Nitakuwa wa mwisho kuamini kama Rais Samia ataendelea na Urais baada ya 2025

Nitakuwa wa mwisho kuamini kama Rais Samia ataendelea na Urais baada ya 2025

Ndugu zangu, Uraisi siyo kazi ya kitoto. Urais siyo lelemama. Hata Nyerere alilitambua hilo hadi akasema mtu anayetumia nguvu au fedha kuingia ikulu ni wa kuogopwa kama ukoma.

Tafasiri ya haraka haraka ni kwamba mpaka Dakika hii Samia nchi imeshamshinda, hakuna nchi ngumu kuongoza kama Tanzania ukizingatia ni Mzanzibar hata jiografia ya bara inampiga chenga.

Iko hivi, kuna maeneo watu wanajipigia bila uoga wala aibu kwa sababu wote ni wezi kuanzia TAKUKURU, Polisi hadi mawaziri Hakuna wa kumchunguza mwenzake. Huko kwenye halmashuri hali ya wizi ni mbaya sana.

Kikwete mwenyewe alishawahi kukiri. Nanukuu, "Nawaletea chuma hiki maana mlikuwa mnasema Mimi ni mpole, sasa anakuja mkali". Mwisho wa kunukuu.

Watanzania hawatakiwi kudekezwa utavuna mabua, nchi ilipokuwa imefikia kipindi cha kikwete Magufuli alikuwa hakwepeki that is why Hayati alipitishwa. Sawa?

Je, mlimsikia Mzee Makamba kipindi hicho? Nanukuu, "Huyu atawabatiza Kwa moto siyo maji tena" Walimtabua Kuwa alikuwa mtu sahihi kwa Watanzania.

Sasa nakuja kwa mama Samia ni hivi, Maza hana meno wahuni wa mjini wanamdhalilisha hajui afanye nini. Muda utafika wanachi hawatataka Hata kusikia jina lake.

Maana hawezi kubatiza Kwa moto wa siyo mkali, upole wake umezidi wa Kikwete. Kwa Mwenendo huu ubadhilifu wa kodi zetu kutumiwa na watu binafsi upo pale pale ndiyo maana kila kukichwa wanampaka mafuta kwa mgongo wa chupa.

Kama wewe unalipa Kodi PAYE, afu mwisho wa SIku unasikia watu wamepiga pesa afu wanaishia kusutwa tu badala ya kurudisha hela inauma sana. Aiseee tunafanyia KAZI watu. Mishahara yetu inakatwa kodi ili watu wale badala ya kuleta maendeleo.

Busara ilikuwa ni kukamilisha miaka 10 ya Awamu ya tano akae pembeni kwa heshima Tofauti na hapo atapata tabu sana. Pia kama taifa tutakuwa tumepata hasara kubwa mno.

Nawasilisha.
Kama wewe unalipa Kodi PAYE, afu mwisho wa SIku unasikia watu wamepiga pesa afu wanaishia kusutwa tu badala ya kurudisha hela inauma sana. Aiseee tunafanyia KAZI watu. Mishahara yetu inakatwa kodi ili watu wale badala ya kuleta maendeleo
[emoji115][emoji115][emoji115][emoji115]
Hiki kipengele kimenifikirisha sana
 
Umeelewa alicho sema.amesema ni bora kipindi cha JPM wizi ulikuwepo ndio ila sio kama wa kipindi hiki huu umezidi mzee
Hakuna tofauti hapo sema tofauti ya kipindi cha Magufuri na Samia ,ni kwamba Samia ni mtu anaye ukubali ukweli hata kama unauma na ndio maana ameruhusu mdhibiti wa serikali kuuweka hadharani wizi huo ,maana alikuwa na uwezo wa kumzuia asiuweke wazi na ww usinge ujua.

Lakini Magu alikuwa ni mtu asiye penda ukweli unao umiza na ndio maana alimtoa profesa Asad baada ya kufichua ubadhirifu wa matrion ya hela.
Nimacho maanisha ni kuwa kwa sasa una uona wizi kwasababu unafichuliwa, lakini kwa magu haukuonekana kwasababu ulikuwa unafichwa.
 
Siipendi CCM na sijawahi kuipa kura ila SSH nitampa kura yangu ya urais!! Ubunge nitampa upinzani,udiwani upinzani!! Huo ndio msimamo wangu!! Nitampigia debe mama mpaka kwenye walevi!!
 
