademia. Tatizo lake alijiingiza kwenye rushwa za wizara ya maji na akaanza kutafuta pesa alizoziita za uchaguzi, akifahamu Pemba hawezi pita. Naamini ameingizwa kwa msimamo wa rais kuinua kuonekana kwa Z’bar pamoja na kwamba uaminifu wake ulishaingia doa.

Eliezer Feleshi na Adelardus Kilangi
Hawa wamekuwa ktk mkanganyiko sana lakini Kilangi tangu alipoingia alikuwa ni mtu ambaye ni kama alibebwa saana bila kujali uwezo wake. Badala yake tukaambiwa sijui anaaminika wapi na wapi lakini msingi wake ktk sheria na hata sifa ya profesa haina msingi wa kuaminika.

Feleshi simfahamu sana ktk mambo yake ya kiofisi. Je ni uzoefu wake wa kunyamazia maovu ktk awamu ya 4? Kama ni hivyo basi naye kaingizwa kwa mtindo wa kazi iendelee. Tutapigwa hadi nchi ichakae.
Dai katiba acha majungu, na mpgiwe mchakae tu . Tukiwamahasisha kudai katiba mnatuita magaidi
 
Japokuwa Rais hapangiwi nani wa kuwateua katika nafasi mbalimbali, lakini ni sahihi wizara isiyo ya Muungano kupangiwa watu kutoka upande wa pili wa Muungano.Pili ni sahihi mkoa mmoja kuwa na mawaziri watatu, kutoka kwenye majimbo, wakati mikoa mingine haijatoa mawaziri kabisa.
 
Hivi ni sharti kila rais akiingia madarakani Mawaziri, RCs na DCs lazima wawe ni watu wale wale wa miaka yote? Kwamba uteuzi lazima uteue watu waliowahi kuwa mawaziri hata kama walitoka baadae kwa ufisadi, ni sharti uchague kutoa hao ama kuwa badirisha tu hao hao. Maana miaka yote majina ni yale yale tu
Hiyo inaonakana ndo kawaida ya viongozi wetu. Maana hata JPM alikuwa anaweza mtumbua mtu na baadae akamrudisha tena. Ona kwa Simbachawene, Nchemba n.k.
 
System imeshakufa mtu anampangia njama Rais kipindi u makamu leo unamrudisha unataka tuseme ulikua kwenye NJAMA ... vetting gani mtu kama MAKAMBA ANAWEZA PITA KAMA sio Tz na UGANDA tu dunia nzima.
Mkuu ni lipi baya la Makamba linalomfanya awe hafai kurudi katika nafasi ya uwaziri ?

Maana kama kuondoka na kurudi barazani, watu wengi tu huwa wanafanya hivyo na mifano ipo.
1. Mwigulu Nchemba
2. George Simbachawene
3. Faustine Ndugulie n.k n.k

Kipi haswa mnakiona kwa January ?
 
JANUARY MAKAMBA alishaingizwa kwenye system na kuonekana ni Mpiga dili, bado anarudishwa tena.

Ataenda kuiba pesa nyingi ili aje kugombea Urais kama ilivyo ndoto yake
Kutaka kugombea urais hapo baadae (kwa mwanasiasa) haliwezi kuwa ni kosa.

Kuiba fedha za umma ni kosa kubwa sana (kwa mtu yeyote yule, sio lazima awe kiongozi au awe mwanasiasa). Sasa swali ni je, January aliiba nini, wapi na lini ?

Isaidie nchi uipendayo kwa kufichua wizi (sio sawa kutoa tuhuma za jumla jumla zisizokua na uthibitisho).
 
Kukopa 1b ktk mifuko ya jamii
Kuna mambo mawili,
1. Ni lazima iwe ni kosa kukopa kwenye mifuko ya jamii.
2. Ni lazima iwe ni kweli unayemtaja alifanya hicho ulichokisema kafanya.

Je, una hakika hayo mawili hapo juu ni kweli kwa Mh. Makamba au ni tuhuma za jumla zisizo na uthibitisho ?
 
