Chibule
Senior Member
- Sep 25, 2024
- 171
- 230
- Thread starter
- #241
1. Dawa ya kawaida
Faida: Inaimarisha meno na kuzuia yasitoboke/kuoza.
Watumiaji Hii inafaa kwa mtu yeyote na muhimu zaidi kwa wale ambao wapo kwenye hatari ya kuoza/kutoboka meno.
2. Dawa ya Kung'arisha meno
Faida: Kung'arisha meno.
3. Dawa ya meno kwaajili ya ganzi kwenye meno /Sensitivity Toothpaste
Faida: Inapunguza hali ya kupata ganzi kwenye meno hasa wakati wa kunywa au kula vitu baridi au vya moto.
Watumiaji: Watu ambao wanapata ganzi kwenye meno, mfano watu ambao meno yao yamelika kuta za pembeni au juu , wanaosaga meno usiku, na watu ambao fizi zao zimelika kiasi kwamba mizizi ya meno inaweza kuonekana .
4. Dawa ya meno ya watoto
Faida: Dawa hizi zinakuwa na kiwango cha madini ya floridi kinachofaa kwa watoto, lakini pia huwa na ladha na muonekano ambao huwavutia watoto kusafisha vinywa na meno yao. Kumbuka hauhitaji kiwango kikubwa cha dawa ya meno. Watu wazima na watoto kuanzia umri wa miaka
6: Saizi ya punje ya njegere.
Watoto wenye umri wa chini ya miaka 6 Saizi ya punje ya mchele.
Kuchagua dawa na kuitumia kiusahihi ni muhimu sana katika kulinda afya ya kinywa chako. Kutokana na kuwepo kwa dawa nyingi sokoni, hakikisha dawa yako ina madini ya floridi, na hakikisha imethibitishwa na shirika la viwango la Tanzania (TBS).
pia Iwe imeandikwa kiwango cha Fluoride 1450- 1500Ppm kwenye box lake.
Muone daktari wa afya ya kinywa na meno kwa msaada zaidi, ,iwapo Unachangamoto za kinywa na meno Unaweza wasiliana nami