Nipo ugenini, wanapika chakula kidogo mno

Nipo ugenini, wanapika chakula kidogo mno

Mwaka jana kuna project nilienda kufanya mkoa fulani hivi ya kama wik mbili nilipofika nikapokelewa na mwenyeji wangu. Basi baada ya stori mbili tatu nikamwambia anipeleke Lodge nzuri. Jamaa akaniambia Lodge ya nini wakati home kwake kuna chumba cha wageni. Nikakataa lkn jamaa akasisitiza niende nikaona isiwe case. Nikajiongeza tukapitia kwa mangi nikafungasha haswa vitu vya ndani mamichele,unga wa ngano mafuta,tambi na mazaga zaga kibao nikamuuliza kama ana frigi akasema anayo tukapitia na buchani kununua nyama na masoseji. Basi tukafika home tukapokelewa na mke wake na watoto wake wanne wawili wa kike wawili wa kiume. Kesho yake nikaanza mishe. Yaani wale watu ni wakarimu ajabu. Shemeji kila asubuhi baada ya heavy breakfast kabla sijaondoka ananiuliza nikirudi nitapendelea kula nini,wale watoto wa kike asubuhi wananiambia niwatolee nguo chafu wafue. Mi ni Mkristo na wao ni Waislamu safi lkn awajawahi kunistrict kupiga mambo yetu yale. Tukienda bar na yule jamaa mi nakamatia vitu yeye anacharaza zake Redbull tukiondoka tunachukua nyama ya mbuzi kilo tunarudi home tunakula na familia yake fresh tuu. Siku ya kuondoka ilivyofika hakuna aliyekuwa anataka niondoke na walihuzunika sana hadi kulia. Mpaka leo ni kama ndugu zangu kabisa wananitembelea na familia yangu huwa tunafunga safari kwenda kuwatembelea. Sorry kwa uandishi mbovu.
God bless
 
Ugenini noma asee nilimtembelea jamaa angu asee yan chakula cha usiku wanakula saa tano usiku...

Siku ya kwanza nilijua labda jion hawali naona chele saa tatu tatu ndio linachambuliwa mama anawasha moto
Haha au walikua wanasubiri ulale
 
Ukweli au niseme nilivyokuwa naona nyumbani. Mara nyingi watu wa Dar hawali sana kama wapo ni wachache sana ambai watakuja kwako na njaa ya tangu asubuhi au ya tangu mchana akiwa anakuja jioni.

Sasa kwa watu wa kijijini au mazingira ya kijijini ni tofauti. Mtu wa kijijini kutokunywa chai ni kawaida ila mchana atakula sana na jioni atakula sana. Mjini mtu akija kukutembelea anaweza akiwa njiani akanywa soda, akala keki nk.

Lakini mtu wa kijijini hawezi kufanya matumizi madogomadogo ya chakula hii inawafanya kutegemea msosi wa mezani. Pia kazi wanazofanya zinawafanya wale sana na wala waspate mavitambi yenu ya mjini.

Nyumbani nilikuwa naona akija mgeni kutoka kijijini mama anahusika ktk kuwawekea chakula yeye mwenyewe Tena alikuwa anawawekea kila mtu ktk sahani yake. Alikuwa hawaamini watoto wake wa kike.

Hii ni moja ya sababu iliyomfanya apendwe na apokee wageni wengi kutoka kijijini kwao.
 
Mkuu mm nimekulia mjini ni mwembamba sana ila ninakula sana, mkate mzima nafuta, chapati nakula NNE kwa kujibana sana, Kuna mgahawa Fulani nakulaga mchana chakula ni expensive ila wananifahamu nauziwa plate mbili za wali au pilau kwa bei ya plate moja ugali nakula plate mbili ndo nishibe, wanaiita msukuma, nameza dawa za minyoo kila mwezi lakini kula kupo palepale, cha ajabu sinenepi hata kidogo nazidi kukonda mpaka najiuliza chakula ninachokula kinaendaga wapi?, mwaka 2012 nilihudhuria semina flan ya mambo HIV njombe wakati wa msosi niliweka mlima wa wali na viazi ndizi Kuna wazungu wakawa wanabishana kama nitamaliza nikasema moyoni hawa hawanijui, nilifuta plate nikanyanyuka nikaongeza plate ya pili nikafuta nikala matunda na maji juu, hahahaha

Eee we kiboko [emoji23][emoji23][emoji23] sasa ukienda ugenin unafanyaje?unaigiza au unakula share za watu watatu huo uroho sasa
 
Anaweza kula ubuyu na maji akalala.
Ukikaa nao sana karibu au ukashare rrom na mpare anaweza kukuambukiza ubahiri. Shida ubahiri wao unaenda mpka ktk kula hapo tu

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nasikia hawaungi mboga
 
Hayo ndo maisha ya daslam🤣🤣njaa tupu,watu wanakula kuepuka kufa sio kushiba,life gumu sana daslam
 
Kweli kabisa,tatizo maisha ya daslam ni magumu sana,wengi nanaexist hawaishi 🤔
Nyumba yenye furaha ni yenye chakula cha kusaza. Sasa unakuta watu wanapika wali kwenye sufuria za kuchemshia chai! Kweli!!? Unakula hata ukienda toi unatoa kama mbuzi au mtoto!! Nyumba isiyo na chakula cha kutosha haina furaha hata kidogo.
 
Mimi nikienda Shy kutembelea ndugu hua wananiuliza kwanini nakula kwa kuogopa? (hapo utakuta nimejilazimisha kula karibu mara 2 ya kawaida ya uwezo wa tumbo langu)
Watu wa vijijini wanakula share kubwa kuliko wa town nahisi.
 
Kuna siku nilikuwa na wageni Fulani watasha sehemu Fulani, wao wanakula Kidogo sana, Mimi nikamsoma dereva maana mswahili mwenzangu, yeye anajifanya anazuga alafu anaaga anaenda kufata vocha aloo Kumbe anaenda kwenye mgahawa wa karibu na kupiga mapigo ya kibongo. Niliunga tela fasta siku inayofata nikamwambia na Mimi nataka nitume M-pesa sehemu akaniambia njiani asee Mimi huwa sishibi hiyo misosi nikamwambia sio peke yako, alicheka sana. Nikaagiza ugali sahani mbili chap, dereva alicheka sana. Hii ndio mipango. [emoji23][emoji23][emoji23]
[emoji23][emoji23]

Sent from my SM-A115F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom