Nini kimemkuta Waziri wa zamani na Wakili Msomi, Lawrence Masha hadi kufika kwa “Kiboko ya Wachawi”?

Kufiriaika kubaya.
Amekata tamaa anazidai kuibiwa na matapeli manabii
Mimi ndiyo maana nikimuona mtu anaenda kwa hao wapigaji wala sihangaiki nae kumzuia maana huwa kwa uwezo wake wa kutambua vitu aliopewa anakuwa amefika mwisho kifikra so nachofanya namuacha aendelee kujifunza in hard way

Kwa msomi level ya huyu jamaa kufikia kwenda Buza huko ndani ndani kwenye banda la mabati kwa so called mtume kutabiriwa unaweza ukaona jinsi maisha yakimpiga mtu yanavyoondoa ufahamu wake.
 
Hata mgombane vipi mke na mume nashauri kutaka kuuana aisee hapana.
Dunia haina Siri .
Watoto na wazazi I na ndugu wa Inayets la kumuua wakijua inategemea utaishia vipi ?

Siku hizi kuna wanawake kuishi single parent au maisha ya ujane hawaoni shida ilimradi kama amefanya maarifa kwa Mwanaume ako na kibanda kinampa Hela za kujikimu.
Fikiria upendo umepotea kiasi hicho kweli kwenye mioyo ya watu?

Wanaume wengi tu wanaliwa timing. 😆😆
 
Daah! Hawa manabii hawa!
 
Kwa video hiyo, nilikuwa nimeanza kuingia kwenye reli ya kumuamini bwana nabii, kiboko ya uchawi... Mpaka hapo mwishoni aliposema kuwa kumbe wamekwishazungumza ofisini.... Nilijua hawajuani na hawajaonana kabisa... Tunapigwa mazee, tunapigwa!!
Wengi sana mtaumia kwa kuwasikiliza hao wendawazimu,wewe umestuka yupo mwenzako yupo Misungwi huko kesho anaenda kuuza mifugo mnadani apate nauli ya kufika Buza kumuona mtume wa wachawi.

Usisahau kabla hujaingia kumuona una-sign contract ya Tsh 200,000/= ili kwamba utabiri uliotegemea atakupa ukienda mrama usimsumbue,in short jamaa ana-behave kama kalumanzila.
 
Tatizo ni kama Kasema uongo lakini kama iwapo alichosema ni ukweli ni afadhali kwa Lawrence itampa kuchukua tahadhari.

Awareness is empowering.

Nabii ni kama mkwezi tu lakini nazi imeliwa na mwezi ( mtesi )👌
 
Kusoma saaana SIYO kuelimika, bali kuelimika ni kuongeza maarifa. Waziri mstaafu na Nabii wake wote wajinga!
 
Kuna uzi uliletwa leo na mdau mmoja kuhusu jamaa huko kenya aliyeua wanae, mkewe na kisha yeye kujiua kwa kuwa alikuwa ana mambo haya haya ya kushirikiana na manabii uchwara.

Kisha akaingizwa kingi na mali zake kutaifishwa.

Religion is the drug, religious leaders are the dealers their followers are the addicts.

Waathirika wa imani uchwara hawana tofauti na waathirika wa madawa ya kulevya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…