korino
JF-Expert Member
- Dec 6, 2011
- 1,004
- 666
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ahsante!Katika mahusiano haya mnaonekana ni wawili msioendana hasa ukizingatia kwamba wewe ni mchanga wa bahari na yeye ni Upepo wa kimbunga;
Unaonaje dhoruba ikitokea kando ya bahari?
Hayo ndio mahusiano yenu yalivyo mkiunganisha roho,
Wewe utajikuta unamuona yeye ni mtu usiyeweza kumtabiri, na yeye atajikuta ni mtu ambaye anashindwa kwenda na wewe kirahisi hadi atumie nguvu nyingi,
Mbinu zako za kawaida tu za kumuendea hata katika kuomba mchezo utakuta kwake ni kero kubwa sana na atakuona kama vile muda wote wewe ni mwenye kumtibua tu mwanzoni utaona kama anakuvumilia lakini baadae sura kamili ya dhoruba itaonekana.
Yeye hujiamini katika kujieleza kimtizamo wake bila maneno.
Na wewe hujiamini katika kujiheshimu bila mipaka, mawasiliano yenu kila mmoja atajikuta haeleweki kwa mwenzie na pia ataona kama anaaibika na kudhalilika kwa mwenzie.
Yeye utakuta ni mtu wa kupenda mitoko na wewe utakuta ni mtu wa kupenda mtu mwenye kumaintain maisha ya nyumbani huyu ni mtu mtafutaji wewe utafurahishwa kwa utafutaji wake mwanzo kwa kufuata mkumbo lakini baadae itakuwa too much hata kama atakuletea maigizo sasa hivi lakini baadae visafari vya kwa ndugu jamaa na marafiki huwa havikatiki.
Yeye alivyompenda uhuru safari ya mapenzi yenu itakuwa ngumu sana na uvumilivu wake kwako ni mdogo huyu anataka mtu mwenye nyota ya moto wa mkaa ambaye yeye akimletea habari za kutoka anakuwa kama kamtia ny*ge. Hakika kipenzi chako hiki ni chenye kupenda kutoka sasa ukimfungia ndani kwa maisha yako ya siasa kali kimbunga kitazunguka kisha vumbi lako litapeperuka na kubaki umechafuka tu.
Nyie mnapendeza zaidi kuwa ni wenye urafiki tu na hata mapenzi yenu mara nyingi huishia kirafiki tu.
Rakims
Ipo hivi kwa mtizamo wewe ni mwenye asili ya mchanga wa bahari na yeye ni moto wa nyasi kwa haraka tu hapa mnakuwa hamuendani mkuu kwa maana mpo tofauti sana kwa maana;- wewe unaonekana ni mwenye kufurahiwa sana na yeye kwa kipindi cha awali na yeye utamuona ni mwenye matumaini makubwa lakini vile vile yeye mtizamo wake kwako anakuona ni sawa na mtu aliyejitosheleza lakini nyote kwa pamoja kwenye mahusiano yenu mapema sana utaanza kukasirishwa na matakwa yake ya uhuru bila masharti.Mkuu Mimi ni mwanamke tarehe yangu ni
26/12
Me tarehe 11/12
Naomba nichambulie huyu mwanaume
Pole sana mkuu.😃😃Ubishi Ubishi tumeachana siku ya 3 leo atuwasiliani afu Jambo ata halieleweki...mi gari lishawaka Ni swala la muda tu hatoamini macho ake..nimekubali kushika mengine
Kuhusu watoto mungu tu asaidie makeeeeeee🤐🤐nlikua sjapanga kabisa kuzaa watoto na mama tofauti Ila ndo hivyo tena... nothing guaranteed forever!
Mahusiano haya ni baina ya maji ya moto na upepo wa kimbunga hii ni fahari wawili hawakai zizi moja na pia hawa ni wagomvi wawili walio kubaliana kila mmoja akae upande wake wa dunia,
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Mahusiano haya ni baina ya maji ya moto na upepo wa kimbunga hii ni fahari wawili hawakai zizi moja na pia hawa ni wagomvi wawili walio kubaliana kila mmoja akae upande wake wa dunia,
Mahusiano yenu yapo hivi:
Wewe utakuta ni mwenye kuwa na matakwa mazito ya kihisia, lakini yeye hata kuruka nae mara moja sio jambo zito kwake kwa upande wako yaani kumvulia nguo kwako yeye kwake ni jambo la kawaida wala halina uzito wowote katika hisia zake, kwake yeye wewe kukutana nae kimwili ni kama tu kupanua upeo wake wa yeye kukujua zaidi wala sio jambo la ajabu na kumfanya ajihisi yupo kwenye serious relationship.
