Nitajieni biashara nyingine inayotoa faida kama mikopo ya kausha damu!

Nitajieni biashara nyingine inayotoa faida kama mikopo ya kausha damu!

Kausha damu: Unawekeza mtaji wa shilingi 1,000,000, unavuna faida ya shilingi 300,000 mpaka 400,000 kwa mwezi. Nitajieni biashara nyingine kama hii.

Tunaposema hii mikopo ni kausha damu na initia watu umasikini, basi hicho ndicho kinachofanyika.

Hivi leo hii ukipewa mtaji wa shilingi 1000,000 unaweza kufanya biashara gani halali ukapata faida kama hiyo ndani ya siku 30 tena ukiwa umetulia tu unahesabu siku? Hiyo ni riba ya asilimia 30 mpaka 40 kwa mwezi na Serikali ipo na Bunge lipo.

Hatumpendi Makonda, lakini saaa tumuombe amvae Waziri wa Fedha na Viongozi wa BOT maana hii biashara ni kama imewashinda kuidhibiti kwani Makonda kwa sasa ndio anasikilizwa na kujadiliwa kwa kila atachokisema.

Uzembe umezidi ndio maana Makonda anakuwa maarufu.
kama riba zao ni 30% -40% mbona kwa mtaji wa 1,000,000 FAIDA SIO 4,000,000 KAMA UNAVYOSEMA ?! Hesabu ulisoma wapi ndugu yangu yani 30% ya million moja ni million nne ?!
 
Kama benki zimeamua kuhudumia matajiri pekee na kuwakataa wauza chai mnawezaje kuiondoa kausha damu ?

Hela za mikopo ya halmashauri mnawanyima mnapeana mnataka waende wapi ?

Kwa mfano Hela zote za mikopo ya wajasiriamali na walemavu Temeke alipewa Mwenyekiti wa Wilaya wa ccm , na hakurejesha .

Peke yake alilamba mil 300 , ushahidi wote upo lakini kesi imezimwa
Kunywa bia popote ulipo .
Ukifika Mbeya mijini , tafadhali njoo Airport ya zamani karibu na gari ziendazo Tunduma utaikuta ofisi ya mikopo sitaji jina ila iko wazi utaiona , wambie wakupe milioni boss wao kasema maana una akili sana .
 
Kumbuka hiyo biashara inatambulika kwenye mamlaka husika. Hivyo ni biashara halali. Na utambue pia hizo taasisi hazimlazimishi mtu kukopa!! Na uzuri wapo wakopaji ambao wanalipa hayo marejesho ya 30% kila mwezi na hawajawahi kukimbia nyumba zao. Kwa sababu wanaitumia kwa malengi ya kibiashara! Na siyo kwa malengo ya kununulia sofa set au kukipia ada za watoto. Ila kwa hao wenzangu na mimi wanaoshindwa kurejesha, ndiyo hao sasa wanaodhalilishwa.

Kumbuka pia watu wanakopa kwa sababu serikali imeshindwa kuwatengezea mazingira mazuri ya kukopa fedha kwa riba ndogo, kutokana na sababu mbalimbali.
Lakini kubwa zaidi ufahamu hao watu wanakopa hela benki kwa ajili ya kuanzishia hiyo biashara. Na riba za benki nazo ziko juu! Asilimia 16+ siyo riba ndogo!

Na wakati huo huo wanatakiwa kulipa kodi za serikali na Halmashauri/miji, nk. Wanatakiwa kuwalipa wafanyakazi, kulipia pango la ofisi zao, nk.
Kwa hiyo mimi nashauri uanzishe kampeni ya kutoa elimu kwa hao wakopaji, ili watambue madhara ya hiyo mikopo ya kausha damu. Kinyume na hapo, hakutakuwa na namna nyingine yoyote ile. By the way, huyo Makonda ni kilaza tu na mtafuta kiki. Wala hana uwezo wa kuzuia mambo ambayo yapo kisheria.
Kwa nondo kama hizi kwanini nisikuheshimu mtani wangu .

Basi tu ni vile hautaki kunipa pumzi toka upate [emoji110]
 
Hiyo mikopo ikizuiliwa maskini ndio watakuwa wa kwanza kupiga kelele.
Maskini wa Tanzania hana pa kujikwamua zaidi ya huko kausha damu.
Kodi , malipo ya natibabu ya afya na misiba ndivyo vinawapeleka huko.
Ni heri kausha damu iendelee.
Nchi bila pesa mfukoni unafia kwenye korido za hospital tena ni hospital za umma
Kausha damu ziendelee
 
Kausha damu: Unawekeza mtaji wa shilingi 1,000,000, unavuna faida ya shilingi 300,000 mpaka 400,000 kwa mwezi. Nitajieni biashara nyingine kama hii.

Tunaposema hii mikopo ni kausha damu na initia watu umasikini, basi hicho ndicho kinachofanyika.

Hivi leo hii ukipewa mtaji wa shilingi 1000,000 unaweza kufanya biashara gani halali ukapata faida kama hiyo ndani ya siku 30 tena ukiwa umetulia tu unahesabu siku? Hiyo ni riba ya asilimia 30 mpaka 40 kwa mwezi na Serikali ipo na Bunge lipo.

