Niulize jambo lolote kuhusu mziki wa Mchiriku/Mnanda

Niulize jambo lolote kuhusu mziki wa Mchiriku/Mnanda

Mkama Shapu mdau mkubwa wa mchuliku.. Kile kikundi chake cha Mchiliku kilitwaje?

Hisani ngoma ilikiwa na mwimbaji wake wa kike, Aligongwa na gari asubuhi mitaa ya Faya, Kutokana na ile ajali wakatunga nyimbo uke mwimbo nimeusahau jina.. Unaitwaje? Kama uko nao tuwekee hapa...
Hussein Mwinyi sasa Rais Zanzibar alikuwa mdau mkubwa wa Hisani ngoma (Mchiliku) unakumbuka aliwahi kutungiwa nyimbo? Mbali na ule ya aliyotungiwa Baba yake Mzee Mwinyi kipindi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...

Mkuu huu mziki ni full masela.. Old is Nile..
Mkama Shapu huyu alikua ni askari polisi aliewahi kufanya kazi mitaa ya Temeke na baadae kituo cha Msimbazi kama sikosei,huyu alikua ni mdau mkubwa wa mziki wa mchiriku kwa wakati huo na bendi ya mwanzo maarufu kuipa saport ni bendi ya Night Star iliyokuwa chini ya Haidari Kesi.

Kuhusu bendi ya Hisani Gari kubwa iliyokuwa na maskani yake pale Mwananyamala Ujiji na ukaribu na familia ya Mwinyi hilo sina uhakika nalo sana, bali ninachokumbuka ni kuwa Hisani wao katika albam yao ya kwanza Hisani Garikubwa Vol.1 iliyotoka 1986 walimtunguia wimbo walioupa jina la #Ally Mwinyi(Nahodha wetu hodari) sababu nyakati hizo ndio katoka kuchukua hatamu za uongozi wa nchi mwaka 85.

Na kuhusu hili la msanii wao wa kike kufariki kwa ajali ya gari pale faya wacha nilifanyie kazi,sababu nina connection ya kutosha ya baadhi ya wasanii wa iliyokua bendi hiyo ambao bado wako hai,mfano aliewahi kuwa mpiga ngoma(Kulwa) ambae kwa sasa natambulika kama Sheshi Jr aliyo
 
wewe kweli ni shabiki wa mchiriku
Yeah ni kweli mdau,lakini kiuhalisia yatupasa sote tuupende mziki huu na kuufuatilia ili urudi kwenye peak,sababu ni mziki halisi kabisa wa Kitanzania uliobuniwa hapahapa nchini kwetu.Na isitoshe umesheheni mashairi murua na mazito yenye kuigusa jamii nzima ya Kitanzania,kilichouharibia mziki huu ni kundi la mashabiki vijana waliojawa na mihemko ya kiuni tu
 
Mimi ni mpz mkubwa wa Jagwa,ila jana usiku E FM walikuwa wanapiga ngoma za Chaukucha family kumbe nao ni wakali aisee,kuna ngoma moja wanasema dogo Jack Simela kuwa anafanya mchezo wa kurudi nyuma,iko pow sana,sijui inaitwaje
 
Mimi ni mpz mkubwa wa Jagwa,ila jana usiku E FM walikuwa wanapiga ngoma za Chaukucha family kumbe nao ni wakali aisee,kuna ngoma moja wanasema dogo Jack Simela kuwa anafanya mchezo wa kurudi nyuma,iko pow sana,sijui inaitwaje
Chaukucha family #Watoto wadogo waliokomaa vichwa( maskani ya Mwananyamala kwa Kopa) ni moja kati ya bendi zilizomaarufu sana kwenye tune ya mziki wa Kinondoni.Huku mwishoni kuna kundi la wasanii nguli na wakongwe walimeguka kutoka Jagwa Music kutokana na malumbano ya mgongano wa kimaslahi na kwenda kujiunga na Chaukucha(wengine walikulia humo kimuziki) na hatimaye kuzuka tungo tata na vijembe kwenye nyimbo zao.

Kuhusu hiyo nyimbo labda ungeukalili angalau ubeti mmoja ingekua rahisi kwangu kuutrack huo wimbo na kukutajia jina.
 
Mkuu Namichiga umenikumbusha mbali Sana. Mwaka 1996 mitaa ya Tandika Azimio,Dmaeks,Mashine ya Maji, Sandali nk.
Nashukuru kuishi kwenye haya mazingira na kutoka salama bila kuvuta sigara wala bangi au kukaba na mchana kupiga ndole ROAD..
Nashukuru basics za Karate zilinifanya niogopwe na kuwa huru kwenye mitaa ya kibishi ya Tandika.
 
