Niulize chochote juu ya tiba za Mitishamba

Niulize chochote juu ya tiba za Mitishamba

Unatakiwa kupata mitishamba inayoweza kurudisha kuijenga misuli husika katika hali ya awali.Usipambane na dawa za kupaka uume zitakuua zaidi.Unatakiwa kunywa zitembee kwenye damu
Asante kwa majibu yako...vipi unanisaidiaje katika hili?
 
Tumia dawa meno inaitwa colget sensitive imechorwa jino na fizi ambayo upandw lina rangi ya dam! Kila unapopiga mswaki tumia bicabonet soda..kuumwa na jino u harufu mbaya ya mdomo utaisikia kwa jiran
Asante sana, Je bicabonet soda naitumia baada ya kupiga mswaki na naitmiaje na kwa kiasi gani?
 
Mitishamba inayotibu bawasili ipo ya aina mbalimbali,lakini majina yake huambatana na lugha ya eneo husika.Mhimu ni kuwa ili uweze kupona bawasili lazima upate dawa ya kunywa itakayopita kwenye utumbo mkubwa ambapo ndiyo viotea halisi vya nyama hutokea.Dawa ya kupaka husaidia tu kuondoa viotea vya nyama kwa wakati huo lakini haiwezi kusaidia wakati wote,kwa hiyo ili kumaliza tatizo kabisa lazima pia upate dawa ya kunywa.
Kwa nini dawa hiyo isitiwe moja kwa moja kwenye haja kubwa kunapo tatizo badala yake ipitie mdomoni mpaka tumboni ?
 
Kwa nini dawa hiyo isitiwe moja kwa moja kwenye haja kubwa kunapo tatizo badala yake ipitie mdomoni mpaka tumboni ?
Kumbuka kuna bawasili huwa haijatokeza ,inakuwa ndani kwenye puru ndo maana ya kunywa dawa huku ukipaka au kuweka nyingine sehemu husika!
 
Asante sana, Je bicabonet soda naitumia baada ya kupiga mswaki na naitmiaje na kwa kiasi gani?
Unaweza kuchanganya na dawa ya meno yaan unapotia dawa kwenye mswaki na yenyewe itie juu ya dawa unaswaki pamoja ila kwasabu bicabonet soda inakakamaza mswaki unaweza kuwa unaitumia peke yake na mswaki wake pale unapopata muda
 
Unaweza kuchanganya na dawa ya meno yaan unapotia dawa kwenye mswaki na yenyewe itie juu ya dawa unaswaki pamoja ila kwasabu bicabonet soda inakakamaza mswaki unaweza kuwa unaitumia peke yake na mswaki wake pale unapopata muda
Shukrani sana
 
Jambo watanzania wenzangu!!

Katika kubadilishana maarifa ninaomba kuulizwa chochote juu ya dawa asili za mimea na mitishamba katika kutibu magonjwa mbalimbali.

NB:Maswali hayo yasihusishe ramli na mambo ya kishirikina,ama mambo dhahania,maswali yajielekeze katika magonjwa ya kila siku ambayo tunaishi nayo na yanatusumbua.
Vp kuhusu mundende

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jambo watanzania wenzangu!!

Katika kubadilishana maarifa ninaomba kuulizwa chochote juu ya dawa asili za mimea na mitishamba katika kutibu magonjwa mbalimbali.

NB:Maswali hayo yasihusishe ramli na mambo ya kishirikina,ama mambo dhahania,maswali yajielekeze katika magonjwa ya kila siku ambayo tunaishi nayo na yanatusumbua.
Mkuu naomba ya usubi ama kwa mitishamba ama kitalaam yaan scientific
 
Katika kupunguza unene na uzito wa mwili,wengi wametumia njia mbalimbali bila mafanikio! Mfano kunywa maji vuguvugu yenye limao,kufanya mazoezi,kufunga kibana tumbo nk,njia hizo zimeshindwa kuwa na ufanisi na wanazidi kunenepeana tu.

Leo ninakuletea njia lishe (formula) ya kupunguza unene na uzito (kilo tano) kwa siku saba tu.

Siku ya 1: Asubuhi kula matunda,mchana chemsa kabichi weka chumvi kidogo na nyanya chemsha na upate supu; kula mchanganyiko huo na utajisikia umeshiba kabisa.Jioni kula tikitimaji na mbogamboga au kabichi kama ulivyotengeneza mchana.

Siku ya 2:Kula mboga za majani asubuhi (usile mboga za majani zenye wanga kama karoti).Mchana kula kabichi iliyochemshwa tengeneza na kachumbari,katika kabichi weka chumvi,pilipili na mafuta ya olive.Jioni unaweza kula mlo kama wa mchana,lakini unaweza kukaanga mboga nyingine za majani.

Siku ya 3:Kula mboga za majani na matunda,unaweza kuongeza kiazi kitamu kimoja.

Siku ya 4:Kula ndizi moja na unywe maziwa ya mtindi wakati wa asubuhi.Mchana kula kabichi kama ulivyotengeneza siku ya kwanza,usiku rudia mlo wa mchana.

Siku ya 5:Kula nyanya nne pamoja na samaki au kipande cha kuku asubuhi.Mchana unaweza kula samaki wa kuchemsha kiasi ambaye amechanganywa na nyanya.Wakati wa jioni unaweza kula chakula kama cha mchana.

Siku ya 6:Unaweza kula chakula cha protini na mboga za majani,anza kwa kula kachumbari asubuhi.Mchana kula tambi kiasi na kipande kidogo cha samaki.Usiku tengeneza supu ya kabichi.

Siku ya 7: Anza kwa matunda na juisi.Mchana kula mboga za majani na usiku kula supu ya kabichi na kiazi kimoja.

KUMBUKA:

Unatakiwa kunywa maji angalau glasi nne kila siku.

Unapomaliza dayati ya kwanza,unapaswa kupumzika wiki moja huku ukitumia vyakula ambavyo havikuongezei tena uzito.

Utaendelea tena na dayati hiyo wiki tatu mpaka pale utakapofikia uzito unaouhitaji.

Wasalaam!!
 
Back
Top Bottom