Watu bado wapo ila saport ilikua chini tu,kuna watu kama akina Mwina,Mudy Jongo, Division Hadji,Amani Stereo,Mudy black,Mudy wa Shamba,Amadi Kiedu,Ally Chande "Dog",akina Machupa kule Bagamoyo na watu lundo tu.Lakini tushukuru E-Fm wameanza kuusaport.ni kweli mkuu..ila wote ni marehemu kwa sasa na wameondoka na mchiriku ndio kwisha habari yake!
amadi kiedu alikuwa 7 sasa wana kundi lao na mudy black....though muddy blacki alikuwa mpiga keyboard hatari, yuko wapi piloti baba isayaa?Watu bado wapo ila saport ilikua chini tu,kuna watu kama akina Mwina,Mudy Jongo, Division Hadji,Amani Stereo,Mudy black,Mudy wa Shamba,Amadi Kiedu,Ally Chande "Dog",akina Machupa kule Bagamoyo na watu lundo tu.Lakini tushukuru E-Fm wameanza kuusaport.
Pamoja mdau nafikili kiu yg niupate huo wimbo mengine yatajili mdauKama bado una vitu unvyohitaji kuvijua/kuuliza kuhusu mnanda uwanja ni wetu mdau.Tujimwage ili tujuane na kuunda mtandao wa kuuenzi mziki huu.
Kwanini kwenye ngoma ya mnanda wanapendelea kuvaa sharti na busta nyeupe na Sisi na viatu vyeupe??Wana jamvi,mimi ni mdau mkubwa wa mziki wa mchiriku/mnanda.Mziki ambao ulitawala na kujizolea umaarufu mkubwa kwenye miaka ya 90 hadi 2000,binafsi nimekulia kwenye jamii yenye kuhusudu mziki huo na hivyo kifuani kwangu nina hazina ya kutosha kuhusu mziki huo hatua kwa hatua tangu ulipotokea hadi ulipokuja kuanguka baada serikali kuingilia kati kutokana na matendo yaliyokua yakifanywa na mashabiki na wapenzi.
Isitoshe nimefanya documentary yangu binafsi kwa kuwatembelea na kuwahoji waliokua/na waliopo kwenye fani hiyo na hivyo kujikusanyia hazina ya kutosha kuhusu mziki huu.
Karibuni wapenzi wa mziki huu tubadilishane mawazo.
Nishakutumia namba mdau ya wsupKama bado una vitu unvyohitaji kuvijua/kuuliza kuhusu mnanda uwanja ni wetu mdau.Tujimwage ili tujuane na kuunda mtandao wa kuuenzi mziki huu.
Mudy black kiukweli ndiye mrithi wa Juma kwenyw kinanda(njia)lakini kiukweli baada ya Lupoz kufa watu walitawaliwa na umimi na kila mtu kujiona anajua.Akina Mudy black walianzisha bendi (Cash Money)maskani Kisemvule na Amadi Kiedu kageukia singeli.Akina Pailot watu wa juu kwa juu tu labda Nikupe namba za Captain Cholo boy yeye anaweza kujua wapi alipo maana ndie Seven Survivor master kwa sasa.Au tembelea maskani Stromberg steel pale Mbagala au Terminal unaweza kumgumia.amadi kiedu alikuwa 7 sasa wana kundi lao na mudy black....though muddy blacki alikuwa mpiga keyboard hatari, yuko wapi piloti baba isayaa?
"Kama miuda,kama midalala yote anaijua mdogo wake Kachala",hii ni baba Asha no.1.Baada ya mjumbe mzee Nanga kwenda kufichua siri nyumbani kwa Omary(baba Asha)kwamba usiku wa jana sungusungu hakulinda na wakati nyumbani aliaga kwamba anakwenda lindo,na hapo wakaleteana kashafa na vitambo(Band Atomic Music-Omary Omary).".......Kama miudaaaa,Kama midaladala yooote anaendesha mdogo wake kachalaaaaa......" huu ulikuwa wimbo gani?..
Enzi hizo tunaishi Temeke Mikoroshini maeneo ya Sandali kuna mahali panaitwa Tops mpaka leo kuna mateja, ndio mitaa unawakuta kina Omary Omary, Charles Tondo, Saidi Ndiga
Nakumbuka Saidi Ndiga alizinguana na anko wangu, basi walileteana mikwara baadae wakaishia kutaniana.
Anyway, hii ndude ilikuwa na vibe fulani hivi mtaani, ile mtu anaimbaaaa halafu ikichanganya unasikia kinanda tuu, hapo masela wanaruka kama wanacheza reggae.
Ujumbe,Vibes, ni muziki wenye mashabiki wengi wahuni ila hakuwa matusi kama miziki ya siku.
Ngoma yangu ya muda wote na hata sasa ninayo kwa simu ni ile, Kivuruge
"......mtazameni kivuruge alivyonyorodoka...., sasa umebaki tuu miguu kama fito.....
Marehemu dogo Jack Simela,alifariki kwa ajali ya gari pale round about ya Msamvu akitokea kwao kwenye msiba Mwembesongo Moro town.Hii imenifanya nidukue zaidi kuhusu mchiriku
Kumbe vijana wapya walipeperusha bendera
Tokea enzi za shule na ndomu kwa sana baada ya hapo sikufatilia kabisa mchiriku
Huyu Kijana Mungu amlaze pema peponi
Aliyaweza sana tena
Marehemu dogo Jack Simela,alifariki kwa ajali ya gari pale round about ya Msamvu akitokea kwao kwenye msiba Mwembesongo Moro town.
Hapo pande za Mwananyamala Ujiji kuna kupindi Hisani walikua wanafanya mazoezi hapo,kwa mzee wetu mmoja mtu wa kusini akiitwa Ally Matanga,wanae akina Baksijo,Mikidadi,Rajabu maarufu Awilo,walikua washkaji zao hao wapiga limba wa Gari kubwa (Meli ya sumu).Wakati huo ujanja ni "Kubembea"(Unga) na ukaribu huo ndio ulipelekea Hisani kukanyaga Kibaha mkoa wa Pwani kwa mara ya kwanza mwaka 92.Haaaaa mnanda ikishafika mida ya hatari vijana washavurugwa hiyo kumtoa mwali uzalamoni
Basi watagonga hii ngoma
"Watoto nyinyi ee
Kwanini hamsikii
Kila mnapoambiwa
Hamtaki kuelewa
Fujo mnatuletea
Kwenye shughuri za watu
Tunawaomba nyieeee....
Mnanda a.k.a 'GITA'
Ikipigwa live na debe lile na kisturi ndo utalielewa hasa ikiwa mtaani
Binafsi nimezaliwa kwa mama zakaria nimekulia
Ujiji manjunju kwa mzee manjunju ulipohasisiwa mnanda enzi Kina Mudy kadogo CHIDIDE wanakimbiza na HISAN MUSICA
Utatuambia nini GITA likifungwa shamba huku VANGA huku GITA hatari yqake si ya kitoto
Mpaka leo mpiga kinanda wa JAGWA wa sasa ni kakaangu BINAMU kwa ufupi mnanda umezaliwa baradhani mtaani kwetu chini ya BABU MZEE MANJUNJU mtaalamu wa kibao kata na chakachaa
Ila nimekubali namichiga we mdau haswa salute kwako
Mwenyewe ni mhanga wa hii, ilikua keko magurumbasi, nimesimama mbele ya mlango naangalia vitu, kurudi ndani wameshapita na radionasikia mlikua kila mkienda kupiga mziki mtaa huo lazima waibiwe