Kuhusu January umesema kweli kweliiii kweliiiii 1000%.

Uwezo wa January ni mdogo mdogo sanaaa, he has no potential kabisa, as you said, nguvu kubwa imetumika kumweka January katika baraza la Mawaziri, ili alinde maslahi ya akina JK ya mafuta, Lake Oil and Lake Gas, pia Maslahi ya Rostam katika Gas, Taifa Gas and Mihan.

Sitegemei kama atadumu muda mrefu katika hii wizara ya Nishati, sbb kashfa ya rushwa au mikataba mibovu atakayoingia baadae au sera mbovu atakazopendekeza baadae kwa kulazimisha au upendeleo wa walimweka utadhihirika mapema na itamuondoa haraka, huwa sikoseagi kubashiri, hasa pia kikubwa kitakacho muondoa ni kutaka kugombea nafasi ya Urais hapo mbeleni, sbb ataanza makundi na mikakati mapema ili agombee, hapo CCM itamkata haraka.
 
Kuna mambo mawili,
1. Ni lazima iwe ni kosa kukopa kwenye mifuko ya jamii.
2. Ni lazima iwe ni kweli unayemtaja alifanya hicho ulichokisema kafanya.

Je, una hakika hayo mawili hapo juu ni kweli kwa Mh. Makamba au ni tuhuma za jumla zisizo na uthibitisho ?
Kwani wewe unaweza kukopeshwa na mifuko ya jamii pamoja na kuwa unaweza kuwa mwanachama
 
Japokuwa Rais hapangiwi nani wa kuwateua katika nafasi mbalimbali, lakini ni sahihi wizara isiyo ya Muungano kupangiwa watu kutoka upande wa pili wa Muungano.Pili ni sahihi mkoa mmoja kuwa na mawaziri watatu, kutoka kwenye majimbo, wakati mikoa mingine haijatoa mawaziri kabisa.
Unaposema WIZARA ISIYO YA MUUNGANO unamaanisha nini ?

Unamaanisha wizara yoyote ile nje na wizara ya muungano na mazingira ?

Ninachofahamu mimi kuna mambo ya muungano na mambo yasiyokua ya muungano, hakuna kitu inaitwa ''wizara za muungano" na "wizara zisizokua za muungano" hivyo tugawane uongozi wa wizara kutokana na nani anatoka upande upi wa JMT.

Labda unielimishe tena kwa mifano kwamba mtu kutoka Unguja au Pemba ni marufuku kuongoza wizara ABC....

Mtu anayetokea Pangani, Tarime au Mafinga ni marufuku kuongoza wizara XYZ....
 
Kwani wewe unaweza kukopeshwa na mifuko ya jamii pamoja na kuwa unaweza kuwa mwanachama
Ningependa sana unijibu mkuu. Ila kama umeamua mjadala uwe ni "swali kwa swali" basi sawa. Naishia hapo.
 
Kuhusu January umesema kweli kweliiii kweliiiii 1000%.

Uwezo wa January ni mdogo mdogo sanaaa, he has no potential kabisa, as you said, nguvu kubwa imetumika kumweka January katika baraza la Mawaziri, ili alinde maslahi ya akina JK ya mafuta, Lake Oil and Lake Gas, pia Maslahi ya Rostam katika Gas, Taifa Gas and Mihan.

Sitegemei kama atadumu muda mrefu katika hii wizara ya Nishati, sbb kashfa ya rushwa au mikataba mibovu atakayoingia baadae au sera mbovu atakazopendekeza baadae kwa kulazimisha au upendeleo wa walimweka utadhihirika mapema na itamuondoa haraka, huwa sikoseagi kubashiri, hasa pia kikubwa kitakacho muondoa ni kutaka kugombea nafasi ya Urais hapo mbeleni, sbb ataanza makundi na mikakati mapema ili agombee, hapo CCM itamkata haraka.

January amewekwa ili alinde maslahi ya akina JK na Rostam dhidi ya nani ?

Hayo maslahi yalikua yanalindwa na nani kabla January hajawa waziri wa nishati ?
 
Back
Top Bottom