Mkuu huwezi tengeneza link tukazipata hizi ngoma aisee...you tube zipo kwa uchache uchachee Sana...
Binafsi nimeahiriki Sana minara ya 7 survivor na Jagwaa enzi hizo wakati nikiwa Naishi Alimaua Campona Camp.
 
Mkuu
Mkuu huwezi tengeneza link tukazipata hizi ngoma aisee...you tube zipo kwa uchache uchachee Sana...
Binafsi nimeahiriki Sana minara ya 7 survivor na Jagwaa enzi hizo wakati nikiwa Naishi Alimaua Campona Camp.
Mkuu usijali maana niko mbioni kufanya kitu kama na wabobezi wenzangu wa tasnia ya mchiriku,itakayoambatana na Mchiriku Summit kitaifa.
 
Mkuu Namichiga umenikumbusha mbali Sana. Mwaka 1996 mitaa ya Tandika Azimio,Dmaeks,Mashine ya Maji, Sandali nk.
Nashukuru kuishi kwenye haya mazingira na kutoka salama bila kuvuta sigara wala bangi au kukaba na mchana kupiga ndole ROAD..
Nashukuru basics za Karate zilinifanya niogopwe na kuwa huru kwenye mitaa ya kibishi ya Tandika.
Yaani zile harakati fulani za kihuni ambazo zilitafsiriwa kama ndio ujanja kwa maisha ya level
 
Alietaka Kichwa Cha Nyoka by Jagwa huo hapoo
 
Jagwa Music,chini ya utawala wa marehemu baba J ndio ilipoanza kupata umaarufu mkubwa na hatimaye kuwa mrithi wa Hisani Gari kubwa pale Mwananyamala.Kila j'mosi watu wanaruka pale CCM Mwin'juma.
Mkuu @namachinga mpaka hivi Sasa kila Jumamos jagwa hua wanapiga hayo maeneo??
 
Yaah hao ni Atomic Music chini ya mafundi kama akina Omary Omary,Saidi Ndiga,Mwamkoto Ngoma,Nanga boy Simela(Wema Said Nanga) na wengineo.Hiyo Kipaka nyimbo inaitwa Kipaka Memory,wakati hiyo baba Asha in muendelezo kuanzia baba Asha no.1,2,3 na 4.

Mkuu, kwani wewe ku-upload hapa hizo nyimbo utaalamu huo huna au..?!

Nogesha Barza shekhe [emoji23][emoji120]!!
 
'...Sifa za uzuri wake e e Mwanaidi,
zafanana na tabia yake ee Mwanaidi,

Kwani kaumbika vema aah Mwanaidiii,
Tumsifu Aliyemuumba aah Mwanaidi,

Yaani kwa utaratibu uuh Mwanaidiii,
Kwa jinsi Alivyompamba aah Mwanaidiii..!

Ooh! Mwanaidiii yoooh Mwanaidiii!
Body lako linayumbayumbaa... Mwanaidi, waumiza roho za vijanaaa Mwanaidi
Malkia wa warembo Mwanaidi...


Nasikitika sikumbuki kundi wala mwamba aliyetiririka hiyo mistari.

Mnanda ilikuwa burudani ya kweli!
 
Ukiingiaa mitandaoo zipo zipo sio habaah ninaziona onaaa
IMG_20210519_091933.jpg
 
Nimeona hizi nyimbo zipo Apple music sijajua Kama wasanii waliopo wa Jagwa wananufaikaa nazo as Kuna malipo yanaingia kwa wanaosikilizaa
IMG_20210519_092424.jpg
 
'...Sifa za uzuri wake e e Mwanaidi,
zafanana na tabia yake ee Mwanaidi,

Kwani kaumbika vema aah Mwanaidiii,
Tumsifu Aliyemuumba aah Mwanaidi,

Yaani kwa utaratibu uuh Mwanaidiii,
Kwa jinsi Alivyompamba aah Mwanaidiii..!

Ooh! Mwanaidiii yoooh Mwanaidiii!
Body lako linayumbayumbaa... Mwanaidi, waumiza roho za vijanaaa Mwanaidi
Malkia wa warembo Mwanaidi...


Nasikitika sikumbuki kundi wala mwamba aliyetiririka hiyo mistari.

Mnanda ilikuwa burudani ya kweli!
Hao ni Hisani Gari kubwa( Meli ya sumu).
 
Mkuu @namachinga mpaka hivi Sasa kila Jumamos jagwa hua wanapiga hayo maeneo??
Hapana,Jagwa hawana Tena huo utamaduni wa kupiga kila juma mosi pale Mwinjuma.Sababu minanda hapa kati ilishuka trend
 
Back
Top Bottom