Usijali mkuu hii dunia tunayoishi ni movie tu Wala sio halisi kwa hiyo usi panic, hii nchi ya Tanzania ndio scene ya ufisadi kwenye hiyo movie
 
Kama wewe unalipa Kodi PAYE, afu mwisho wa SIku unasikia watu wamepiga pesa afu wanaishia kusutwa tu badala ya kurudisha hela inauma sana. Aiseee tunafanyia KAZI watu. Mishahara yetu inakatwa kodi ili watu wale badala ya kuleta maendeleo
[emoji115][emoji115][emoji115][emoji115]
Hiki kipengele kimenifikirisha sana

Siyo kusutwa tu, hafukuzwi kazi japo anahamishiwa kitengo kingine aisee
 
Mbona kuna mengi tu yamefichwa ambayo yakiachiwa nchi itapasuka. Kuna pesa nyingi mno huyu mama ka,itoa nje ya utaratibu wa bunge na bajeti.

Mfano aliwalipa dowans billion 360 bila hata bunge kujua, amempa January Makamba trillion moja wanazosema wanaboresha mitambo ya tanesco ambapo Januari alisema zinatakiwa trilioni 4 ili kukamilisha zoezi.

Kuna pesa ambazo Nape alikiri wamewapa wenye maduka ya kubadilisha fedha kama kifuta machozi.

Kuna billions of shillings zimepigwa wakati wa zoezi la anuani ya makazi na hakuna chochote cha maana zaidi ya kuchukua mitipori na kupachika.

Huko NHIF alipo Makinda wamepotea ripoti sababu Makinda alimsifia sana Magu kiasi cha kuwabeza wanaomsema vibaya Magu ndio maana file lake limeachiwa.

Ndugu kila kitu kikiwekwa wazi tutakimbiana. Ikumbukwe mpaka sasa mama ameshakopa zaidi ya trilioni 20 ndani ya miaka miwili na mpaka sasa thamani ya vitu alivyofanya haifiki hata trilioni 7.
Kipindi cha jiwe ndio alikuwa akiiba hadi akashindwa kuajiri wafanyakazi na kuongeza mishahara

Samia anaajiri na kuongeza mishahara bado miradi ya jiwe aliyoianzisha kwa pupa
 
Hakuna kipindi ambacho hii nchi haijawahi kuibiwa, huyo jiwe mnaye sema sijui kipindi chake hakukuwa na wizi ndo kipindi akina makonda walimiliki majumba na magari kifahari yenye thamani ya mabilion ya pesa wakati wanapokea mshahara wa million 6 tu kwa mwezi.

Pia kipindi hicho cha jiwe ndo profesa Asad alifichua ubadhirifu wa trion 1.5 lakini jiwe akamshukia kama mwewe.

Miaka 6 ya jiwe hatukuwahi kuona fisadi yeyote akihukumiwa kwenda jera hali ya kuwa mafisadi yanajulikana.

Jiwe kitu ambacho alikifanya mpaka nikamkubali ni kukomesha tabia za uzembe makazini na kuanzisha baadhi ya miradi mikubwa ya kimkakati lakini kuja kunambia eti alidhibiti wizi hilo nakukatalia mpaka nakufa.
Habari imejikita zaidi kwa Samia we unajikita na jiwe.....akili za wapi hizi?
 
Umeelewa alicho sema.amesema ni bora kipindi cha JPM wizi ulikuwepo ndio ila sio kama wa kipindi hiki huu umezidi mzee
Kipindi cha jiwe 1.5 trilioni ilionekana kuibwa, wizi gani umefikia 1.5 t awamu hii?
 
Deep state ya Tanzania sijui ni akina Nani, ila mataifa yaliyomakini angestep down Kwa maslahi mapana ya taifa. kama Trump alivyofanyiwa USA.
Deep State ya Tz ingekuwa imelala ungekuta hadi leo nchi hii watu wanatekwa na miili yao kuokotwa
 
unakatwa PAYE??????.......kwani ajira zimetoka?????😀😀😀
 
Yaani mwizi anakuibia nyumbani kwako unamuona kisha unamuambia stupid wewe toka hapa tuache.
Magufuli aliwahi kumfunga nani kwenye wizi wa ripoti ya CAG? Au ripoti kipindi hicho kila kitu kilikuwa safi? 😂😂
 
Namuomba Raisi wangu mpendwa ampe rufaa huyu mgonjwa Tanzania anahitaji specialist sio daktar wa kawaida kama yeye aking'ang'ania mgonjwa atamfia mikononi mwake.
 
Kipindi cha jiwe ndio alikuwa akiiba hadi akashindwa kuajiri wafanyakazi na kuongeza mishahara

Samia anaajiri na kuongeza mishahara bado miradi ya jiwe aliyoianzisha kwa pupa
Lakini yeye haanzishi mradi mkubwa
 
Back
Top Bottom