Nini njia ya kukomesha wizi huu majumbani?

Nini njia ya kukomesha wizi huu majumbani?

Niende moja kwa moja kwenye mada kama maeneo nayoishi kumekuwa na vitendo vya wizi mchana na usiku ila style wanayotumia wizi ni kama aina mpya flani kwani kama miezi miwili kuna wezi walivamia usiku kwenye duka la vifaa vya ujenzi na kuiba bila kuvunja grill yaani walifungua kufuli kama kwao vile.

Juzi tena kuna jirani mchana ametoka amefunga mlango pamoja na grill jamaa wakaenda wakafungua kama kwao na kubeba kila kitu walichotamani kubeba.

Usiku wa leo jamaa wameenda tena mtaa wa jirani wakafungua mlango bila kuvunja wakabeba Tv ,simu pamoja na pesa japo kwa maelezo yake anahisi walimpulizia dawa za kulala .

Hatua ya kwanza tumechukua ni kuaza kulala na majaba au mabeseni ya maji chumbani kwani inasemekana hata wakikupulizia dawa ya kulala haifanyi kazi (hatuna uhakika).
Ila kinachotupa shida wanawezaje kufungua milango na magrill bila kufunja wanatumia njia gani na njia gani ya kuweza kudhibiti wizi huu wa majumbani?
Pamoja na kulala na hayo, majaba ya Maji, pia nyunyuzia ugolo, madirishani kwa nje. Maana kabla ya kukupulizia hiyo dawa, lazima vichwa vyao viwe karibu na dirisha, ili kukuchungulia.

pua yake itaikaribia ugolo, na watapiga chafya za kutosha, hizo kelele za chafya za zitawakimbiza, maana mwizi hapigi kelele.
Hivyo watashindwa kuendelea na dhamira yao kwa kelele wanazo piga wenyewe.
 
Tatizo la hizi adhabu za papo kwa papo ni namna ya kuthibitisha kama mnayemuua ndiye haswa ni Mwizi.

Mnaweza kukurupusha Wezi wakasepa alafu mkakutana na Jamaa katoka kwenye shughuli zake wala ahusiki na Wananchi tayari mihemuko ipo juu unafikiri atapona?.
Nilimpoteza jamaa yangu kwa style hiyo Mkuu,

Sitaki Kukumbuka Ile siku, Bado lile tukio linanitesa Hadi kesho.

TooBad .
Mungu ampumzishe rafiki huko aliko. Alikuwa mtu mwema mno.
 
Mtunze funguo zenu vizuri, anaugandamiza kwenye sabuni na kwenda kutoa ufunguo kama wako bila kujijua.

Sent using Jamii Forums mobile app
KIwa maelezo ya Mleta uzi sidhani kama ni aina ya Wezi wa kupitia hizo tabu zote.

Hawa ni kama tayari wana mbinu mbadala ya ku dili na aina tofauti za kofuli...inabidi Raia nao waje na mbinu mbadala ya kufunga Nyumba na Fremu zao.
 
Nina rafiki majambazi wezi sijui, walipofika nyumbani kwake, waka wanahangaika na mlango wa jikoni, hapo mlinzi walishampiga mapanga, R.I.P alifariki, rafiki akawa bize kupigia simu majirani, katika purukushani, mmoja wao wale wezi, akawaambia wenzake, siyo mlango huu ni ule mlango wa Mbele, wakaenda mlango wa Mbele, wanajua walichofanya, Ila mlango ulifunguka fasta Tu, wakaingia, wakakomba walivyoweza, DK 10 nyingi, majirani wakawa wameshaamshana, mmoja alikuwa na silaha akaipiga juu, wezi wakakimbia!

Nahisi wakati wa ujenzi. Kuna Kikundi cha mafundi au someone kwenye shughuli nzima anayewapa ramani!

Mpaka kesho hatukujua nini, Ila walibadili milango, na locks na makomeo yakaongezeka!
 
Halafu wakichomwa moto watetezi wanaibuka msijichukulie Sheria mkononi, hali yenyewe ngumu halafu mtu anakusafisha
Umenikumbusha Kuna mzee kitaa kakatazwa kupiga mwizi [emoji2]. Hata wapigaji mnatetemeka huwa anawapasua mapumbu linawekwa kwenye jiwe au mbao na ngozi lake alafu jiwe moja anashakilia yeye

Kila mtu lazima ushijike chini hakuna mwenye roho ya kuangalia

Kuna watu wana roho ngumu
 
Thank me later.
1C9006A3-F291-4A82-94D3-A315E41B0B56.jpeg
1C9006A3-F291-4A82-94D3-A315E41B0B56.jpeg
4304E736-2775-43F0-ABAC-6151536F7A11.jpeg
BE38C513-492D-4B56-BAFE-0BB88A12DD33.jpeg
7593DDA6-B115-4BE0-B818-313DDEA15434.jpeg
 
Ni sawa wanaiba ILA HILI la kuwapa napanga na kuwachoma moto sio zuri mkimkamata pelekeni mahala husika sio kujichukulia sheria mkonon
 
Akili kisoda tu zina mtazamo huu, dogo aliibiwa kwa style hiyohiyo 2018. Huyo JPM akiwa rais, muacheni Mzee wa watu apumzike mnajifanya mnamkumbuka katika issues za kijinga kama hizi zisizo na ukweli. Mnatupandisha hasira tu, tunaishia mtukana tu marehemu.

Muacheni Mzee apumzike
Matukio yamezidi kuongezeka sasa hivi ukilinganisha na wakati huo. Jitahidi kuelewa.
 
Back
Top Bottom