Zanzibar 2020 Njama? Mgombea wa Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, Maalim Seif awekewa Pingamizi

Zanzibar 2020 Njama? Mgombea wa Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, Maalim Seif awekewa Pingamizi

Hii ndio taarifa iliyotolewa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar kwa waandishi wa habari, huku ofisa wa Tume hiyo akionekana kuwa na uso wa bashasha jambo lililoashiria kufurahia pingamizi hilo, ameendelea kusisitiza uhalali wa pingamizi jambo lililoshangaza wengi.


Tuendelee kutega sikio kwa yatakayojiri .

======

View attachment 1565642
Sasa kulingana na hii fomu, hivi ilikuwa lazima ijazwe ile siku ya kurudisha hiyo fomu kwa tume au baada tu ya kuichukua ndani ya hizo siku walizopewa mtu anaweza kuijaza?

Pia naona kama jaji naye kaweka hiyo tarehe, je yeye hakuona hilo au halimuhusu yeye?
 
Maalim alipaswa kuwa preemptive kama lisu alivyofanya huku bara

Baada ya lisu kupata tetesi kwamba wanampango wa kumuwekea pingamizi akawaabarisha john naye ajiandae kukutana tume kutoa utetezi wake,wote tunajua nn kilitokea

Akina lipumba ambao waliandaliwa kwa kazi hiyo waliyeyuka kama barafu

The same na zenji angetishia kumuwekea pingamizi mwinyi haya yasingetokea,

Tusije kishangaa uchaguzi ukaishia hapo na mwinyi kupita bila kupingwa.

Ccm sio wa kucheka nao
Maalim alilisema hivo mbona kwenye mkutano wake na vijana wa ACT-Wazalendo. Aliwaataarifu siku kabla hajarudisha fomu kwamba kuna vyama viwili vilipangwa kuweka pingamizi na imetokea hivo kweli
 
Hii ndio taarifa iliyotolewa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar kwa waandishi wa habari, huku ofisa wa Tume hiyo akionekana kuwa na uso wa bashasha jambo lililoashiria kufurahia pingamizi hilo, ameendelea kusisitiza uhalali wa pingamizi jambo lililoshangaza wengi.


Tuendelee kutega sikio kwa yatakayojiri .

======

View attachment 1565642

Sasa nimeanza kukuelewa Hayati Benjamin Mkapa kuwa hawa watu ni wa ... na tena ni mslofa. Wenyewe wakiweka pungamizi ni haki, wanafuata sheria. Wakiwekewa wao eti ni njama, ama kweli zwazwa ni zwazwa na nyumbu ni nyumbu tu. Wangekuwa wao hawaweki mapungamizi basi. Wanayahalakisha wao wenyewe, wanalia wenyewe pia
 
Waliomuwekea pingamizi maalim Seif kuwa amekosea kujaza tarehe ya fomu kwa kujaza tarehe 7/7/2020 ni pingamizi la hoja ya uwongo.

Maalim Seif jinsi anavyoandika Saba anaikata katikati, kwa hiyo hoja ya kuwa amekosea kujaza tarehe ni hoja ya kihuni na ya kizushi!

ZEC iache michezo yake ya kutaka kuwanyima wazanzibar haki ya kuchagua wamtakaye

Hoja yenyewe ya sababu za pingamizi hii hapa kwenye video:




Na fomu yenyewe ya Maalim Seif hii hapa chini:

Seif Hamad Suleiman_20200911_2.jpg


Sasa swali la msingi ni

Hiyo Tarehe wanayosema kajaza Tarehe 7/7/2020 iko wapi kwenye hiyo fomu?
 
Viongozi wangu wa upinzani. Mkishajua kuwa mnatafutwa kwa udi na uvumba, punguzeni sababu za shetwani kuwavamia. Naona hata mwandiko wa mwapishwaji na mwapishaji uko sawa. Fomu imejazwa pote na mtu mmoja. Wino tu wa kalamu ndio umebadilishwa (mweusi na bluu). Maalim hawezi kujaza fomu mwenyewe ili kuepusha uwezekano wa "kuuzwa"?
Mkuu kuna kitu hapo hujaangalia kwa umakini. Unaposema Maalim kajaza kote siyosahihi. Amejaza maeneo yote yanayomuhusu. Hakimu kaanzia kwenye sehemu ya Hakimu aliyeshuhudia. Shida iko wapi hapo?
 
Jamani tuache ujinga.
Signature hazifanani , zote za Sharif na Muapaji
Dates forgerer kasahau, huku ni 07/09/2020, wakati forgerer kaweka 07/07/2020.
Mhuri ni ule ule lakini mlalo wake haulingani-huku kwenye date 2020 haijafunikwa , forgere kaigusa 2020.
Stupid games!!!
 
ZEC wanaweza kusema ile “T” kwenye ACT ni Transparency na sio Trasparency. Wanaweza kusema pia kifupi cha ACT sio ACTWAZALENDO bali ni ACT - WAZALENDO

Wana mbinu nyingi hawa watu. Wanaweza kumwambia pia jina lake sahihi ni SeifU SharifU HamadI😁

Maamuzi yatatoka Magogoni.... as always
 
Sometimes lengo huwa tu ni kuweka watu roho juu na si kitu kingine.

Kama ni kumuhujumu,watatumia mbinu nyingine lakini sio hii, lengo hapa ni kutaka kupima upepo na kuweka watu roho juu tu.
 
Kuna wagombea ubunge wa ACT waliandika jina la chama kama Maalim hapo "ACT Wazalendo". Wameenguliwa kwa kutokuweka "-" yaani "ACT-Wazalendo". Naona Maalim naye hakuweka hako ka-. Yaani hata mimi mkulima nilikwishajua kuwa kutokuweka hako ka - inaweza kuwa nongwa. Maalim bado hajajua tu?

IMG-20200911-WA0012.jpg
 
Waliomuwekea pingamizi maalim Seif kuwa amekosea kujaza tarehe ya fomu kwa kujaza tarehe 7/7/2020 ni pingamizi la hoja ya uwongo.

Maalim Seif jinsi anavyoandika Saba anaikata katikati, kwa hiyo hoja ya kuwa amekosea kujaza tarehe ni hoja ya kihuni na ya kizushi!

ZEC iache michezo yake ya kutaka kuwanyima wazanzibar haki ya kuchagua wamtakaye

Hoja yenyewe ya sababu za pingamizi hii hapa kwenye video:

View attachment 1565881


Na fomu yenyewe ya Maalim Seif hii hapa chini:

View attachment 1565884

Sasa swali la msingi ni

Hiyo Tarehe wanayosema kajaza Tarehe 7/7/2020 iko wapi kwenye hiyo fomu?
Ccm wanapima upepoo
 
Back
Top Bottom