Wewe ni mtu ambaye hutaweza kuvumilia jinsi yeye atakavyo kuwa anachukulia mapenzi yako kirahisi rahisi.
na kila mara unaweza kuwa na hisia kwamba hayupo serious na wewe isipokuwa ni part time tu.
Yeye binafsi ni mtu ambaye ni mwenye kuvutiwa zaidi na vya nje hata hivyo vya nje akiingiza ndani bado atavutiwa na vya nje tu hata ukiwa kwenye ndoa nae huyu hashindwi siku moja kukwambia umalaya upo kwenye damu you deal with it or leave it.
Japo akimpata anaemmudu kinyota huwa mpole kama kondoo.
Kitu ambacho wewe kitakutia wivu wa ajabu na vile una asili ya wivu, basi utataka kujaribu kumtawala na utakuta kila mara anakuvuruga jinsi anavyopenda uhuru na alivyo na mood za kuswing basi safari yenu itakuwa ngumu.
Wewe utakuta ni mwenye kupenda kuwa nyumbani na yeye utakuta ni mwenye kupenda uhuru wa kuendelea hadi mwisho kila mtu atashika njia yake.
Mkilazimisha nyie ni mtu na jamaa yake wasioelewana wanaochangia nyumba kulipia kodi.
Rakims
Mahusiano haya ni baina ya moto wa nyasi kwa moto wa nyasi moja kwa moja unaweza kusema ni mfano watoto mapacha yaani wenye kufanana sana.
Lakini hata hivyo ukirejea mwanzo nilishaelezea kuwa hata nyota zenye kufanana huwa zina mushkeli yake.
Baadhi ya wanajimu huamini kwamba mwenye kuweza kumtosheleza Mwenye nyota sawa na nyota hii yako ni pacha wake lakini kwa uzoefu na elimu pamoja na experience nilionayo katika unajimu hapana hii pekee haitoshi bila kuwa na marekebisho.
Imagine mnaishi na mtu mnafanana kila kitu?
Mapenzi yenu yatakuwa lakini lazima tu kuna migongano,
Moja kwa moja twende kwenye uchambuzi wako:
Nyote wawili mnaonekana ni wenye kupenda maendeleo na wenye kuendana sana mwanzoni karibu kila kitu chenu, wenye kupenda kutoka toka na kuroam, japo kuwa ni jambo zuri kwenu machafuko, uhusiano wa matukio yasiyotabirika wala kufikirika huja kwa kushangaza sana.
mnaonekana hata kwenye macho ya watu ni wenye kuendana na kupendezana sana.
Lakini ni kawaida sana kwenu kila mmoja wenu kumletea majanga mwenzie, Kila mmoja kati yenu anakuwa sio mwenye kujitolea kwa mwenzie kwa udhati na mnakuwa nyote wawili ni wenye kupenda kuchakatia nje,
Pair yenu huwa inaokolewa sana na imani ya dini hasa ukizingatia nyota yenu inatawala sana elimu ya dini na vilevile akili ya kiimani zaidi lakini kwa Sagitarians ambao hawana dini katika nyoyo zao utakuta mwanaume anachakatia huku na mwanamke kule.
Mkikutana kila mmoja anaweza kumlia mwenzie yamini kwamba hana hayo mambo lakini pale zinapoanza kuingia mimba za ghafla na kuletewa watoto usio wajua ndio unakumbuka kumbe naishi na jini mwenye miguu miwili.
Wote kati yenu mnatabia ya kumsukuma mwenzie katika kufanya mambo maovu mnapokuwa mnakwazana anaweza kukuboost na kukwambia katembeze nje sibabaiki na wewe ukajaa kweli,
Ni nyota moja ya mahusiano ikiwa na msimamo na imani basi dunia nzima huona kama ya kwao lakini otherwise ni wachezaji wazuri tu wa nje furaha ikiisha ndani.
Rakims
Katika mahusiano haya wewe ni maji ya bahari yaani kaa hivyo unahitajika kuzoea hali ya yeye moto wa mkaa katika mitoko kutoka toka, uchangamfu. kitofauti,vinginevyo, ukarimu wake, uridhie moyo wake wa kujitolea katika kusaidia,


Sawa mkuu kwa mtizamo unaonekana ni mtu mwenye mwenendo wa upepo wa kimbunga na yeye ni mchanga mwekundu kwa mtizamo huu tu ni watu ambao hamuendani lakini nitakufafanulia hapa kwa ziada maana mnaendana kwa asilimia 30 tu na tofauti na hii na mkuu aliye pita hapo nyuma ni vile yeye alikuwa kinyume chenu yani yeye alikuwa katika asili ya kinyume cha yako hivyo inakuwa hivi;-Mimi ni Ke
Ke: 22/02 - A
Me: 26/08 - E