Hatumpendi Makonda, lakini saaa tumuombe amvae Waziri wa Fedha na Viongozi wa BOT maana hii biashara ni kama imewashinda kuidhibiti kwani Makonda kwa sasa ndio anasikilizwa na kujadiliwa kwa kila atachokisema.

Uzembe umezidi ndio maana Makonda anakuwa maarufu.

Samahani mkuu.

Kausha damu ni sawa na loan sharking?

Na ni halali kabisa kwa sheria za bongo yetu?
 
Kama Riba ni kubwa kakope bank! Kwann uje kukopa kwangu si ni shida zako kwani Umelazimishwa Mkuu.

Binafsi nafanya hii biashara mwaka wa 8 huu riba yangu ilikua 20% kwa mwezi nimeshusha imekua 15% kwa mwezi.

Wabongo bwana yaani unaumia watu kukopeshwa.

Kwa mtu yoyote anaetaka kufanya hii biashara, ni biashara nzuri sana kikubwa uwe na wateja wazuri na uandae mikataba kisheria iliyokaa na ujisajili BOT
 
Kumbuka hiyo biashara inatambulika kwenye mamlaka husika. Hivyo ni biashara halali. Na utambue pia hizo taasisi hazimlazimishi mtu kukopa!! Na uzuri wapo wakopaji ambao wanalipa hayo marejesho ya 30% kila mwezi na hawajawahi kukimbia nyumba zao. Kwa sababu wanaitumia kwa malengi ya kibiashara! Na siyo kwa malengo ya kununulia sofa set au kukipia ada za watoto. Ila kwa hao wenzangu na mimi wanaoshindwa kurejesha, ndiyo hao sasa wanaodhalilishwa.

Kumbuka pia watu wanakopa kwa sababu serikali imeshindwa kuwatengezea mazingira mazuri ya kukopa fedha kwa riba ndogo, kutokana na sababu mbalimbali.
Lakini kubwa zaidi ufahamu hao watu wanakopa hela benki kwa ajili ya kuanzishia hiyo biashara. Na riba za benki nazo ziko juu! Asilimia 16+ siyo riba ndogo!

Na wakati huo huo wanatakiwa kulipa kodi za serikali na Halmashauri/miji, nk. Wanatakiwa kuwalipa wafanyakazi, kulipia pango la ofisi zao, nk.
Kwa hiyo mimi nashauri uanzishe kampeni ya kutoa elimu kwa hao wakopaji, ili watambue madhara ya hiyo mikopo ya kausha damu. Kinyume na hapo, hakutakuwa na namna nyingine yoyote ile. By the way, huyo Makonda ni kilaza tu na mtafuta kiki. Wala hana uwezo wa kuzuia mambo ambayo yapo kisheria.

Mkuu Heshima yako[emoji1545]
 
Pamoja na wizi kwenye hizo kampuni za mikopo lakini nadhani hapa Duniani sidhani kama kuna watu wajinga kama raia wa Tanzania.......

Bila shaka hao mabwana kabla ya kukupatia huo mkopo wanakufahamisha kupitia mkataba wao kwa maana mpaka unachukua mkopo maana yake ni khiyari yako......

Inakosa nguvu kwa kuwa ipo kwenye khiyari........
Tatizo umasikini mkuu. Ukishaona njia ya kupata hela na una shida hauwezi kukumbuka hayo mengine.
 
Kausha damu: Unawekeza mtaji wa shilingi 1,000,000, unavuna faida ya shilingi 300,000 mpaka 400,000 kwa mwezi. Nitajieni biashara nyingine kama hii.

Tunaposema hii mikopo ni kausha damu na initia watu umasikini, basi hicho ndicho kinachofanyika.

Hivi leo hii ukipewa mtaji wa shilingi 1000,000 unaweza kufanya biashara gani halali ukapata faida kama hiyo ndani ya siku 30 tena ukiwa umetulia tu unahesabu siku? Hiyo ni riba ya asilimia 30 mpaka 40 kwa mwezi na Serikali ipo na Bunge lipo.

Hatumpendi Makonda, lakini saaa tumuombe amvae Waziri wa Fedha na Viongozi wa BOT maana hii biashara ni kama imewashinda kuidhibiti kwani Makonda kwa sasa ndio anasikilizwa na kujadiliwa kwa kila atachokisema.

Uzembe umezidi ndio maana Makonda anakuwa maarufu.
Pesa haramu hizo...
Zinasafishwa.
 
Kausha damu wamewezaje ?
Wapo wakopaji wababaishaji na wengi wao ni wanawake. We unafikiri hao kausha damu wanakula faida tu kila siku? Nina ndugu mwanamke wa makamo tu ni mwaka wa 5 sasa hivi kesi na hao jamaa wa kausha damu haziishi. Kila tukimsaidia kulipa baada ya muda wanaibuka tena wengine wanaomdai wanampokonya simu au chochote chenye thamani.
 
Kama benki zimeamua kuhudumia matajiri pekee na kuwakataa wauza chai mnawezaje kuiondoa kausha damu ?

Hela za mikopo ya halmashauri mnawanyima mnapeana mnataka waende wapi ?

Kwa mfano Hela zote za mikopo ya wajasiriamali na walemavu Temeke alipewa Mwenyekiti wa Wilaya wa ccm , na hakurejesha .

Peke yake alilamba mil 300 , ushahidi wote upo lakini kesi imezimwa
CCM ndio kausha damu wenyewe
 
Back
Top Bottom